< Matthew 28 >

1 Now after the Sabbath, as it began to dawn on the first day of the week, Mary Magdalene and the other Mary came to see the tomb.
Baada ya Sabato, karibu na mapambazuko ya siku ile ya Jumapili, Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikwenda kutazama lile kaburi.
2 Behold, there was a great earthquake, for an angel of the Lord descended from the sky and came and rolled away the stone from the door and sat on it.
Ghafla kutatokea tetemeko kubwa la nchi; malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akalivingirisha lile jiwe, akalikalia.
3 His appearance was like lightning, and his clothing white as snow.
Alionekana kama umeme na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.
4 For fear of him, the guards shook, and became like dead men.
Walinzi wa lile kaburi wakatetemeka kwa hofu kubwa, hata wakawa kama wamekufa.
5 The angel answered the women, “Do not be afraid, for I know that you seek Jesus, who has been crucified.
Lakini yule malaika akawaambia wale wanawake, “Ninyi msiogope! Najua kwamba mnamtafuta Yesu aliyesulubiwa.
6 He is not here, for he has risen, just like he said. Come, see the place where the Lord was lying.
Hayupo hapa maana amefufuka kama alivyosema. Njoni mkaone mahali alipokuwa amelala.
7 Go quickly and tell his disciples, ‘He has risen from the dead, and behold, he goes before you into Galilee; there you will see him.’ Behold, I have told you.”
Basi, nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba amefufuka kutoka wafu, na sasa anawatangulieni kule Galilaya; huko mtamwona. Haya, mimi nimekwisha waambieni.”
8 They departed quickly from the tomb with fear and great joy, and ran to bring his disciples word.
Wakiwa wenye hofu na furaha kubwa, hao wanawake walitoka upesi kaburini, wakakimbia kwenda kuwaambia wanafunzi wake.
9 As they went to tell his disciples, behold, Jesus met them, saying, “Rejoice!” They came and took hold of his feet, and worshiped him.
Mara, Yesu akakutana nao, akawasalimu: “Salamu.” Hao wanawake wakamwendea, wakapiga magoti mbele yake, wakashika miguu yake.
10 Then Jesus said to them, “Do not be afraid. Go tell my brothers that they should go into Galilee, and there they will see me.”
Kisha Yesu akawaambia, “Msiogope! Nendeni mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya, na huko wataniona.”
11 Now while they were going, behold, some of the guards came into the city and told the chief priests all the things that had happened.
Wale wanawake walipokuwa wanakwenda zao, baadhi ya walinzi wa lile kaburi walikwenda mjini kutoa taarifa kwa makuhani wakuu juu ya mambo yote yaliyotukia.
12 When they were assembled with the elders and had taken counsel, they gave a large amount of silver to the soldiers,
Basi, wakakutana pamoja na wazee, na baada ya kushauriana, wakawapa wale askari kiasi kikubwa cha fedha
13 saying, “Say that his disciples came by night and stole him away while we slept.
wakisema, “Ninyi mtasema hivi: Wanafunzi wake walikuja usiku, wakamwiba sisi tukiwa tumelala.
14 If this comes to the governor’s ears, we will persuade him and make you free of worry.”
Na kama mkuu wa mkoa akijua jambo hili, sisi tutasema naye na kuhakikisha kuwa ninyi hamtapata matatizo.”
15 So they took the money and did as they were told. This saying was spread abroad among the Jews, and continues until today.
Wale walinzi wakazichukua zile fedha, wakafanya kama walivyofundishwa. Habari hiyo imeenea kati ya Wayahudi mpaka leo.
16 But the eleven disciples went into Galilee, to the mountain where Jesus had sent them.
Wale wanafunzi kumi na mmoja walikwenda Galilaya kwenye ule mlima aliowaagiza Yesu.
17 When they saw him, they bowed down to him; but some doubted.
Walipomwona, wakamwabudu, ingawa wengine walikuwa na mashaka.
18 Jesus came to them and spoke to them, saying, “All authority has been given to me in heaven and on earth.
Yesu akaja karibu, akawaambia, “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.
19 Go and make disciples of all nations, baptizing them in the name of the Father and of the Son and of the Holy Spirit,
Nendeni basi, mkawafanye watu wa mataifa yote wawe wanafunzi wangu; mkiwabatiza kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu.
20 teaching them to observe all things that I commanded you. Behold, I am with you always, even to the consummation of the age (aiōn g165)." Amen.
Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni. Nami nipo pamoja nanyi siku zote; naam, mpaka mwisho wa nyakati.” (aiōn g165)

< Matthew 28 >