< Exodus 20 >

1 And God spoke all these words, saying,
Ndipo Mungu akasema maneno haya yote:
2 I am the LORD your God, which have brought you out of the land of Egypt, out of the house of bondage.
“Mimi ndimi Bwana Mungu wako, niliyekutoa Misri, kutoka nchi ya utumwa.
3 You shall have no other gods before me.
Usiwe na miungu mingine ila mimi.
4 You shall not make unto you any graven image, or any likeness of any thing that is in heaven above, or that is in the earth beneath, or that is in the water under the earth.
Usijitengenezee sanamu katika umbo la kitu chochote kilicho juu mbinguni, au duniani chini, au ndani ya maji.
5 You shall not bow down yourself to them, nor serve them: for I the LORD your God am a jealous God, visiting the iniquity of the fathers upon the children unto the third and fourth generation of them that hate me;
Usivisujudie wala kuviabudu; kwa kuwa Mimi, Bwana Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu, ninayewaadhibu watoto kwa ajili ya dhambi za baba zao hadi kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,
6 And showing mercy unto thousands of them that love me, and keep my commandments.
lakini ninaonyesha upendo kwa maelfu ya vizazi vya wale wanipendao na kuzishika amri zangu.
7 You shall not take the name of the LORD your God in vain; for the LORD will not hold him guiltless that takes his name in vain.
Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako, kwa kuwa Bwana hataacha kumhesabia hatia yeye alitajaye jina lake bure.
8 Remember the sabbath day, to keep it holy.
Ikumbuke siku ya Sabato, uitakase.
9 Six days shall you labour, and do all your work:
Kwa siku sita utafanya kazi na kutenda shughuli zako zote,
10 But the seventh day is the sabbath of the LORD your God: in it you shall not do any work, you, nor your son, nor your daughter, your manservant, nor your maidservant, nor your cattle, nor your stranger that is within your gates:
lakini siku ya saba ni Sabato kwa Bwana Mungu wako. Siku hiyo hutafanya kazi yoyote, wewe, wala mwanao au binti yako, wala mtumishi wako wa kiume au wa kike, wala wanyama wako, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.
11 For in six days the LORD made heaven and earth, the sea, and all that in them is, and rested the seventh day: wherefore the LORD blessed the sabbath day, and hallowed it.
Kwa kuwa kwa siku sita, Bwana aliumba mbingu na nchi, bahari na vyote vilivyomo, lakini akapumzika siku ya saba. Kwa hiyo Bwana akaibariki siku ya Sabato na kuifanya takatifu.
12 Honour your father and your mother: that your days may be long upon the land which the LORD your God gives you.
Waheshimu baba yako na mama yako, ili upate kuishi siku nyingi katika nchi anayokupa Bwana Mungu wako.
13 You shall not kill.
Usiue.
14 You shall not commit adultery.
Usizini.
15 You shall not steal.
Usiibe.
16 You shall not bear false witness against your neighbour.
Usimshuhudie jirani yako uongo.
17 You shall not covet your neighbour's house, you shall not covet your neighbour's wife, nor his manservant, nor his maidservant, nor his ox, nor his ass, nor any thing that is your neighbour's.
Usiitamani nyumba ya jirani yako. Usimtamani mke wa jirani yako, wala mtumishi wake wa kiume au wa kike, wala ngʼombe wake au punda wake, wala chochote kile alicho nacho jirani yako.”
18 And all the people saw the thunderings, and the lightnings, and the noise of the trumpet, and the mountain smoking: and when the people saw it, they removed, and stood far off.
Watu walipoona ngurumo na radi, na kusikia mlio wa tarumbeta, na kuuona mlima katika moshi, walitetemeka kwa woga. Wakasimama mbali
19 And they said unto Moses, Speak you with us, and we will hear: but let not God speak with us, lest we die.
na wakamwambia Mose, “Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini usimwache Mungu aseme nasi, la sivyo tutakufa.”
20 And Moses said unto the people, Fear not: for God has come to prove you, and that his fear may be before your faces, that all of you sin not.
Mose akawaambia watu, “Msiogope! Mungu amekuja kuwajaribu, ili kwamba hofu ya Mungu iwakalie, msitende dhambi.”
21 And the people stood far off, and Moses drew near unto the thick darkness where God was.
Watu wakabaki mbali, wakati Mose alipolisogelea lile giza nene mahali pale Mungu alipokuwa.
22 And the LORD said unto Moses, Thus you shall say unto the children of Israel, All of you have seen that I have talked with you from heaven.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Waambie Waisraeli hivi: ‘Mmejionea wenyewe kwamba nimesema nanyi kutoka mbinguni:
23 All of you shall not make with me gods of silver, neither shall all of you make unto you gods of gold.
Msijifanyizie miungu yoyote na kuilinganisha nami, msijitengenezee miungu ya fedha wala miungu ya dhahabu.
24 An altar of earth you shall make unto me, and shall sacrifice thereon your burnt offerings, and your peace offerings, your sheep, and your oxen: in all places where I record my name I will come unto you, and I will bless you.
“‘Utanitengenezea madhabahu ya udongo, na juu yake utoe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani, kondoo zako, mbuzi na ngʼombe zako. Popote nitakapofanya Jina langu liheshimiwe, nitakuja kwenu na kuwabariki.
25 And if you will make me an altar of stone, you shall not build it of hewn stone: for if you lift up your tool upon it, you have polluted it.
Ikiwa unanitengenezea madhabahu ya mawe, usiijenge kwa mawe ya kuchonga, maana mkitumia chombo cha kuchongea mtaitia unajisi.
26 Neither shall you go up by steps unto mine altar, that your nakedness be not discovered thereon.
Msitumie ngazi kupandia kwenye madhabahu yangu, uchi wako usije ukadhihirika kwa chini.’

< Exodus 20 >