< 2 Thessalonians 1 >

1 Paul, Silvanus and Timothy, to the congregation of the Thessalonians in God our Father and Sovereign Jesus Christ:
Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo.
2 Grace and peace to you from God our Father and Sovereign Jesus Christ.
Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
3 We are obligated to always give thanks to God about you, brothers, and properly so, because your faith is really growing, and the love of each and every one of you towards each other keeps increasing;
Ndugu, tunapaswa kushukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana.
4 so that we ourselves boast about you among God's congregations, referring to your steadfastness and faith in the midst of all your persecutions, and the tribulations that you are enduring
Ndio maana sisi tunajivunia ninyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
5 —the above is evidence that God's judgment is right, to the end that you be considered worthy of the Kingdom of God, on behalf of which you are actually suffering;
Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake ninyi mtastahili Utawala wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
6 since to God it is right to pay back affliction to those who are afflicting you
Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,
7 and rest (along with us) to you who are being afflicted, at the revelation of the Lord Jesus from heaven with His powerful angels in blazing fire,
na kuwapeni nafuu ninyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake na wakuu
8 inflicting vengeance on those who do not know God and on those who do not obey the Gospel of our Lord Jesus Christ,
na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
9 who will pay a penalty: everlasting ruin, away from the face of the Lord and from the glory of His might, (aiōnios g166)
Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu, (aiōnios g166)
10 whenever He comes to be glorified by His saints, yes to be marveled at by all who have believed (because our testimony to you was believed); in that Day.
wakati atakapokuja Siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
11 To this end we also pray always for you, that our God may count you worthy of the calling and fulfill with power every desire of usefulness and work of faith,
Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezeshe muyastahili maisha aliyowaitia myaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
12 so that the name of our Lord Jesus Christ may be glorified in you, and you in Him, according to the grace of our God and Lord, Jesus Christ.
Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.

< 2 Thessalonians 1 >