< Hebrews 3 >

1 Therefore, holy brothers, partakers of a heavenly calling, consider the Apostle and High Priest of our confession: Jesus,
Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
2 who was faithful to him who appointed him, as also Moses was in all his house.
Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
3 For he has been counted worthy of more glory than Moses, because he who built the house has more honor than the house.
Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
4 For every house is built by someone; but he who built all things is God.
Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani—na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
5 Moses indeed was faithful in all his house as a servant, for a testimony of those things which were afterward to be spoken,
Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
6 but Christ is faithful as a Son over his house. We are his house, if we hold fast our confidence and the glorying of our hope firm to the end.
Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
7 Therefore, even as the Holy Spirit says, “Today if you will hear his voice,
Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
8 do not harden your hearts as in the rebellion, in the day of the trial in the wilderness,
msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
9 where your fathers tested me and tried me, and saw my deeds for forty years.
Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
10 Therefore I was displeased with that generation, and said, ‘They always err in their heart, but they did not know my ways.’
Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
11 As I swore in my wrath, ‘They will not enter into my rest.’”
Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko.”
12 Beware, brothers, lest perhaps there might be in any one of you an evil heart of unbelief, in falling away from the living God;
Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
13 but exhort one another day by day, so long as it is called “today”, lest any one of you be hardened by the deceitfulness of sin.
Maadamu hiyo “Leo” inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
14 For we have become partakers of Christ, if we hold the beginning of our confidence firm to the end,
Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
15 while it is said, “Today if you will hear his voice, do not harden your hearts, as in the rebellion.”
Maandiko yasema hivi: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu.”
16 For who, when they heard, rebelled? Was not it all those who came out of Egypt led by Moses?
Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
17 With whom was he displeased forty years? Was not it with those who sinned, whose bodies fell in the wilderness?
Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
18 To whom did he swear that they would not enter into his rest, but to those who were disobedient?
Mungu alipoapa: “Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko,” alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
19 We see that they were not able to enter in because of unbelief.
Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.

< Hebrews 3 >