< Revelation 9 >

1 The fifth angel sounded, and I saw a star from the sky which had fallen to the earth. The key to the pit of the Abyss (Abyssos g12) was given to him.
Kisha malaika wa tano alipiga tarumbeta yake. Niliona nyota kutoka mbinguni iliyokuwa imeanguka kwenye dunia. Nyota ilipewa ufunguo wa shimo linaloelekea kwenye shimo lisilo na mwisho. (Abyssos g12)
2 He opened the pit of the Abyss (Abyssos g12), and smoke went up out of the pit, like the smoke from a burning furnace. The sun and the air were darkened because of the smoke from the pit.
Alifungua shimo lisilo na kikomo, na moshi ukapanda juu kwa safu kutoka ndani ya shimo kama moshi kutoka katika tanuru kubwa. Jua na anga vilibadilika vikawa giza kwa sababu ya moshi uliotoka shimoni. (Abyssos g12)
3 Then out of the smoke came locusts on the earth, and power was given to them, as the scorpions of the earth have power.
Ndani ya moshi nzige walitoka kuja juu ya dunia, nao walipewa nguvu kama ile ya nge juu ya dunia.
4 They were told that they should not hurt the grass of the earth, neither any green thing, neither any tree, but only those people who do not have God’s seal on their foreheads.
Waliambiwa kutokudhuru majani katika nchi au mmea wowote wa kijani au mti, isipokuwa tu watu ambao hawakuwa na muhuri wa Mungu katika paji za nyuso zao.
5 They were given power, not to kill them, but to torment them for five months. Their torment was like the torment of a scorpion when it strikes a person.
Hawakupewa ruhusa ya kuwaua hao watu, bali kuwatesa tu kwa miezi mitano. Uchungu wao ulikuwa kama ule wa kuumwa na nge amwumapo mtu.
6 In those days people will seek death, and will in no way find it. They will desire to die, and death will flee from them.
Katika siku hizo watu watatafuta kifo, lakini hawatakipata. Watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.
7 The shapes of the locusts were like horses prepared for war. On their heads were something like golden crowns, and their faces were like people’s faces.
Nzige walifanana na farasi walioandaliwa kwa vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji ya dhahabu na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
8 They had hair like women’s hair, and their teeth were like those of lions.
Walikuwa na nywele kama za wanawake na meno yao yalikuwa kama ya simba.
9 They had breastplates like breastplates of iron. The sound of their wings was like the sound of many chariots and horses rushing to war.
Walikuwa na vifua kama vifua vya chuma na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari mengi ya vita na farasi wakimbiao kwenda vitani.
10 They have tails like those of scorpions, with stingers. In their tails they have power to harm men for five months.
Walikuwa na mikia inayouma kama nge; katika mikia yao walikuwa na nguvu ya kudhuru watu kwa miezi mitano.
11 They have over them as king the angel of the Abyss (Abyssos g12). His name in Hebrew is "Abaddon", and in Greek, he has the name "Apollyon".
Walikuwa naye kama mfalme juu yao malaika wa shimo lisilokuwa na mwisho. Jina lake katika Kiebrania ni Abadoni, na katika Kiyunani ana jina Apolioni. (Abyssos g12)
12 The first woe is past. Behold, there are still two woes coming after this.
Ole ya kwanza imepita. Angalia! Baada ya hili kuna maafa mawili yaja.
13 The sixth angel sounded. I heard a voice from the horns of the golden altar which is before God,
Malaika wa sita alipiga tarumbeta yake, na nikasikia sauti ikitoka katika pembe ya madhabahu ya dhahabu ambayo iko mbele za Mungu.
14 saying to the sixth angel who had the trumpet, “Free the four angels who are bound at the great river Euphrates!”
Sauti ilimwambia malaika wa sita aliyekuwa na tarumbeta, “Waachie malaika wanne ambao wamefungwa katika mto mkubwa Efrata.”
15 The four angels were freed who had been prepared for that hour and day and month and year, so that they might kill one third of mankind.
Malaika wale wanne waliokuwa wameandaliwa kwa saa hiyo maalumu, siku hiyo, mwezi huo, na mwaka huo, waliachiwa wawaue theluthi ya wanadamu.
16 The number of the armies of the horsemen was two hundred million. I heard the number of them.
Idadi ya maaskari waliokuwa juu ya farasi ilikuwa 200, 000, 000. Nilisikia idadi yao.
17 Thus I saw the horses in the vision and those who sat on them, having breastplates of fiery red, hyacinth blue, and sulfur yellow; and the horses’ heads resembled lions’ heads. Out of their mouths proceed fire, smoke, and sulfur.
Hivi ndivyo nilivyoona farasi katika maono yangu na wale waliopanda juu yao: Vifua vyao vilikuwa vyekundu kama moto, bluu iliyoiva na njano isiyoiva. Vichwa vya farasi vilifanana na vichwa vya simba, na midomoni mwao ulitoka moto, moshi na salfa.
18 By these three plagues, one third of mankind was killed: by the fire, the smoke, and the sulfur, which proceeded out of their mouths.
Theluthi ya wanadamu waliuawa na haya mapigo matatu: moto, moshi, na salfa iliyotoka katika midomo yao.
19 For the power of the horses is in their mouths and in their tails. For their tails are like serpents, and have heads; and with them they harm.
Kwa kuwa nguvu ya farasi ilikuwa katika midomo yao na katika mikia yao—kwa kuwa mikia yao ilikuwa kama nyoka, na walikuwa na vichwa ambavyo walitumia kuwatia majeraha wanadamu.
20 The rest of mankind, who were not killed with these plagues, did not repent of the works of their hands, that they would not worship demons, and the idols of gold, and of silver, and of brass, and of stone, and of wood, which cannot see, hear, or walk.
Watu waliobaki, wale ambao walikuwa hawajauawa na mapigo haya, hawakutubia matendo yao waliyokuwa wamefanya, wala hawakuacha kuabudu mapepo na miungu ya dhahabu, fedha, shaba, mawe na miti—vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia au kutembea.
21 They did not repent of their murders, their sorceries, their sexual immorality, or their thefts.
Wala hawakutubia uuaji wao, uchawi wao, uasherati wao au njia zao za wizi.

< Revelation 9 >