< Acts 4 >

1 And while they were talking to the people, the priests and the captain of the Temple and the Sadducees came up to them,
Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakizungumza na watu, makuhani na mlinzi wa hekalu na masadukayo waliwaendea.
2 Being greatly troubled because they were teaching the people and preaching Jesus as an example of the coming back from the dead.
Walikuwa wameudhika sana kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
3 And they took them and put them in prison till the morning, for it was now evening.
Waliwakamata na kuwaweka gerezani hadi asubuhi iliyofuata, kwani tayari ilikuwa jioni.
4 But a number of those who gave hearing to the word had faith; and they were now about five thousand.
Lakini watu wengi waliokuwa wamesikia ujumbe waliamini; na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini walikadiliwa kuwa elfu tano.
5 And on the day after, the rulers and those in authority and the scribes came together in Jerusalem;
Hata ilipofika asubuhi siku iliyofuata, kwamba wakuu wao, wazee na waandishi, kwa pamoja walikusanyika Yerusalemu.
6 And Annas, the high priest, was there, and Caiaphas and John and Alexander, and all the relations of the high priest.
Anasi kuhani mkuu alikuwepo, na Kayafa, na Yohana, na Iskanda, na wote waliokuwa ni ndugu wa kuhani mkuu.
7 Then sending for Peter and John, they said, By what power and in whose name have you done this?
Walipokuwa wamewaweka Petro na Yohana katikati yao, waliwauliza, “Kwa uwezo gani, au kwa jina gani mmefanya hili?”
8 Then Peter, being full of the Holy Spirit, said to them, O you rulers of the people and men of authority,
Kisha, Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akawaambia, “Ninyi wakuu wa watu, na wazee,
9 If we are questioned today about a good work done to a man who was ill, as to how he has been made well,
kama sisi siku ya leo tunahojiwa kuhusu tendo jema lililofanywa kwa mtu huyu mgonjwa - kwa namna gani mtu huyu alifanywa mzima?
10 Take note, all of you, and all the people of Israel, that in the name of Jesus Christ of Nazareth, whom you put to death on the cross, whom God gave back from the dead, even through him is this man now before you completely well.
Hebu lijulikane hilo kwenu na kwa watu wote katika Israel, kwamba kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye mlimsulibisha, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, ni kwa njia yake kwamba mtu huyu anasimama hapa mbele yenu akiwa mwenye afya.
11 He is the stone which you builders had no use for, but which has been made the chief stone of the building.
Yesu Kristo ni jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilidharau, lakini ambalo limefanywa kuwa jiwe kuu la pembeni.
12 And in no other is there salvation: for there is no other name under heaven, given among men, through which we may have salvation.
Hakuna wokovu katika mtu mwingine awaye yote. Kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa watu, ambalo kwa hilo tunaweza kuokolewa.”
13 Now when they saw that Peter and John were without fear, though they were men of no education or learning, they were greatly surprised; and they took note of them that they had been with Jesus.
Sasa walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na wakagundua kwamba walikuwa ni watu wakawaida wasio na elimu, walishangaa, wakafahamu kwamba Petro na Yohana wamekuwa pamoja na Yesu.
14 And, seeing that the man who had been made well was there with them, they were not able to say anything against it.
Kwa sababu walimwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuwa na kitu cha kusema dhidi ya hili.
15 But when they had given them orders to go out of the Sanhedrin, they had a discussion among themselves,
Lakini walipokuwa wamekwisha kuwaamuru mitume waondoke mbele ya mkutano wa baraza, walizungumza wao kwa wao.
16 Saying, What are we to do with these men? for certainly it is clear to all who are living in Jerusalem that a most important sign has been done by them, and it is not possible to say that it is not so.
Walisema, tutawafanyaje watu hawa? Ni kweli kwamba muujiza wa ajabu umefanyika kupitia wao unajulikana na kila mmoja anayeishi Yerusalemu; hatuwezi kulikataa hilo.
17 But so that it may not go farther among the people, let us put them in fear of punishment if they say anything in future in this name.
Lakini, ili kwamba jambo hili lisienee miongoni mwa watu, hebu tuwaonye wasinene tena kwa mtu yeyote kwa jina hili.
18 And they sent for them, and gave them orders not to make statements or give teaching in the name of Jesus.
Waliwaita Petro na Yohana ndani na kuwaamuru kamwe wasinene wala kufundisha kwa jina la Yesu.
19 But Peter and John in answer said to them, It is for you to say if it is right in the eyes of God to give attention to you more than to God:
Lakini Petro na Yohana walijibu na kuwaambia, “Kama ni sahihi machoni pa Mungu kuwatii ninyi kuliko Mungu, hukumuni wenyewe.
