< 2 John 1 >

1 The elder unto the elect lady and her children, whom I love in the truth; and not I only, but also all they that have known the truth;
Mimi Mzee nakuandikia wewe Bimkubwa mteule, pamoja na watoto wako ninaowapenda kweli. Wala si mimi tu ninayewapenda, bali pia wote wanaoujua ule ukweli wanawapenda ninyi,
2 For the truth’s sake, which dwelleth in us, and shall be with us for ever. (aiōn g165)
kwa sababu ukweli unakaa nasi milele. (aiōn g165)
3 Grace be with you, mercy, [and] peace, from God the Father, and from the Lord Jesus Christ, the Son of the Father, in truth and love.
Neema na huruma na amani zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Yesu Kristo, Mwana wa Baba, zitakuwa pamoja nasi katika ukweli na upendo.
4 I rejoiced greatly that I found of thy children walking in truth, as we have received a commandment from the Father.
Nilifurahi sana kuona kwamba baadhi ya watoto wako wanaishi katika ukweli kama Baba alivyotuamuru.
5 And now I beseech thee, lady, not as though I wrote a new commandment unto thee, but that which we had from the beginning, that we love one another.
Basi, Bimkubwa, ninalo ombi moja kwako: tupendane. Ombi hili si amri mpya, bali ni amri ileile tuliyokuwa nayo tangu mwanzo.
6 And this is love, that we walk after his commandments. This is the commandment, That, as ye have heard from the beginning, ye should walk in it.
Upendo maana yake ni kuishi kwa kuzitii amri zake Mungu. Amri niliyoisikia tangu mwanzo ndiyo hii: mnapaswa nyote kuishi katika upendo.
7 For many deceivers are entered into the world, who confess not that Jesus Christ is come in the flesh. This is a deceiver and an antichrist.
Wadanganyifu wengi wamezuka duniani, watu ambao hawakiri kwamba Yesu Kristo amekuja kwetu akawa binadamu. Mtu asemaye hivyo ni mdanganyifu na ni Adui wa Kristo.
8 Look to yourselves, that we lose not those things which we have wrought, but that we receive a full reward.
Basi, jihadharini ninyi wenyewe ili msije mkapoteza kile mlichokishugulikia, bali mpate tuzo lenu kamili.
9 Whosoever transgresseth, and abideth not in the doctrine of Christ, hath not God. He that abideth in the doctrine of Christ, he hath both the Father and the Son.
Asiyezingatia na kudumu katika mafundisho ya Kristo, bali anayakiuka, hana Mungu. Lakini anayedumu katika mafundisho hayo anaye Baba na Mwana.
10 If there come any unto you, and bring not this doctrine, receive him not into [your] house, neither bid him God speed:
Basi, kama mtu akija kwenu bila kuwaleteeni mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani kwenu, wala msimsalimu.
11 For he that biddeth him God speed is partaker of his evil deeds.
Maana anayemsalimu mtu huyo, anashirikiana naye katika matendo yake maovu.
12 Having many things to write unto you, I would not [write] with paper and ink: but I trust to come unto you, and speak face to face, that our joy may be full.
Ninayo mengi ya kuwaambieni lakini sipendi kufanya hivyo kwa karatasi na wino; badala yake, natumaini kuwatembeleeni na kuzungumza nanyi ana kwa ana, ili furaha yetu ikamilike.
13 The children of thy elect sister greet thee. Amen.
Watoto wa dada yako mteule wanakusalimu.

< 2 John 1 >