< Ordsprogene 19 >

1 Bedre Fattigmand med lydefri færd end en, som går Krogveje, er han end rig.
Bora mtu masikini ambaye huenenda katika uadilifu wake kuliko mwenye ukaidi katika maneno yake na ni mpumbavu.
2 At mangle Kundskab er ikke godt, men den træder fejl, som har Hastværk.
Tena, si vizuri kuwa na hamu bila maarifa na mwenye kukimbia haraka sana hukosea njia.
3 Et Menneskes Dårskab øder hans Vej, men på HERREN vredes hans Hjerte.
Upuuzi wa mtu unaharibu maisha yake na moyo wake hughadhabika dhidi ya Yehova.
4 Gods skaffer mange Venner, den ringe skiller hans Ven sig fra.
Utajiri huongeza marafiki wengi, bali mtu masikini hutengwa na rafiki zake.
5 Det falske Vidne undgår ej Straf; den slipper ikke, som farer med Løgn.
Shahidi wa uongo hatakosa adhabu na mwenye kupumua uongo hataokoka.
6 Mange bejler til Stormands Yndest, og alle er Venner med gavmild Mand.
Wengi wataomba fadhila kutoka kwa mtu mkarimu na kila mtu ni rafiki wa yule anayetoa zawadi.
7 Fattigmands Frænder hader ham alle, end mere skyr hans Venner ham da. Ej frelses den, som jager efter Ord.
Mtu masikini huchukiwa na ndugu zake wote; je marafiki wengi kiasi gani hujitenga kutoka kwake! Anawaita, lakini wameondoka.
8 Den, der vinder Vid, han elsker sin Sjæl, og den, der vogter på Indsigt, får Lykke.
Anayepata hekima huyapenda maisha yake mwenyewe; yeye atunzaye ufahamu atapata kilicho chema.
9 Det falske Vidne undgår ej Straf, og den, der farer med Løgn, går under.
Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, bali mwenye kupumua uongo ataangamia.
10 Vellevned sømmer sig ikke for Tåbe, end mindre for Træl at herske over Fyrster.
Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa- wala kwa mtumwa kutawala juu ya wafalme.
11 Klogskab gør Mennesket sindigt, hans Ære er at overse Brøde.
Busara humfanya mtu achelewe kukasirika na utukufu wake ni kusamehe kosa.
12 Som Brøl af en Løve er Kongens Vrede, som Dug på Græs er hans Gunst.
Ghadhabu ya mfalme ni kama muungurumo wa simba kijana, bali fadhila yake ni kama umande kwenye majani.
13 Tåbelig Søn er sin Faders Ulykke, Kvindekiv er som ustandseligt Tagdryp.
Mwana mpumbavu ni uharibifu kwa baba yake na mke mgomvi ni maji yanayochuruzika daima.
14 Hus og Gods er Arv efter Fædre, en forstandig Hustru er fra HERREN.
Nyumba na utajiri ni urithi kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.
15 Dovenskab sænker i Dvale, den lade Sjæl må sulte.
Uvivu unamtupa mtu kwenye usingizi mzito, bali asiyetamani kufanya kazi atakwenda njaa.
16 Den vogter sin Sjæl, som vogter på Budet, men skødesløs Vandel fører til Død.
Yeye anayetii amri huyaongoza maisha yake, bali mtu asiyefikiri juu ya njia zake atakufa.
17 Er man god mod den ringe, låner man HERREN, han gengælder en, hvad godt man har gjort.
Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya.
18 Tugt din Søn, imens der er Håb, ellers stiler du efter at slå ham ihjel.
Mrudi mwanao wakati kuna matumaini na usiwe na shauku ya kumweka katika mauti.
19 Den, som er hidsig, må bøde, ved Skånsel gør man det værre.
Mtu mwenye hasira kali lazima alipe adhabu; kama ukimwokoa, utafanya hivyo mara mbili.
20 Hør på Råd og tag ved Lære, så du til sidst bliver viis.
Sikiliza ushauri na ukubali maelekezo, ili uweze kuwa na hekima mwishoni mwa maisha yako.
21 I Mands Hjerte er mange Tanker, men HERRENs Råd er det, der står fast.
Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
22 Vinding har man af Godhed, hellere fattig end Løgner.
Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
23 HERRENs Frygt er Vej til Liv, man hviler mæt og frygter ej ondt.
Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
24 Den lade rækker til Fadet, men fører ej Hånden til Munden.
Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
25 Får Spottere Hug, bliver tankeløs klog, ved Revselse får den forstandige Kundskab.
Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
26 Mishandle Fader og bortjage Moder gør kun en dårlig, vanartet Søn.
Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
27 Hør op, min Søn, med at høre på Tugt og så fare vild fra Kundskabsord.
Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
28 Niddingevidne spotter Retten, gudløses Mund er glubsk efter Uret.
Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.
29 Slag er rede til Spottere, Hug til Tåbers Ryg.
Hukumu ipo tayari kwa wenye dhihaka na mjeledi kwa migongo ya wapumbavu.

< Ordsprogene 19 >