< Matthew 13 >

1 On that day Jesus went out of the house and sat by the seaside.
Katika siku hiyo Yesu aliondoka nyumbani na kukaa kando ya bahari.
2 Great multitudes gathered to him, so that he entered into a boat and sat; and all the multitude stood on the beach.
Umati mkubwa ulikusanyika kwa kumzunguka, aliingia ndani ya mtumbwi na kukaa ndani yake. Umati wote walisimama kando ya bahari.
3 He spoke to them many things in parables, saying, “Behold, a farmer went out to sow.
Kisha Yesu alisema maneno mengi kwa mifano, Alisema, “Tazama, mpanzi alienda kupanda.
4 As he sowed, some seeds fell by the roadside, and the birds came and devoured them.
Alipokuwa akipanda baadhi ya mbegu zilianguka kando ya njia na ndege walikuja wakazidonoa.
5 Others fell on rocky ground, where they did not have much soil, and immediately they sprang up, because they had no depth of earth.
Mbegu zingine zilianguka juu ya mwamba, ambapo hazikupata udongo wa kutosha. Ghafla zilichipuka kwa sababu udongo haukuwa na kina.
6 When the sun had risen, they were scorched. Because they had no root, they withered away.
Lakini jua lilipo chomoza zilichomwa kwa sababu hazikuwa na mizizi, na zilikauka.
7 Others fell among thorns. The thorns grew up and choked them.
Mbengu zingine zilianguka kati ya miti yenye miiba. Miti yenye miiba ilirefuka juu ikaisonga.
8 Others fell on good soil and yielded fruit: some one hundred times as much, some sixty, and some thirty.
Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri na kuzaa mbegu, zingine mara mia moja zaidi, zingine sitini na zingine thelathini
9 He who has ears to hear, let him hear.”
Aliye na masikio na asikie.
10 The disciples came, and said to him, “Why do you speak to them in parables?”
Wanafunzi walikuja na kumwambia Yesu, “Kwa nini unazungumza na makutano kwa mifano?”
11 He answered them, “To you it is given to know the mysteries of the Kingdom of Heaven, but it is not given to them.
Yesu alijibu kuwaambia, “Mmepewa upendeleo wa kufahamu siri za ufalme wa mbinguni, bali kwao hawajapewa.
12 For whoever has, to him will be given, and he will have abundance; but whoever does not have, from him will be taken away even that which he has.
Lakini yeyote aliyenacho, kwake yeye ataongezewa zaidi, na atapata faida kubwa. Ilasiye nacho hata kile alichonacho atanyang'anywa.
13 Therefore I speak to them in parables, because seeing they do not see, and hearing, they do not hear, neither do they understand.
Hivyo naongea nao kwa mifano kwa sababu ingawa wanaona, wasione kweli. Na ingawa wanasikia wasisikie wala kufahamu.
14 In them the prophecy of Isaiah is fulfilled, which says, ‘By hearing you will hear, and will in no way understand; Seeing you will see, and will in no way perceive;
Unabii wa Isaya umetimia kwao, ule usemao, “Msikiapo msikie, lakini kwa namna yoyote hamtaelewa; wakati mwonapo muweze kuona, lakini kwa namna yeyote ile msijue.
15 for this people’s heart has grown callous, their ears are dull of hearing, and they have closed their eyes; or else perhaps they might perceive with their eyes, hear with their ears, understand with their heart, and would turn again, and I would heal them.’
Na mioyo ya watu hawa imekuwa giza, ni vigumu kusikia, na wamefumba macho yao, ili wasiweze kuona kwa macho yao, au kusikia kwa masikio yao, au kufahamu kwa mioyo yao, hivyo wangenigeukia tena, na ningewaponya.'
16 “But blessed are your eyes, for they see; and your ears, for they hear.
Bali macho yenu yamebarikiwa, kwa kuwa yanaona, na masikio yenu kwa kuwa yanasikia.
17 For most certainly I tell you that many prophets and righteous men desired to see the things which you see, and did not see them; and to hear the things which you hear, and did not hear them.
Hakika nawaambia manabii wengi na watu wenye haki walikuwa na hamu ya kuyaona mambo yale myaonayo, na hawakuweza kuyaona. Walitamani kusikia mambo yale mnayosikia, hawakuyasikia.
18 “Hear, then, the parable of the farmer.
. Sasa sikilizeni mfano wa mpanzi.
19 When anyone hears the word of the Kingdom and does not understand it, the evil one comes and snatches away that which has been sown in his heart. This is what was sown by the roadside.
Wakati yeyote asikiapo neno la ufalme na asilifahamu, ndipo mwovu huja na kukinyakua kilichokwisha kupandwa ndani ya moyo wake. Hii ni mbegu ile iliyopandwa kando ya njia.
