< 2 Corinthians 2 >

1 But I determined this with myself, that I would not come again to you in heaviness.
Basi nimeamua nisiwatembelee tena kuwatia huzuni.
2 For if I make you sorry, who is he then that maketh me glad, but the same which is made sorry by me?
Maana nikiwahuzunisha ninyi, basi, ni nani atakayenifariji? Ni walewale niliowahuzunisha!
3 And I wrote this same unto you, lest, when I came, I should have sorrow from them of whom I ought to rejoice; having confidence in you all, that my joy is [the joy] of you all.
Ndiyo maana niliwaandikia—sikutaka kuja kwenu na kuhuzunishwa na ninyi ambao ndio mngepaswa kuwa furaha yangu. Nina hakika kwamba, mimi nikifurahi, ninyi nyote pia mnafurahi.
4 For out of much affliction and anguish of heart I wrote unto you with many tears; not that ye should be grieved, but that ye might know the love which I have more abundantly unto you.
Nilipowaandikia hapo awali katika hali ya huzuni na sikitiko moyoni na kwa machozi mengi, haikuwa kwa ajili ya kuwahuzunisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwaonyesheni kwamba nawapenda mno.
5 But if any have caused grief, he hath not grieved me, but in part: that I may not overcharge you all.
Ikiwa kuna mtu aliyemhuzunisha mwingine, hakunihuzunisha mimi—ila amewahuzunisha ninyi nyote, na sipendi kuwa mkali zaidi.
6 Sufficient to such a man [is] this punishment, which [was inflicted] of many.
Adhabu aliyokwisha pata kutoka kwa wengi wenu inamtosha.
7 So that contrariwise ye [ought] rather to forgive [him], and comfort [him], lest perhaps such a one should be swallowed up with overmuch sorrow.
Iliyobakia ni afadhali kwenu kumsamehe mtu huyo na kumpa moyo ili asije akahuzunika mno na kukata tamaa kabisa.
8 Wherefore I beseech you that ye would confirm [your] love toward him.
Kwa hiyo nawasihi: mwonyesheni kwamba mnampenda.
9 For to this end also did I write, that I might know the proof of you, whether ye be obedient in all things.
Madhumuni yangu kuandika ile barua yalikuwa kutaka kujua kama mko tayari kutii katika kila jambo.
10 To whom ye forgive any thing, I [forgive] also: for if I forgave any thing, to whom I forgave [it], for your sakes [forgave I it] in the person of Christ;
Mkimsamehe mtu, nami pia ninamsamehe. Maana ninaposamehe—kama kweli ninacho cha kusamehe—nasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
11 Lest Satan should get an advantage of us: for we are not ignorant of his devices.
ili tusimpe nafasi Shetani atudanganye; maana twaijua mipango yake ilivyo.
12 Furthermore, when I came to Troas to [preach] Christ’s gospel, and a door was opened unto me of the Lord,
Nilipofika Troa kuhubiri Habari Njema ya Kristo, nilikuta mlango u wazi kwa ajili ya kazi ya Bwana.
13 I had no rest in my spirit, because I found not Titus my brother: but taking my leave of them, I went from thence into Macedonia.
Lakini nilifadhaika sana kwa kutomkuta ndugu yetu Tito. Ndiyo maana niliwaaga wote pale nikaenda Makedonia.
14 Now thanks [be] unto God, which always causeth us to triumph in Christ, and maketh manifest the savour of his knowledge by us in every place.
Lakini, shukrani kwa Mungu anayetuongoza daima katika msafara wa ushindi wa Kristo. Yeye hutufanya tuueneze ukweli wa Kristo kama harufu nzuri, kila mahali.
15 For we are unto God a sweet savour of Christ, in them that are saved, and in them that perish:
Maana sisi ni kama harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mungu, harufu nzuri inayofikia wote wanaookolewa na wanaopotea.
16 To the one [we are] the savour of death unto death; and to the other the savour of life unto life. And who [is] sufficient for these things?
Kwa wale wanaopotea, harufu hiyo ni kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, harufu hiyo ni uhai. Nani basi, awezaye kushiriki katika kazi ya namna hiyo?
17 For we are not as many, which corrupt the word of God: but as of sincerity, but as of God, in the sight of God speak we in Christ.
Sisi si kama wengine ambao hufanya biashara na ujumbe wa Mungu; sisi tunahubiri kwa unyofu mbele ya Mungu, kama watu tuliotumwa na Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo.

< 2 Corinthians 2 >