< Ephesians 5 >

1 Be ye therefore followers of God, as dear children;
Kwa hiyo, mwigeni Mungu, maana ninyi ni watoto wake wapenzi.
2 And walk in love, as Christ also hath loved us, and hath given himself for us an offering and a sacrifice to God for a sweetsmelling savour.
Upendo uongoze maisha yenu, kama vile Kristo alivyotupenda, na kwa ajili yetu akajitoa mwenyewe kama dhabihu yenye harufu nzuri na tambiko impendezayo Mungu.
3 But fornication, and all uncleanness, or covetousness, let it not be once named among you, as becometh saints;
Kwa vile ninyi ni watu wa Mungu, basi uasherati, uchafu wowote ule au choyo visitajwe kamwe miongoni mwenu.
4 Neither filthiness, nor foolish talking, nor jesting, which are not convenient: but rather giving of thanks.
Tena maneno ya aibu, ya upuuzi au ubishi, yote hayo hayafai kwenu; maneno ya kumshukuru Mungu ndiyo yanayofaa.
5 For this ye know, that no whoremonger, nor unclean person, nor covetous man, who is an idolater, hath any inheritance in the kingdom of Christ and of God.
Jueni wazi kwamba mwasherati yeyote au mchafu au mfisadi, (ufisadi ni sawa na kuabudu sanamu), au mtu yeyote wa aina hiyo hataambulia chochote katika Utawala wa Kristo na wa Mungu.
6 Let no man deceive you with vain words: for because of these things cometh the wrath of God upon the children of disobedience.
Msikubali kudanganywa na mtu kwa maneno matupu; maana, kwa sababu ya mambo kama hayo ghadhabu ya Mungu huwajia wote wasiomtii.
7 Be not ye therefore partakers with them.
Basi, msishirikiane nao.
8 For ye were sometimes darkness, but now [are ye] light in the Lord: walk as children of light:
Zamani ninyi mlikuwa gizani, lakini sasa ninyi mko katika mwanga kwa kuungana na Bwana. Ishini kama watoto wa mwanga:
9 (For the fruit of the Spirit [is] in all goodness and righteousness and truth; )
maana matokeo ya mwanga ni wema kamili, uadilifu na ukweli.
10 Proving what is acceptable unto the Lord.
Jaribuni kujua yale yanayompendeza Bwana.
11 And have no fellowship with the unfruitful works of darkness, but rather reprove [them].
Msishiriki katika matendo yasiyofaa, ya giza bali yafichueni.
12 For it is a shame even to speak of those things which are done of them in secret.
Mambo yanayotendwa kwa siri ni aibu hata kuyataja.
13 But all things that are reproved are made manifest by the light: for whatsoever doth make manifest is light.
Lakini mambo yale yanayotendwa katika mwanga, ukweli wake hudhihirishwa;
14 Wherefore he saith, Awake thou that sleepest, and arise from the dead, and Christ shall give thee light.
na kila kilichodhihirishwa huwa mwanga. Ndiyo maana Maandiko yasema: “Amka wewe uliyelala, fufuka kutoka wafu, naye Kristo atakuangaza.”
15 See then that ye walk circumspectly, not as fools, but as wise,
Basi, muwe waangalifu jinsi mnavyoishi: Msiishi kama wapumbavu, bali kama wenye hekima.
16 Redeeming the time, because the days are evil.
Tumieni vizuri muda mlio nao maana siku hizi ni mbaya.
17 Wherefore be ye not unwise, but understanding what the will of the Lord [is].
Kwa hiyo, msiwe wapumbavu, bali jaribuni kujua matakwa ya Bwana.
18 And be not drunk with wine, wherein is excess; but be filled with the Spirit;
Acheni kulewa divai maana hiyo itawaangamiza, bali mjazwe Roho Mtakatifu.
19 Speaking to yourselves in psalms and hymns and spiritual songs, singing and making melody in your heart to the Lord;
Zungumzeni kwa maneno ya Zaburi, nyimbo na tenzi za kiroho; mwimbieni Bwana nyimbo na zaburi kwa shukrani mioyoni mwenu.
20 Giving thanks always for all things unto God and the Father in the name of our Lord Jesus Christ;
Mshukuruni Mungu Baba daima kwa ajili ya yote, kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo.
21 Submitting yourselves one to another in the fear of God.
Kila mmoja amstahi mwenzake kwa sababu ya kumcha Kristo.
22 Wives, submit yourselves unto your own husbands, as unto the Lord.
Wake wawatii waume zao kama kumtii Bwana.
23 For the husband is the head of the wife, even as Christ is the head of the church: and he is the saviour of the body.
Maana mume anayo mamlaka juu ya mkewe, kama vile Kristo alivyo na mamlaka juu ya kanisa; naye Kristo mwenyewe hulikomboa kanisa, mwili wake.
24 Therefore as the church is subject unto Christ, so [let] the wives [be] to their own husbands in every thing.
Kama vile kanisa linavyomtii Kristo, vivyo hivyo, wake wawatii waume zao katika mambo yote.
25 Husbands, love your wives, even as Christ also loved the church, and gave himself for it;
Nanyi waume, wapendeni wake zenu kama Kristo alivyolipenda kanisa, akajitoa mwenyewe sadaka kwa ajili yake.
26 That he might sanctify and cleanse it with the washing of water by the word,
Alifanya hivyo, ili kwa neno lake, aliweke wakfu kwa Mungu, baada ya kulifanya safi kwa kuliosha katika maji,
27 That he might present it to himself a glorious church, not having spot, or wrinkle, or any such thing; but that it should be holy and without blemish.
kusudi ajipatie kanisa lililo takatifu na safu kabisa, kanisa lisilo na doa, kasoro au chochote cha namna hiyo.
28 So ought men to love their wives as their own bodies. He that loveth his wife loveth himself.
Basi, waume wanapaswa kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe.
29 For no man ever yet hated his own flesh; but nourisheth and cherisheth it, even as the Lord the church:
(Hakuna mtu yeyote auchukiaye mwili wake; badala ya kuuchukia, huulisha na kuuvika. Ndivyo naye Kristo anavyolitunza kanisa,
30 For we are members of his body, of his flesh, and of his bones.
maana sisi ni viungo vya mwili wake.)
31 For this cause shall a man leave his father and mother, and shall be joined unto his wife, and they two shall be one flesh.
Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja.”
32 This is a great mystery: but I speak concerning Christ and the church.
Kuna ukweli uliofichika katika maneno haya, nami naona kwamba yamhusu Kristo na kanisa lake.
33 Nevertheless let every one of you in particular so love his wife even as himself; and the wife [see] that she reverence [her] husband.
Lakini yanawahusu ninyi pia: kila mume lazima ampende mkewe kama nafsi yake mwenyewe, naye mke anapaswa kumstahi mumewe.

< Ephesians 5 >