< 1 Samuel 2 >

1 Hannah prayed, “I'm so happy in the Lord! He has empowered me! Now I have plenty to say in answer to those who hate me. I celebrate your salvation!
Kisha Hana akaomba na kusema: “Moyo wangu wamshangilia Bwana, katika Bwana pembe yangu imeinuliwa juu. Kinywa changu chajisifu juu ya adui zangu, kwa kuwa naufurahia wokovu wako.
2 There's no one holy like the Lord—no one apart from you, no Rock like our God!
“Hakuna yeyote aliye mtakatifu kama Bwana, hakuna mwingine zaidi yako; hakuna Mwamba kama Mungu wetu.
3 Don't speak so conceitedly! Don't talk so arrogantly! For the Lord is a God who knows everything—doesn't he judge what you do?
“Msiendelee kusema kwa kiburi hivyo wala msiache vinywa vyenu kunena kwa kiburi, kwa kuwa Bwana ndiye Mungu ajuaye, na kwa yeye matendo hupimwa.
4 The weapons of the powerful are shattered, while those who stumble along are made strong.
“Pinde za mashujaa zimevunjika, lakini wale wanaojikwaa wamevikwa nguvu.
5 Those who used to have plenty of food now have to work to earn a crust, while those who used to be hungry now have become fat. The woman who was childless now has seven children, while the woman with many children fades away.
Wale waliokuwa na chakula tele wamejikodisha wenyewe ili kupata chakula, lakini wale waliokuwa na njaa hawana njaa tena. Mwanamke yule aliyekuwa tasa amezaa watoto saba, lakini yule ambaye alikuwa na wana wengi amedhoofika.
6 The Lord kills and he revives; he sends some down to the grave, but he raises others up. (Sheol h7585)
“Bwana huua na huleta uhai, hushusha chini mpaka kaburini na hufufua. (Sheol h7585)
7 The Lord makes some poor, but others rich; he brings some down, but he lifts others up.
Bwana humfanya mtu maskini naye hutajirisha, hushusha na hukweza.
8 He helps the poor up from the dust; he raises the lowborn from the trash pile and seats them with the upper class in places of honor. For the foundations of the earth belong to the Lord, and he has placed the world on them.
Humwinua maskini kutoka mavumbini na humwinua mhitaji kutoka lundo la majivu; huwaketisha pamoja na wakuu na kuwafanya warithi kiti cha enzi cha heshima. “Kwa kuwa misingi ya dunia ni ya Bwana; juu yake ameuweka ulimwengu.
9 He will take care of those who trust him, but the wicked vanish into the darkness, for people don't succeed through their own strength.
Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake, lakini waovu watanyamazishwa kwenye giza. “Si kwa nguvu mtu hushinda;
10 The Lord crushes his enemies, he thunders against them from heaven. He rules the whole earth; he strengthens his king, and gives power to the one he has anointed.”
wale wampingao Bwana wataharibiwa kabisa. Atapiga radi dhidi yao kutoka mbinguni; Bwana ataihukumu miisho ya dunia. “Atampa nguvu mfalme wake, na kuitukuza pembe ya mpakwa mafuta wake.”
11 Then Elkanah went home to Ramah while the boy stayed with Eli the priest serving the Lord.
Kisha Elikana akaenda nyumbani Rama, lakini mtoto akahudumu mbele za Bwana chini ya kuhani Eli.
12 Eli's sons were worthless men who didn't have any time for the Lord
Wana wa Eli walikuwa watu wabaya kabisa, hawakumheshimu Bwana.
13 or their role as priests to the people. They would send one of their servants over with a fork when anyone came to offer a sacrifice.
Basi ilikuwa desturi ya makuhani pamoja na watu kwamba kila mara yeyote anapotoa dhabihu na huku nyama ikiwa inachemshwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na uma wenye meno matatu mkononi mwake.
14 The servant would stick the fork into the pot while the meat from the sacrifice was being boiled, and would take whatever meat came up on the fork to Eli's sons. This is how they treated all the Israelites who came to Shiloh.