20 What was sown on the rocky places, this is he who hears the word and immediately with joy receives it;
Yeye aliyepandwa katika miamba ni yule asikiaye neno na kulipokea haraka kwa furaha.
21 yet he has no root in himself, but endures for a while. When oppression or persecution arises because of the word, immediately he stumbles.
Bado hana mizizi ndani yake, ila huvumilia kwa kitambo kifupi. Wakati matatizo au mateso yanapotokea kwa sababu ya neno hujikwaa ghafla.
22 What was sown among the thorns, this is he who hears the word, but the cares of this age (aiōn g165) and the deceitfulness of riches choke the word, and he becomes unfruitful.
Aliyepandwa kati ya miti ya miiba, huyu ni yule alisikiaye neno lakini masumbuko ya ulimwengu na udaganyifu wa utajiri hulisonga lile neno lisije likazaa matunda. (aiōn g165)
23 What was sown on the good ground, this is he who hears the word and understands it, who most certainly bears fruit and produces, some one hundred times as much, some sixty, and some thirty.”
Aliyepandwa kwenye udongo mzuri, huyu ni yule asikiaye neno na kulifahamu. Huyu ni yule azaaye matunda na kuendelea kuzaa moja zaidi ya mara mia, nyingine sitini, nyingine thelathini.''
24 He set another parable before them, saying, “The Kingdom of Heaven is like a man who sowed good seed in his field,
Yesu aliwapa mfano mwingine. Akisema, “Ufalme wa mbinguni unafananishwa na mtu aliye panda mbengu nzuri katika shamba lake
25 but while people slept, his enemy came and sowed darnel weeds also among the wheat, and went away.
Lakini watu waliposinzia, adui wake akaja pia akapanda magugu katikati ya ngano kisha akaenda zake.
26 But when the blade sprang up and produced grain, then the darnel weeds appeared also.
Baadaye ngano ilipoota na kutoa mazao yake, ndipo magugu yalitokea pia.
27 The servants of the householder came and said to him, ‘Sir, did not you sow good seed in your field? Where did these darnel weeds come from?’
Na watumishi wa mwenye shamba walikuja wakamwambia, 'Bwana, hukupanda mbengu nzuri katika shamba lako? Imekuwaje sasa lina magugu?
28 “He said to them, ‘An enemy has done this.’ “The servants asked him, ‘Do you want us to go and gather them up?’
Akawaambia, Adui ametenda hili.' Watumishi walimwambia, “Kwa hiyo unataka twende tukayang'oe?”
29 “But he said, ‘No, lest perhaps while you gather up the darnel weeds, you root up the wheat with them.
Mwenye shamba akisema, 'Hapana, wakati mnayang'oa magugu mtang'oa pamoja na ngano.
30 Let both grow together until the harvest, and in the harvest time I will tell the reapers, “First, gather up the darnel weeds, and bind them in bundles to burn them; but gather the wheat into my barn.”’”
Yaacheni yakue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati wa mavuno nitasema kwa wavunaji, 'Kwanza yang'oeri magugu na yafungeni matita matita na kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika ghala langu.''''
31 He set another parable before them, saying, “The Kingdom of Heaven is like a grain of mustard seed which a man took, and sowed in his field,
Kisha Yesu aliwatolea mfano mwingine. Akasema, “Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake.
32 which indeed is smaller than all seeds. But when it is grown, it is greater than the herbs and becomes a tree, so that the birds of the air come and lodge in its branches.”
Mbegu hii kwa hakika ni ndogo kuliko mbegu zingine zote. Lakini imeapo huwa kubwa kuliko mimea yote ya bustani, huwa mti, kiasi kwamba ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake.”
33 He spoke another parable to them. “The Kingdom of Heaven is like yeast which a woman took and hid in three measures of meal, until it was all leavened.”
Akawaambia mfano mwingine tena.”Ufalme wa mbinguni ni kama chachu ile iliyo twaliwa na mwanamke na kuichanganya kwa vipimo vitatu kwa unga mpaka viumuke.
34 Jesus spoke all these things in parables to the multitudes; and without a parable, he did not speak to them,
Hayo yote Yesu aliyasema kwenye umati kwa mifano. Na pasipo mifano hakusema chochote kwao.
35 that it might be fulfilled which was spoken through the prophet, saying, “I will open my mouth in parables; I will utter things hidden from the foundation of the world.”
Hii ilikuwa kwamba kile kilichokwisha semwa kupitia kwa nabii kiweze kutimia, pale aliposema, “Nitafumbua kinywa changu katika mifano. Nitasema mambo yale yaliyokuwa yamefichwa tangu misingi ya ulimwengu”.
36 Then Jesus sent the multitudes away, and went into the house. His disciples came to him, saying, “Explain to us the parable of the darnel weeds of the field.”
Kisha Yesu aliwaacha makutano na kwenda nyumbani. Wanafunzi wake walimwendea na kusema, “Tufafanulie mfano wa magugu ya shambani.''
