< Luke 4 >

1 And Jesus, full of the Holy Spirit, returned from the Jordan, and was led by the Spirit into the wilderness,
Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
2 and was there forty days, to be tempted by the devil. And he ate nothing during those days; and when they were ended, he was afterward hungry.
kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
3 And the devil said to him: If you are the Son of God, command this stone to become bread.
Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
4 And Jesus answered him, and said: It is written, Man shall not live by bread alone, but by every word of God.
Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
5 And the devil took him up into a high mountain, and showed him all the kingdoms of the world, in a moment of time.
Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
6 And the devil said to him: I will give you all the authority and glory of these, for it is delivered to me; and to whomever I will, I give it.
Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
7 If, therefore, you will bow with reverence before me, all shall be yours.
Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
8 And Jesus answered and said to him: Get behind me, Satan; it is written, You shall worship the Lord your God, and him only shall you serve.
Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
9 And he brought him to Jerusalem, and placed him on the pinnacle of the temple, and said to him: If you are the Son of God, throw yourself down from this place;
Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
10 for it is written, He will give his angels charge concerning you, to guard you carefully;
Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
11 and in their hands they shall take you up, lest you strike your foot against a stone.
na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
12 And Jesus answered and said to him: It is said, You shall not put the Lord your God to the proof.
Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
13 And when the devil had ended all the temptation, he departed from him for a time.
Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
14 And Jesus returned in the power of the Spirit into Galilee: and his fame went throughout the whole of that region.
Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
15 And he taught in their synagogues, being glorified by all.
Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
16 And he came to Nazareth, where he had been brought up; and, as his custom was, he entered the synagogue on the sabbath-day, and stood up to read.
Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
17 And the volume of Isaiah the prophet was given to him: and when he had unrolled the volume, he found the place where it was written:
Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
18 The Spirit of the Lord is upon me; because he has anointed me to preach the gospel to the poor; he has sent me to heal the brokenhearted; to proclaim liberty to the captives, and recovery of sight to the blind; to set free the oppressed;
“Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
19 to proclaim the acceptable year of the Lord.
kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
20 And he rolled up the volume, and save it back to the attendant, and sat down; and the eyes of all that were in the synagogue were earnestly fixed upon him.
Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
21 And he began to say to them: This scripture which you have heard, is this day fulfilled.
Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
22 And all extolled him; and they wondered at the words of grace which proceeded out of his mouth, and said: Is not this the son of Joseph?
Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
23 And he said to them: You will assuredly apply to me this proverb, Physician, heal yourself. Whatever things we have heard were done in Capernaum, do also here in your country.
Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
24 And he said: Verily I say to you, No prophet is accepted in his own country.
Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
25 And I tell you, in truth, there were many widows in Israel in the days of Elijah, when the heaven was shut up for three years and six months, so that a great famine was on all the land:
Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
26 and to no one of them was Elijah sent, but to Sarepta, a city of Sidon, to a woman that was a widow.
Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
27 And many lepers were in Israel, in the time of Elisha the prophet; and no one of them was cleansed but Naaman the Syrian.
Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
28 And all that were in the synagogue, when they heard these things, were filled with anger,
Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
29 and arose, and drove him out of the city, and brought him to the brow of the hill on which their city was built, that they might throw him down headlong.
Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
30 But he passed through the midst of them, and went away.
Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
31 And he went down to Capernaum, a city of Galilee. And he was teaching them on the sabbath-days.
Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
32 And they were astonished at his teaching, for his word was with authority.
Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
33 And there was in the synagogue a man who had the spirit of an unclean demon; and he cried out with a loud voice,
Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
34 saying: Let us alone; what have we to do with thee, Jesus, thou Nazarene? Hast thou come to destroy us? I know thee who thou art, the Holy One of God.
“Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
35 And Jesus rebuked him, saying: Be silent, and come out of him. And the demon threw him into the midst, and came out of him, and hurt him not.
Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
36 And amazement came upon all, and they spoke one to another, saying: What teaching is this? for with authority and power he commands the unclean spirits, and they come out.
Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
37 And his fame went abroad into every place of the country round about.
Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
38 And he arose and went out of the synagogue into the house of Simon. And Simon’s mother-in-law was confined with a violent fever: and they besought him in her behalf.
Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
39 And he stood over her, and rebuked the fever, and it left her: and she arose immediately, and ministered to them.
Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
40 And when the sun had gone down, all that had any sick with various diseases, brought them to him; and he laid his hands on every one of them, and cured them.
Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
41 Demons also came out of many, crying out and saying: Thou art the Christ, the Son of God. And he rebuked them, and did not permit them to speak, because they knew that he was the Christ.
Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
42 And when it was day, he went out and departed into a desert place; and the multitudes sought for him, and came to him and endeavored to detain him, that he should not go away from them.
Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
43 But he said to them: I must make known the good news of the kingdom of God to other cities also; for to this end I have been sent.
Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
44 And he continued to preach in the synagogues of Galilee.
Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.

< Luke 4 >