< 1 Corinthians 8 >

1 Now about things offered to images: we all seem to ourselves to have knowledge. Knowledge gives pride, but love gives true strength.
Sasa kuhusu chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, tunajua kwamba “sisi sote tuna ujuzi.” Lakini ujuzi hujivuna, bali upendo hujenga.
2 If anyone seems to himself to have knowledge, so far he has not the right sort of knowledge about anything;
Mtu yeyote anayedhani kwamba anajua kitu, bado hajui kama impasavyo kujua.
3 But if anyone has love for God, God has knowledge of him.
Lakini mtu ampendaye Mungu, hujulikana naye Mungu.
4 So, then, as to the question of taking food offered to images, we are certain that an image is nothing in the world, and that there is no God but one.
Hivyo basi, kuhusu kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu: Tunajua kwamba “Sanamu si kitu chochote kabisa duniani,” na kwamba “Kuna Mungu mmoja tu.”
5 For though there are those who have the name of gods, in heaven or on earth, as there are a number of gods and a number of lords,
Kwa kuwa hata kama wapo hao wanaoitwa miungu, kama wakiwa mbinguni au duniani (kama ilivyo kweli wapo “miungu” wengi na “mabwana” wengi),
6 There is for us only one God, the Father, of whom are all things, and we are for him; and one Lord, Jesus Christ, through whom are all things, and we have our being through him.
kwetu sisi yuko Mungu mmoja, aliye Baba, ambaye vitu vyote vyatoka kwake na kwa ajili yake sisi twaishi; na kuna Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa yeye vitu vyote vimekuwepo na kwa yeye tunaishi.
7 Still, all men have not that knowledge: but some, being used till now to the image, are conscious that they are taking food which has been offered to the image; and because they are not strong in the faith, their minds are troubled.
Lakini si wote wanaojua jambo hili. Baadhi ya watu bado wamezoea sanamu kuwa halisi hivi kwamba wanapokula chakula kama hicho wanadhani kimetolewa sadaka kwa sanamu na kwa kuwa dhamiri zao ni dhaifu, dhamiri yao inanajisika.
8 But God's approval of us is not based on the food we take: if we do not take it we are no worse for it; and if we take it we are no better.
Lakini chakula hakituleti karibu na Mungu, wala hatupotezi chochote tusipokula, wala hatuongezi chochote kama tukila.
9 But take care that this power of yours does not give cause for trouble to the feeble.
Lakini angalieni jinsi mnavyotumia uhuru wenu usije ukawa kikwazo kwao walio dhaifu.
10 For if a man sees you, who have knowledge, taking food as a guest in the house of an image, will it not give him, if he is feeble, the idea that he may take food offered to images?
Kwa maana kama mtu yeyote mwenye dhamiri dhaifu akiwaona ninyi wenye ujuzi huu mkila katika hekalu la sanamu, je, si atatiwa moyo kula chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu?
11 And so, through your knowledge, you are the cause of destruction to your brother, for whom Christ underwent death.
Kwa njia hiyo, huyo ndugu mwenye dhamiri dhaifu, ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake, ataangamia kwa sababu ya ujuzi wenu.
12 And in this way, doing evil to the brothers, and causing trouble to those whose faith is feeble, you are sinning against Christ.
Mnapotenda dhambi dhidi ya ndugu zenu kwa njia hii na kujeruhi dhamiri zao zilizo dhaifu, mnamkosea Kristo.
13 For this reason, if food is a cause of trouble to my brother, I will give up taking meat for ever, so that I may not be a cause of trouble to my brother. (aiōn g165)
Kwa hiyo, kama kile ninachokula kitamfanya ndugu yangu aanguke katika dhambi, sitakula nyama kamwe, nisije nikamfanya ndugu yangu aanguke. (aiōn g165)

< 1 Corinthians 8 >