Angeutumbukiza huo uma kwenye sufuria au birika au sufuria kubwa au chungu, naye kuhani angalijichukulia mwenyewe chochote ambacho uma ungekileta. Hivi ndivyo walivyowatendea Waisraeli wote waliokuja Shilo.
15 In fact even before the fat of the sacrifice was burned up the servant would come and would demand from the man sacrificing, “Give me meat to roast for the priest. He doesn't want boiled meat from you—he wants it raw.”
Lakini hata kabla mafuta ya mnyama hayajachomwa, mtumishi wa kuhani angalikuja na kusema kwa mtu ambaye alikuwa akitoa dhabihu, “Mpe kuhani nyama akaoke, kwani hatapokea nyama iliyochemshwa kutoka kwako, ila iliyo mbichi tu.”
16 The man might answer, “Let me first burn up all the fat, and then you can have as much as you want.” But the priest's servant would reply, “No, you must give it to me now. If you don't, I'll take it by force.”
Kama mtu akimwambia, “Mafuta ya mnyama na yachomwe kwanza, ndipo uchukue chochote unachotaka,” mtumishi angalijibu, “Hapana, nipe sasa, kama huwezi nitaichukua kwa nguvu.”
17 The sins of these young men were extremely serious from the Lord's perspective because they were treating with contempt the Lord's offerings.
Hii Dhambi ya hawa vijana ilikuwa kubwa sana machoni pa Bwana, kwa kuwa waliitendea dhabihu ya Bwana kwa dharau.
18 But Samuel served before the Lord—a boy dressed as a priest, wearing a linen ephod.
Lakini Samweli alikuwa akihudumu mbele za Bwana, kijana akivaa kisibau cha kitani.
19 Every year his mother made him a little robe and took it to him when she went with her husband to offer the annual sacrifice.
Kila mwaka mama yake alimshonea joho dogo na kumchukulia wakati alipokwea pamoja na mumewe kutoa dhabihu ya mwaka.
20 Eli would bless Elkanah and his wife, saying, “May the Lord give you children by this woman to replace the one she prayed for and dedicated to the Lord.” Then they would return home.
Eli alikuwa akiwabariki Elikana na mkewe, akisema, “Bwana na akupe watoto kwa mwanamke huyu ili kuchukua nafasi ya yule aliyekuwa amemwomba na akamtoa kwa Bwana.” Kisha wakawa wanakwenda nyumbani.
21 The Lord blessed Hannah with three sons and two daughters. The boy Samuel grew up in the presence of the Lord.
Bwana akawa mwenye neema kwa Hana, naye akapata mimba akazaa wana watatu na binti wawili. Wakati huo, kijana Samweli akaendelea kukua mbele za Bwana.
22 Eli was very old, however he had heard about all the things his sons were doing to the people of Israel, and how they were seducing the women who were serving at the entrance to the Tent of Meeting.
Basi Eli, ambaye alikuwa mzee sana, alisikia kuhusu kila kitu ambacho wanawe walikuwa wakiwafanyia Israeli wote na jinsi walivyokutana kimwili na wanawake waliohudumu kwenye ingilio la Hema la Kukutania.
23 He asked them, “Why are you doing all this? I keep on hearing from everyone about your evil actions.
Hivyo akawaambia, “Kwa nini mmefanya mambo kama haya? Nimesikia kutoka kwa watu wote juu ya haya matendo yenu maovu.
24 No, my sons, the report I hear about you from the Lord's people isn't good.
Sivyo, wanangu, hii si habari nzuri ambayo ninasikia ikienea miongoni mwa watu wa Bwana.
25 If a man sins against someone, God can intercede for him; but if a man sin against the Lord, who is going to intercede for him?” But they didn't pay attention to what their father said, for the Lord was planning to put them to death.
Kama mtu akifanya dhambi dhidi ya mtu mwenzake, mtu mwingine aweza kumwombea kwa Mungu, lakini kama mtu akimfanyia Mungu dhambi, ni nani atakayemwombea?” Hata hivyo wanawe hawakusikia maonyo ya baba yao, kwa sababu Bwana alitaka kuwaua.
26 The boy Samuel grew physically, and also grew in the approval of both the Lord and the people.
Naye kijana Samweli akaendelea kukua katika kimo, akimpendeza Bwana na wanadamu.
