< Genesis 9 >

1 And God blessed Noah and his sons, and said unto them, Be fruitful, and multiply, and replenish the earth.
Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
2 And the fear of you and the dread of you shall be upon every beast of the earth, and upon every bird of the heavens; with all wherewith the ground teemeth, and all the fishes of the sea, into your hand are they delivered.
Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
3 Every moving thing that liveth shall be food for you; as the green herb have I given you all.
Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
4 But flesh with the life thereof, [which is] the blood thereof, shall ye not eat.
Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
5 And surely your blood, [the blood] of your lives, will I require; at the hand of every beast will I require it: and at the hand of man, even at the hand of every man’s brother, will I require the life of man.
Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
6 Whoso sheddeth man’s blood, by man shall his blood be shed: for in the image of God made he man.
Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
7 And you, be ye fruitful, and multiply; bring forth abundantly in the earth, and multiply therein.
Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
8 And God spake unto Noah, and to his sons with him, saying,
Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
9 And I, behold, I establish my covenant with you, and with your seed after you;
“Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
10 and with every living creature that is with you, the birds, the cattle, and every beast of the earth with you; of all that go out of the ark, even every beast of the earth.
na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
11 And I will establish my covenant with you; neither shall all flesh be cut off any more by the waters of the flood; neither shall there any more be a flood to destroy the earth.
Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
12 And God said, This is the token of the covenant which I make between me and you and every living creature that is with you, for perpetual generations:
Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
13 I do set my bow in the cloud, and it shall be for a token of a covenant between me and the earth.
Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
14 And it shall come to pass, when I bring a cloud over the earth, that the bow shall be seen in the cloud,
Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
15 and I will remember my covenant, which is between me and you and every living creature of all flesh; and the waters shall no more become a flood to destroy all flesh.
ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
16 And the bow shall be in the cloud; and I will look upon it, that I may remember the everlasting covenant between God and every living creature of all flesh that is upon the earth.
Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
17 And God said unto Noah, This is the token of the covenant which I have established between me and all flesh that is upon the earth.
Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
18 And the sons of Noah, that went forth from the ark, were Shem, and Ham, and Japheth: and Ham is the father of Canaan.
Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
19 These three were the sons of Noah: and of these was the whole earth overspread.
Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
20 And Noah began to be a husbandman, and planted a vineyard:
Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
21 and he drank of the wine, and was drunken; and he was uncovered within his tent.
Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
22 And Ham, the father of Canaan, saw the nakedness of his father, and told his two brethren without.
Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 And Shem and Japheth took a garment, and laid it upon both their shoulders, and went backward, and covered the nakedness of their father; and their faces were backward, and they saw not their father’s nakedness.
Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
24 And Noah awoke from his wine, and knew what his youngest son had done unto him.
Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
25 And he said, Cursed be Canaan; A servant of servants shall he be unto his brethren.
Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
26 And he said, Blessed be Jehovah, the God of Shem; And let Canaan be his servant.
Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
27 God enlarge Japheth, And let him dwell in the tents of Shem; And let Canaan be his servant.
Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
28 And Noah lived after the flood three hundred and fifty years.
Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
29 And all the days of Noah were nine hundred and fifty years: and he died.
Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.

< Genesis 9 >