< Galatians 6 >

1 Brethren, if a man be overtaken in a fault, ye which are spiritual, restore such an one in the spirit of meekness; considering thyself, lest thou also be tempted.
Ndugu, kama mkimwona mtu fulani amekosea, basi, ninyi mnaoongozwa na Roho mwonyeni mtu huyo ajirekebishe; lakini fanyeni hivyo kwa upole, mkiwa na tahadhari msije nanyi wenyewe mkajaribiwa.
2 Bear ye one another’s burdens, and so fulfil the law of Christ.
Saidianeni kubeba mizigo yenu na hivyo mtatimiza sheria ya Kristo.
3 For if a man think himself to be something, when he is nothing, he deceiveth himself.
Mtu akijiona kuwa ni kitu, na kumbe si kitu, huyo anajidanganya mwenyewe.
4 But let every man prove his own work, and then shall he have rejoicing in himself alone, and not in another.
Lakini kila mmoja na aupime vizuri mwenendo wake mwenyewe. Ukiwa mwema, basi, anaweza kuona fahari juu ya alichofanya bila kuwa na sababu ya kujilinganisha na mtu mwingine.
5 For every man shall bear his own burden.
Maana kila mmoja anao mzigo wake mwenyewe wa kubeba.
6 Let him that is taught in the word communicate unto him that teacheth in all good things.
Mwenye kufundishwa neno la Mungu na amshirikishe mwalimu wake riziki zake.
7 Be not deceived; God is not mocked: for whatsoever a man soweth, that shall he also reap.
Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna.
8 For he that soweth to his flesh shall of the flesh reap corruption; but he that soweth to the Spirit shall of the Spirit reap life everlasting. (aiōnios g166)
Apandaye katika tamaa za kidunia, atavuna humo uharibifu; lakini akipanda katika Roho, atavuna kutoka kwa Roho uzima wa milele. (aiōnios g166)
9 And let us not be weary in well doing: for in due season we shall reap, if we faint not.
Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake.
10 As we have therefore opportunity, let us do good unto all [men], especially unto them who are of the household of faith.
Kwa hiyo, tukiwa bado na wakati, tuwatendee watu wote mema, na hasa ndugu wa imani yetu.
11 Ye see how large a letter I have written unto you with mine own hand.
Tazameni jinsi nilivyoandika kwa herufi kubwa, kwa mkono wangu mwenyewe.
12 As many as desire to make a fair shew in the flesh, they constrain you to be circumcised; only lest they should suffer persecution for the cross of Christ.
Wale wanaotaka kuonekana wazuri kwa mambo ya mwili ndio wanaotaka kuwalazimisha ninyi mtahiriwe. Wanafanya hivyo kwa sababu moja tu: kusudi wao wenyewe wasije wakadhulumiwa kwa sababu ya msalaba wa Kristo.
13 For neither they themselves who are circumcised keep the law; but desire to have you circumcised, that they may glory in your flesh.
Maana, hao wenyewe waliotahiriwa hawaishiki Sheria; huwataka ninyi mtahiriwe wapate kujivunia alama hiyo mwilini mwenu.
14 But God forbid that I should glory, save in the cross of our Lord Jesus Christ, by whom the world is crucified unto me, and I unto the world.
Lakini mimi sitajivunia kamwe chochote isipokuwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo; maana kwa njia ya msalaba huo ulimwengu umesulubiwa kwangu, nami nimesulubiwa kwa ulimwengu.
15 For in Christ Jesus neither circumcision availeth any thing, nor uncircumcision, but a new creature.
Kutahiriwa au kutotahiriwa si kitu; cha maana ni kuwa kiumbe kipya.
16 And as many as walk according to this rule, peace [be] on them, and mercy, and upon the Israel of God.
Wanaoufuata mwongozo huo nawatakia amani na huruma; amani na huruma kwa Israeli—Wateule wa Mungu.
17 From henceforth let no man trouble me: for I bear in my body the marks of the Lord Jesus.
Basi, sasa mtu yeyote asinisumbue tena, maana alama nilizo nazo mwilini mwangu ni zile za Yesu.
18 Brethren, the grace of our Lord Jesus Christ [be] with your spirit. Amen.
Ndugu, nawatakieni ninyi nyote neema ya Bwana wetu Kristo. Amina.

< Galatians 6 >