< Job 3 >

1 After this Job opened his mouth, and cursed his day,
Baada ya jambo hili, Ayubu akafumbua kinywa chake na kuilaani siku ya kuzaliwa kwake.
2 saying,
Kisha akasema:
3 Let the day perish in which I was born, and that night in which they said, Behold a boy!
“Siku ya kuzaliwa kwangu na ipotelee mbali, nao usiku ule iliposemekana, ‘Mtoto wa kiume amezaliwa!’
4 Let that night be darkness, and let not the Lord regard it from above, neither let light come upon it.
Siku ile na iwe giza; Mungu juu na asiiangalie; nayo nuru isiiangazie.
5 But let darkness and the shadow of death seize it; let blackness come upon it;
Giza na kivuli kikuu kiikalie tena; wingu na likae juu yake; weusi na uifunike nuru yake.
6 let that day and night be cursed, let darkness carry them away; let it not come into the days of the year, neither let it be numbered with the days of the months.
Usiku ule na ushikwe na giza kuu; usihesabiwe katika siku za mwaka, wala usihesabiwe katika siku za mwezi wowote.
7 But let that night be pain, and let not mirth come upon it, nor joy.
Usiku ule na uwe tasa; sauti ya furaha na isisikike ndani yake.
8 But let him that curses that day curse it, [even] he that is ready to attack the great whale.
Wale wazilaanio siku wailaani hiyo siku, wale walio tayari kumwamsha Lewiathani.
9 Let the stars of that night be darkened; let it remain [dark], and not come into light; and let it not see the morning star arise:
Nyota zake za alfajiri na ziwe giza; nao ungojee mwanga bila mafanikio, wala usiuone mwonzi wa kwanza wa mapambazuko,
10 because it shut not up the gates of my mother's womb, for [so] it would have removed sorrow from my eyes.
kwa sababu huo usiku haukunifungia mlango wa tumbo la mama yangu, ili kuyaficha macho yangu kutokana na taabu.
11 For why died I not in the belly? and [why] did I not come forth from the womb and die immediately?
“Kwa nini sikuangamia wakati wa kuzaliwa? Kwa nini sikufa nilipokuwa ninatoka tumboni?
12 and why did the knees support me? and why did I suck the breasts?
Kwa nini pakawa na magoti ya kunipokea na matiti ili nipate kunyonyeshwa?
13 Now I should have lain down and been quiet, I should have slept and been at rest,
Kwa maana sasa ningekuwa nimepumzika kwa amani. Ningekuwa nimelala na kupumzika
14 with kings [and] councillors of the earth, who gloried in [their] swords;
pamoja na wafalme na washauri wa dunia, waliojijengea mahali ambapo sasa ni magofu,
15 or with rulers, whose gold was abundant, who filled their houses with silver:
pamoja na watawala waliokuwa na dhahabu, waliozijaza nyumba zao kwa fedha.
16 or [I should have been] as an untimely birth proceeding from his mother's womb, or as infants who never saw light.
Au kwa nini sikufichwa ardhini kama mtoto aliyezaliwa mfu, kama mtoto mchanga ambaye kamwe hakuuona mwanga?
17 There the ungodly have burnt out the fury of rage; there the wearied in body rest.
Huko waovu huacha kusumbua na huko waliochoka hupumzika.
18 And the men of old time have together ceased to hear the exactor's voice.
Wafungwa nao hufurahia utulivu wao, hawasikii tena sauti ya kukemea ya kiongozi wa watumwa.
19 The small and great are there, and the servant that feared his lord.
Wadogo na wakubwa wamo humo, na mtumwa ameachiwa huru kutoka kwa bwana wake.
20 For why is light given to those who are in bitterness, and life to those souls which are in griefs?
“Mbona nuru inawaangazia wale walio taabuni, na hao wenye uchungu kupewa uhai,
21 who desire death, and obtain it not, digging [for it] as [for] treasures;
wale wanaotamani kifo ambacho hakiji, wale watafutao kufa zaidi ya kutafuta hazina iliyofichwa,
22 and would be very joyful if they should gain it?
ambao hujawa na furaha, na hushangilia wafikapo kaburini?
23 Death [is] rest to [such] a man, for God has hedged him in.
Kwa nini uhai hupewa mtu ambaye njia yake imefichika, ambaye Mungu amemzungushia boma?
24 For my groaning comes before my food, and I weep being beset with terror.
Kwa maana kulia kwangu kwa uchungu kwanijia badala ya chakula; kusononeka kwangu kunamwagika kama maji.
25 For the terror of which I meditated has come upon me, and that which I had feared has befallen me.
Lile nililokuwa naliogopa limenijia; lile nililokuwa ninalihofia limenipata.
26 I was not at peace, nor quiet, nor had I rest; yet wrath came upon me.
Sina amani, wala utulivu; sina pumziko, bali taabu tu.”

< Job 3 >