27 A man of God came to Eli and told him, “This is what the Lord says: Didn't I very clearly reveal myself to your forefather's family when they were ruled by Pharaoh in Egypt?
Basi mtu wa Mungu akaja kwa Eli na kumwambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Je, sikujifunua waziwazi kwa nyumba ya baba yako wakati walikuwa huko Misri chini ya Farao?
28 I chose him out of all the tribes of Israel as my priest, to offer sacrifices on my altar, to burn incense, and to wear an ephod in my presence. I also gave to your forefather's family all the Israelites' offerings made with fire.
Nilimchagua baba yako kati ya makabila yote ya Israeli kuwa kuhani wangu, kukwea kwenye madhabahu yangu, kufukiza uvumba na kuvaa kisibau mbele yangu. Pia niliwapa nyumba ya baba yako sadaka zote zilizotolewa kwa moto na Waisraeli.
29 So why have you treated with contempt my sacrifices and offerings that I have ordered for my place of worship? You honor your sons more than me by fattening yourselves with the best parts of all the offerings from my people Israel.
Kwa nini unadharau dhabihu zangu na sadaka zile nilizoziamuru kwa ajili ya makao yangu? Kwa nini unawaheshimu wanao kuliko mimi kwa kujinenepesha wenyewe kwa kula sehemu zilizo bora za kila sadaka zinazotolewa na watu wangu wa Israeli?’
30 Consequently, this is the declaration of the Lord: I made a definite promise that your family and your father's family would always serve me as priests. But now the Lord declares: Not anymore! Instead I will honor those who honor me, but those who despise me I will treat with contempt.
“Kwa hiyo, Bwana, Mungu wa Israeli asema: ‘Niliahidi kuwa nyumba yako na nyumba ya baba yako wangehudumu mbele zangu milele.’ Lakini sasa Bwana anasema: ‘Jambo hili na liwe mbali nami! Wale wanaoniheshimu nitawaheshimu, wale wanaonidharau mimi watadharauliwa.
31 The time is coming when I will bring your family and your father's family to an end. No one will live to an old age.
Wakati unakuja nitakapozipunguza nguvu zenu na nguvu ya nyumba ya baba yenu, ili pasiwepo mtu katika mbari yenu atakayeishi kuuona uzee
32 You will see tragedy in the place of worship. While Israel will prosper, no one in your family will ever again reach old age.
nanyi mtaona huzuni katika makao yangu. Ingawa Israeli watafanyiwa mema, katika mbari yenu kamwe hapatakuwepo mtu atakayeishi hadi kuwa mzee.
33 Anyone of your family not cut off from serving at my altar will make your eyes weep and cause you grief. All your descendants will die when full of life.
Kila mmoja wenu ambaye sitamkatilia mbali kutoka madhabahuni pangu atabakizwa tu kupofusha macho yenu kwa machozi na kuihuzunisha mioyo yenu, nao wazao wenu wote watakufa watakapokuwa wamefikia umri wa kustawi.
34 Here is a sign for you that this will happen regarding your two sons Hophni and Phinehas: both will die on the same day.
“‘Kile kitakachotokea kwa wanao wawili, Hofni na Finehasi, kitakuwa ishara kwako. Wote wawili watakufa katika siku moja.
35 I will choose for myself a trustworthy priest who will do what I really want, what I have in mind. I will make sure he and his descendants are trustworthy and they will always serve my anointed one.
Mimi mwenyewe nitajiinulia kuhani mwaminifu, ambaye atafanya sawasawa na kile kilichoko moyoni mwangu na akilini mwangu. Nitaifanya nyumba yake kuwa imara, naye atahudumu mbele ya mpakwa mafuta wangu daima.
36 Every one of your descendants who is left will come and bow down to him, asking for money and food, saying, ‘Please give me work as a priest so that I can have food to eat.’”
Kisha kila mmoja aliyeachwa katika mbari yenu atakuja na kusujudu mbele yake kwa ajili ya kipande cha fedha na ganda la mkate akisema, “Niteue katika baadhi ya ofisi ya ukuhani ili niweze kupata chakula.”’”

< 1 Samuel 2 >