20 For it is not possible for us to keep from saying what we have seen and have knowledge of.
Maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.”
21 And when they had said more sharp words to them, they let them go, not seeing what punishment they might give them, because of the people; for all men were giving praise to God for what had taken place.
Baada ya kuwaonya sana Petro na Yohana, waliwaacha waende. Hawakuweza kupata sababu yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetendeka.
22 For the man on whom this act of power was done was more than forty years old.
Mtu aliyekuwa amepokea muujiza wa uponyaji alipata kuwa na umri zaidi ya miaka arobaini.
23 And when they had been made free, they came back to their friends, and gave an account of all the things which the chief priests and the authorities had said to them.
Baada ya kuwaacha huru, Petro na Yohana walikuja kwa watu wao na kuwataarifu yote ambayo makuhani wakuu na wazee walikuwa wamewaambia.
24 And hearing it, they all, with one mind, made prayer to God and said, O Lord, maker of heaven and earth and the sea and all things in them:
Walipoyasikia, walipaza sauti zao kwa pamoja kwa Mungu na kusema, “Bwana, wewe uliyeumba mbingu na dunia na bahari na kila kitu ndani yake,
25 Who has said, by the Holy Spirit, through the mouth of our father David your servant, Why are the nations so violently moved, and why are the thoughts of the people so foolish?
wewe ambaye, kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema, “Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?
26 The kings of the earth were lifted up, the rulers came together, against the Lord, and against his Christ:
Wafalme wa dunia wamejipanga pamoja, na watawala wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya masihi wake.”
27 For, truly, in this town, against your holy servant, Jesus, who was marked out by you as Christ, Herod, and Pontius Pilate, with the Gentiles and the people of Israel, came together,
Ni hakika, wote Herode na Pontio Pilato, pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika kwa pamoja katika mji huu dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimpaka mafuta.
28 To do that which had been fixed before by your hand and your purpose.
Walikusanyika kwa pamoja kufanya yote ambayo mkono wako na mapenzi yako yaliyaamuru tangu awali kabla hayajatokea.
29 And now, Lord, take note of their cruel words, and give your servants power to be preachers of your word without fear,
Sasa, Bwana, yaangalie matisho yao, na ukawajaalie watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri wote. Ili
30 While your hand is stretched out to do works of mercy; so that signs and wonders may be done through the name of your holy servant Jesus.
kwamba unaponyosha mkono wako kuponya, ishara na maajabu viweze kutokea kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”
31 And when their prayer was ended, the place where they were was violently moved, and they all became full of the Holy Spirit, preaching the word of God without fear.
Walipomaliza kuomba, eneo ambalo walikusanyika kwa pamoja likatikiswa, na wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, na walinena neno la Mungu kwa ujasili.
32 And all those who were of the faith were one in heart and soul: and not one of them said that any of the things which he had was his property only; but they had all things in common.
Idadi kubwa ya wale walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja: na hakuna hata mmoja wao aliyesema kwamba chochote alichomiliki kilikuwa cha kwake mwenyewe; badala yake walikuwa na vitu vyote shirika.
33 And with great power the Apostles gave witness of the coming back of the Lord Jesus from the dead; and grace was on them all.
Kwa nguvu kubwa mitume walikuwa wakiutangaza ushuhuda wao kuhusu ufufuo wa Bwana Yesu, na neema kubwa ilikuwa juu yao wote.
34 And no one among them was in need; for everyone who had land or houses, exchanging them for money, took the price of them,
Hapakuwa na mtu yeyote miongoni mwao aliyepungukiwa na mahitaji, kwa sababu watu wote waliokuwa na hati za viwanja au nyumba, waliviuza na kuleta pesa ya vitu waliyokuwa wameuza
35 And put it at the feet of the Apostles for distribution to everyone as he had need.
na kuviweka chini ya miguu ya mitume. Na mgawanyo ulifanywa kwa kila muumini, kulingana na kila mmoja alivyokuwa na hitaji.
36 And Joseph, who was given by the Apostles the name of Barnabas (the sense of which is, Son of comfort), a Levite and a man of Cyprus by birth,
Yusufu, mlawi, mtu kutoka Kipro, alipewa jina la Barnabasi na mitume (hiyo ikitafasiriwa, ni mwana wa faraja).
37 Having a field, got money for it and put the money at the feet of the Apostles.
Akiwa na shamba, aliliuza na akaleta fedha, akaziweka chini ya miguu ya mitume.

< Acts 4 >