< Genesis 28 >

1 And Isaac called Jacob, and blessed him, and ordered him, and said to him, Thou shall not take a wife of the daughters of Canaan.
Isaka akamwita Yakobo, akambariki, na kumwagiza, “Usichukuwe mwanamke katika wanawake wa Kikanaani.
2 Arise, go to Paddan-aram, to the house of Bethuel thy mother's father, and take thee a wife from there of the daughters of Laban thy mother's brother.
Inuka, nenda Padani Aramu, katika nyumba ya Bethueli baba wa mama yako, na uchukue mwanamke pale, mmojawapo wa binti za Labani, kaka wa mama yako.
3 And God Almighty bless thee, and make thee fruitful, and multiply thee, that thou may be a company of peoples,
Mungu Mwenyezi na akubariki, akupe uzao na akuzidishe, hata uwe wingi wa watu.
4 and give thee the blessing of Abraham, to thee, and to thy seed with thee, that thou may inherit the land of thy sojourning, which God gave to Abraham.
Na akupe baraka ya Ibrahimu, wewe, na uzao wako baada yako, kwamba uweze kumilki nchi ambapo umekuwa ukiishi, ambayo Mungu alimpa Ibrahimu.”
5 And Isaac sent Jacob away. And he went to Paddan-aram to Laban, son of Bethuel the Syrian, the brother of Rebekah, Jacob's and Esau's mother.
Hivyo Isaka akamwondoa Yakobo. Yakobo akaenda Padani Aramu, kwa Labani mwana wa Bethueli Mwaramu, kaka wa Rebeka, mama yao Yakobo na Esau.
6 Now Esau saw that Isaac had blessed Jacob and sent him away to Paddan-aram, to take for him a wife from there, and that as he blessed him he gave him an order, saying, Thou shall not take a wife of the daughters of Canaan,
Basi Esau alipoona kwamba Isaka amembariki Yakobo na kumpeleka Padani Aramu, kuchukua mke kutoka pale. Lakini pia akaona kwamba Isaka alikuwa amembariki na kumwagiza, akisema, “Usichukue mke katika wanawake wa Kanaani.”
7 and that Jacob obeyed his father and his mother, and was gone to Paddan-aram.
Esau pia akaona kwamba Yakobo alikuwa amemtii baba yake na mama yake, na alikuwa amekwenda Padani Aramu.
8 And Esau saw that the daughters of Canaan did not please Isaac his father.
Esau akaona kwamba wanawake wa Kanaani hawakumpendeza Isaka baba yake.
9 And Esau went to Ishmael, and took, besides the wives that he had, Mahalath the daughter of Ishmael Abraham's son, the sister of Nebaioth, to be his wife.
Hivyo akaenda kwa Ishmaeli, na kuchukua, mbali na wake aliokuwa nao, Mahalathi binti Ishmaeli, mwana wa Ibrahimu, dada wa Nebayothi, kuwa mke wake.
10 And Jacob went out from Beersheba, and went toward Haran.
Yakobo akatoka Beersheba na akaelekea Harani.
11 And he touched upon a certain place, and tarried there all night, because the sun was set. And he took one of the stones of the place, and put it under his head, and lay down in that place to sleep.
Akaja mahali fulani na akakaa pale usiku kucha, kwa kuwa jua lilikuwa limekuchwa. Akachukua mojawapo ya mawe katika eneo hilo, akaliweka chini ya kichwa chake, na akalala usingizi katika eneo hilo.
12 And he dreamed, and, behold, a ladder set up on the earth, and the top of it reached to heaven. And, behold, the agents of God ascending and descending on it.
Akaota na kuona ngazi imewekwa juu ya nchi. Ncha yake ilifika hata mbinguni na malaika wa Mungu walikuwa wakishuka na kupanda juu yake.
13 And, behold, Jehovah stood above it, and said, I am Jehovah, the God of Abraham thy father, and the God of Isaac. The land on which thou lie, to thee I will give it, and to thy seed.
Tazama, Yahwe amesimama juu yake na kusema, “Mimi ni Yahwe, Mungu wa Ibrahimu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nchi uliyolala juu yake, nitakupa wewe na uzao wako.
14 And thy seed shall be as the dust of the earth, and thou shall spread abroad to the west, and to the east, and to the north, and to the south. And in thee and in thy seed shall all the families of the earth be blessed.
Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya ardhi, na utaenea mbali kuelekea magharibi, mashariki, kaskazini, na kusini. Kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa.
15 And, behold, I am with thee, and will keep thee wherever thou go, and will bring thee again into this land. For I will not leave thee, until I have done that which I have spoken to thee of.
Tazama, mimi nipo nawe, na nitakulinda kila uendako, Nitakurudisha katika nchi hii tena; kwani sitakuacha. Nitafanya kila nililokuahidi.”
16 And Jacob awoke out of his sleep, and he said, Surely Jehovah is in this place, and I did not know it.
Yakobo akaamka katika usingizi, na akasema, “Hakika Yahwe yupo mahali hapa, sikujua hili.”
17 And he was afraid, and said, How awesome is this place! This is none other than the house of God, and this is the gate of heaven.
Akaogopa na kusema, “Eneo hili linatisha kama nini! Hili sio kingine zaidi ya nyumba ya Mungu. Hili ni lango la mbinguni.”
18 And Jacob rose up early in the morning, and took the stone that he had put under his head, and set it up for a pillar, and poured oil upon the top of it.
Yakobo akaamka mapema asubuhi na akachukua jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake. Akaliweka kama nguzo na kumimina mafuta juu yake.
19 And he called the name of that place Bethel, but the name of the city was Luz at first.
Akapaita pale Betheli, lakini jina la kawaida la mji lilikuwa Luzu.
20 And Jacob vowed a vow, saying, If God will be with me, and will keep me in this way that I go, and will give me bread to eat, and raiment to put on,
Yakobo akatoa nadhiri, kusema, “Ikiwa Mungu atakuwa nami na atanilinda katika njia nipitayo, na atanipa mkate wa kula, na mavazi ya kuvaa,
21 so that I come again to my father's house in peace, and Jehovah will be my God,
hata nikarudi salama katika nyumba ya baba yangu, ndipo Yahwe atakapokuwa Mungu wangu.
22 then this stone, which I have set up for a pillar, shall be God's house. And of all that thou shall give me I will surely give the tenth to thee.
Kisha jiwe hili nililoliweka kama nguzo litakuwa jiwe takatifu. Kutoka katika kila utakachonipa, kwa hakika nitakupa tena sehemu ya kumi.”

< Genesis 28 >