37 He answered them, “He who sows the good seed is the Son of Man,
Yesu alijibu na kusema, “Apandae mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
38 the field is the world, the good seeds are the children of the Kingdom, and the darnel weeds are the children of the evil one.
Shamba ni ulimwengu; na mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu, na adui aliye zipanda ni ibilisi.
39 The enemy who sowed them is the devil. The harvest is the consummation of the age (aiōn g165), and the reapers are angels.
Na mavuno ni mwisho wa ulimwengu, na wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
40 As therefore the darnel weeds are gathered up and burned with fire; so will it be at the consummation of this age (aiōn g165).
Kama vile magugu yanavyo kusanywa na kuchomwa moto, hivyo ndivyo itakavyo kuwa mwisho wa ulimwengu. (aiōn g165)
41 The Son of Man will send out his angels, and they will gather out of his Kingdom all things that cause stumbling and those who do iniquity,
Mwana wa Adamu atatuma malaika wake, na kukusanya kutoka katika ufalme wake mambo yote yaliyosababisha dhambi na wale watendao maasi.
42 and will cast them into the furnace of fire. There will be weeping and gnashing of teeth.
Watawatupa wote katika tanuru la moto, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
43 Then the righteous will shine like the sun in the Kingdom of their Father. He who has ears to hear, let him hear.
Ndipo watu wenye haki watakapong'aa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio na sikie.
44 “Again, the Kingdom of Heaven is like treasure hidden in the field, which a man found and hid. In his joy, he goes and sells all that he has and buys that field.
Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa shambani. Mtu akaiona na kuificha. Katika furaha yake akaenda kuuza vyote alivyokuwa navyo, na kulinunua shamba.
45 “Again, the Kingdom of Heaven is like a man who is a merchant seeking fine pearls,
Tena, ufalme wa mbinguni ni kama mtu anayefanya biashara atafutaye lulu yenye thamani.
46 who having found one pearl of great price, he went and sold all that he had and bought it.
Wakati alipoiona ile yenye thamani, alienda akauza kila kitu alichokuwa nacho na akainunua.
47 “Again, the Kingdom of Heaven is like a dragnet that was cast into the sea and gathered some fish of every kind,
Ufalme wa mbinguni ni kama nyavu iliyo ndani ya bahari, na kwamba hukusanya viumbe vya kila aina.
48 which, when it was filled, fishermen drew up on the beach. They sat down and gathered the good into containers, but the bad they threw away.
Ulipojaa wavuvi waliuvuta ufukweni. Kisha wakakaa chini wakakusanya vitu vyema ndani ya vyombo, lakini visivyo na thamani vilitupwa mbali.
49 So it will be in the consummation of the age (aiōn g165). The angels will come and separate the wicked from among the righteous,
Itakuwa namna hii katika mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenga watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki. (aiōn g165)
50 and will cast them into the furnace of fire. There will be weeping and gnashing of teeth.”
Na kuwatupa ndani ya tanuru ya moto, ambako kutakuwa na maombolezo na kusaga meno.
51 Jesus said to them, “Have you understood all these things?” They answered him, “Yes, Lord.”
Mmefahamu mambo yote haya? Wanafunzi walimjibu, ''Ndiyo.''
52 He said to them, “Therefore every scribe who has been made a disciple in the Kingdom of Heaven is like a man who is a householder, who brings out of his treasure new and old things.”
Kisha Yesu akawambia, ''Kila mwandishi ambaye amekuwa mwanafunzi wa ufalme anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.''
53 When Jesus had finished these parables, he departed from there.
IkawaYesu alipomaliza mifano yote hiyo, akaondoka katika sehemu hiyo.
54 Coming into his own country, he taught them in their synagogue, so that they were astonished and said, “Where did this man get this wisdom and these mighty works?
Kisha Yesu akafika katika mkoa wake na akawafundisha watu katika sinagogi. Matokeo yake ni kuwa walishangaa na kusema, “Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza hii?
55 Is not this the carpenter’s son? Is not his mother called Mary, and his brothers James, Joses, Simon, and Judas?
Mtu huyu siyo mwana wa seremala? Mariamu siyo mamaye? Na ndugu zake siyo Yakobo, Yusuph, Simoni na Yuda?
56 Are not all of his sisters with us? Where then did this man get all of these things?”
Na dada zake tunao hapa petu? Basi mtu huyu ameyapata wapi haya yote?”.
57 They were offended by him. But Jesus said to them, “A prophet is not without honor, except in his own country and in his own house.”
Aliwachukiza. Lakini Yesu aliwambia, “Nabii hakosi kuwa na heshima isipokuwa kwao na katika nchi yao.
58 He did not do many mighty works there because of their unbelief.
Na hakuweza kufanya miujiza mingi kwa sababu hawakuwa na imani naye.

< Matthew 13 >