< Osee 4 >

1 Hear the word of the Lord, ye children of Israel: for the Lord [has] a controversy with the inhabitants of the land, because there is no truth, nor mercy, nor knowledge of God in the land.
Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli, kwa sababu Bwana analo shtaka dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi: “Hakuna uaminifu, hakuna upendo, hakuna kumjua Mungu katika nchi.
2 Cursing, and lying, and murder, and theft, and adultery abound in the land, and they mingle blood with blood.
Kuna kulaani tu, uongo na uuaji, wizi na uzinzi, bila kuwa na mipaka, nao umwagaji damu mmoja baada ya mwingine.
3 Therefore shall the land mourn, and shall be diminished with all that dwell in it, with the wild beasts of the field, and the reptiles of the earth, and with the birds of the sky, and the fish of the sea shall fail:
Kwa sababu hii nchi huomboleza, wote waishio ndani mwake wanadhoofika, wanyama wa kondeni, ndege wa angani na samaki wa baharini wanakufa.
4 that neither any one may plead, nor any one reprove [another]; but my people are as a priest spoken against.
“Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka, mtu yeyote na asimlaumu mwenzake, kwa maana watu wako ni kama wale waletao mashtaka dhidi ya kuhani.
5 Therefore they shall fall by day, and the prophet with thee shall fall: I have compared thy mother unto night.
Unajikwaa usiku na mchana, nao manabii hujikwaa pamoja nawe. Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:
6 My people are like as if they had no knowledge: because thou hast rejected knowledge, I will also reject thee, that thou shalt not minister as priest to me: and [as] thou has forgotten the law of thy God, I also will forget thy children.
watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa, “Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa, mimi nami nitakukataa wewe usiwe kuhani kwangu mimi; kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako mimi nami sitawajali watoto wako.
7 According to their multitude, so they sinned against me: I will turn their glory into shame.
Kadiri makuhani walivyoongezeka, ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu, walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.
8 They will devour the sins of my people, and will set their hearts on their iniquities.
Hujilisha dhambi za watu wangu na kupendezwa na uovu wao.
9 And the priest shall be as the people: and I will avenge on them their ways, and I will recompense to them their counsels.
Hata itakuwa: Kama walivyo watu, ndivyo walivyo makuhani. Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao na kuwalipa kwa matendo yao.
10 And they shall eat, and shall not be satisfied: they have gone a-whoring, and shall by no means prosper: because they have left off to take heed to the Lord.
“Watakula lakini hawatashiba; watajiingiza katika ukahaba lakini hawataongezeka, kwa sababu wamemwacha Bwana na kujiingiza wenyewe
11 The heart of my people has gladly engaged in fornication and wine and strong drink.
katika ukahaba, divai ya zamani na divai mpya, ambavyo huondoa ufahamu
12 They asked counsel by [means of] signs, and they reported answer to them by their staves: they have gone astray in a spirit of whoredom, and gone grievously a-whoring from their God.
wa watu wangu. Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti nao hujibiwa na fimbo ya mti. Roho ya ukahaba imewapotosha, hawana uaminifu kwa Mungu wao.
13 They have sacrificed on the tops of the mountains, and on the hills they have sacrificed under the oak and poplar, and under the shady tree, because the shade was good: therefore your daughters shall go a-whoring, and your daughters-in-law shall commit adultery.
Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima, chini ya mialoni, milibua na miela, ambako kuna vivuli vizuri. Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba na wake za wana wenu uzinzi.
14 And I will not visit upon your daughters when they shall commit fornication, nor your daughters-in-law when they shall commit adultery: for they themselves mingled themselves with harlots, and sacrificed with polluted ones, and the people that understood not entangled itself with a harlot.
“Sitawaadhibu binti zenu wakati wanapogeukia ukahaba, wala wake za wana wenu wanapofanya uzinzi, kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya na kutambikia pamoja na makahaba wa mahali pa kuabudia miungu: watu wasiokuwa na ufahamu wataangamia!
15 But thou, O Israel, be not ignorant, and go ye not, [men of] Juda, to Galgala; and go not up to the house of On, and swear not by the living Lord.
“Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli, Yuda naye asije akawa na hatia. “Usiende Gilgali, usipande kwenda Beth-Aveni Wala usiape, ‘Hakika kama Bwana aishivyo!’
16 For Israel was maddened like a mad heifer: now the Lord will feed them as a lamb in a wide place.
Waisraeli ni wakaidi, kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi. Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga kama wana-kondoo katika shamba la majani?
17 Ephraim, joined with idols, has laid stumbling-blocks in his own way.
Efraimu amejiunga na sanamu, ondokana naye!
18 He has chosen the Chananites: they have grievously gone a-whoring: they have loved dishonour through her insolence.
Hata wakati wamemaliza vileo vyao wanaendelea na ukahaba wao, watawala wao hupenda sana njia za aibu.
19 Thou art a blast of wind in her wings, and they shall be ashamed because of their altars.
Kisulisuli kitawafagilia mbali na dhabihu zao zitawaletea aibu.

< Osee 4 >