< Colossians 4 >

1 Masters, give unto [your] servants that which is just and equal; knowing that ye also have a Master in heaven.
Nanyi wakuu, watendeeni watumwa wenu kwa uadilifu na haki, mkikumbuka kwamba nanyi pia mnaye Bwana mbinguni.
2 Continue in prayer, and watch in the same with thanksgiving;
Dumuni katika sala, na mnaposali muwe waangalifu, mkimshukuru Mungu.
3 Withal praying also for us, that God would open unto us a door of utterance, to speak the mystery of Christ, for which I am also in bonds:
Vilevile, mtuombee sisi pia ili Mungu atupe fursa ya kuuhubiri ujumbe wake kuhusu siri ya Kristo. Kwa ajili hiyo mimi niko sasa kifungoni.
4 That I may make it manifest, as I ought to speak.
Basi, ombeni ili niweze kusema kama inavyonipasa na kwa namna itakayodhihirisha siri hiyo.
5 Walk in wisdom toward them that are without, redeeming the time.
Muwe na hekima katika uhusiano wenu na watu wasioamini, mkitumia vizuri kila nafasi mliyo nayo.
6 Let your speech [be] alway with grace, seasoned with salt, that ye may know how ye ought to answer every man.
Mazungumzo yenu yanapaswa kuwa daima mema na ya kuvutia, na mnapaswa kujua jinsi ya kumjibu vizuri kila mmoja.
7 All my state shall Tychicus declare unto you, [who is] a beloved brother, and a faithful minister and fellowservant in the Lord:
Ndugu yetu mpenzi Tukiko, mfanyakazi mwaminifu na mtumishi mwenzetu katika kazi ya Bwana, atawapeni habari zangu zote.
8 Whom I have sent unto you for the same purpose, that he might know your estate, and comfort your hearts;
Ndiyo maana namtuma, ili aichangamshe mioyo yenu kwa kuwaambieni habari zetu.
9 With Onesimus, a faithful and beloved brother, who is [one] of you. They shall make known unto you all things which [are done] here.
Anakuja pamoja na Onesimo, ndugu yetu mpenzi na mwaminifu, ambaye ni mwananchi mwenzenu. Watawapeni habari za mambo yote yanayofanyika hapa.
10 Aristarchus my fellowprisoner saluteth you, and Marcus, sister’s son to Barnabas, (touching whom ye received commandments: if he come unto you, receive him; )
Aristarko, ambaye yuko kifungoni pamoja nami, anawasalimuni; hali kadhalika Marko, binamu yake Barnaba, (mmekwisha pata maagizo juu yake; akifika kwenu mkaribisheni).
11 And Jesus, which is called Justus, who are of the circumcision. These only [are my] fellowworkers unto the kingdom of God, which have been a comfort unto me.
Naye Yoshua aitwaye Yusto, anawasalimuni. Miongoni mwa Wayahudi waliokwisha pokea imani, hawa tu peke yao, ndio wanaofanya kazi pamoja nami kwa ajili ya Utawala wa Mungu; nao wamekuwa msaada mkubwa kwangu.
12 Epaphras, who is [one] of you, a servant of Christ, saluteth you, always labouring fervently for you in prayers, that ye may stand perfect and complete in all the will of God.
Epafra, mwananchi mwenzenu na mtumishi wa Kristo Yesu anawasalimuni. Daima anawaombeeni ninyi kwa bidii ili mpate kusimama imara, mkomae na kuwa thabiti kabisa katika mambo yote anayotaka Mungu.
13 For I bear him record, that he hath a great zeal for you, and them [that are] in Laodicea, and them in Hierapolis.
Naweza kushuhudia kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu na kwa ajili ya watu wa Laodikea na Hierapoli.
14 Luke, the beloved physician, and Demas, greet you.
Luka, daktari wetu mpenzi, na Dema, wanawasalimuni.
15 Salute the brethren which are in Laodicea, and Nymphas, and the church which is in his house.
Salamu zetu kwa ndugu zetu wa Laodikea; msalimuni dada Nimfa pamoja na jumuiya yote ya waumini inayokutana nyumbani kwake.
16 And when this epistle is read among you, cause that it be read also in the church of the Laodiceans; and that ye likewise read the [epistle] from Laodicea.
Mkisha soma barua hii, hakikisheni kwamba inasomwa na Wakristo wa Laodikea; na ninyi fanyeni mpango mpate kuisoma barua waliyoipata kwao.
17 And say to Archippus, Take heed to the ministry which thou hast received in the Lord, that thou fulfil it.
Mwambieni Arkipo aitekeleze vizuri ile huduma aliyokabidhiwa na Bwana.
18 The salutation by the hand of me Paul. Remember my bonds. Grace [be] with you. Amen.
Naandika haya kwa mkono wangu mwenyewe: Salamu kutoka kwangu, mimi Paulo. Kumbukeni kwamba niko kifungoni. Neema ya Mungu iwe nanyi.

< Colossians 4 >