< Nehemias 3 >

1 Ypperstepræsten Eljasjib og hans Brødre Præsterne tog fat på at bygge Fåreporten; de forsynede den med Bjælkeværk og indsatte Portfløjene; derefter byggede de videre hen til Meatårnet og helligede det og igen videre hen til Hanan'eltårnet.
Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
2 Ved Siden af ham byggede Mændene fra Jeriko, ved Siden af dem Zakkur, Imris Søn.
Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
3 Fiskeporten byggede Sena'as Efterkommere; de forsynede den med Bjælkeværk og indsatte Portfløje, Kramper og Portslåer.
Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
4 Ved Siden af dem arbejdede Meremot, en Søn af Hakkoz's Søn Uruja, med at istandsætte Muren. Ved Siden af ham arbejdede Mesjullam, en Søn af Berekja, en Søn af Mesjezab'el, ved Siden af ham Zadok, Ba'anas Søn.
Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
5 Ved Siden af ham arbejdede Folkene fra Tekoa, men de store iblandt dem bøjede ikke deres Nakke under deres Herres Arbejde.
Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
6 Jesjanaporten istandsatte Jojada, Paseas Søn, og Mesjullam, Besodejas Søn; de forsynede den med Bjælkeværk og indsatte Portfløje, Kramper og Portslåer.
Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
7 Ved Siden af dem arbejdede Gibeoniten Melatja og Meronotiten Jadon sammen med Mændene fra Gibeon og Mizpa, der stod under Statholderen hinsides Floden.
Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati.
8 Ved Siden af ham arbejdede Uzziel, en Søn af Harhaja, en af Guldsmedene. Ved Siden af ham arbejdede Hananja, en af Salvehandlerne; de udbedrede Jerusalem hen til den brede Mur.
Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana.
9 Ved Siden af dem arbejdede Øversten over den ene Halvdel af Jerusalems Område, Refaja, Hurs Søn.
Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
10 Ved Siden af ham arbejdede Jedaja, Harumafs Søn, ud for sit eget Hus. Ved Siden af ham arbejdede Hattusj, Hasjabnejas Søn.
Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
11 En anden Strækningistandsatte Malkija, Harims Søn, og Hassjub, Pahat-Moabs Søn, hen til Ovntårnet.
Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
12 Ved Siden af ham arbejdede Øversten over den anden Halvdel af Jerusalems Område, Sjallum, Hallohesj's Søn, sammen med sine Døtre.
Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
13 Dalporten istandsatte Hanun og Folkene fra Zanoa; de byggede den og indsatte Portfløje, Kramper og Portslåer, og desuden 1000 Alen af Muren hen til Møgporten.
Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.
14 Møgporten istandsatte Øversten over Bet-Kerems Område, Malkija, Rekabs Søn; han byggede den og indsatte Portfløje, Kramper og Portslåer.
Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
15 Kildeporten istandsatte Øversten over Mizpas Område, Sjallun, Kol-Hozes Søn; han byggede den, forsynede den med Tag og indsatte Portfløje, Kramper og Portslåer; han byggede også Muren ved Dammen, fra hvilken Vandledningen fører til Kongens Have, og hen til Trinene, der fører ned fra Davidsbyen.
Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
16 Efter ham arbejdede Øversten over den ene Halvdel af Bet-Zurs Område, Nehemja, Azbuks Søn, hen til Pladsen ud for Davids Grave, til den udgravede Dam og til Kærnetroppernes Hus.
Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
17 Efter ham arbejdede Leviterne, ført af Rehum, Banis Søn. Ved Siden af ham arbejdede Øversten over den ene Halvdel af Ke'ilas Område, Hasjabja.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
18 Efter ham arbejdede deres Bysbørn, ført af Binnuj, Henadads Søn, Øversten over den anden Halvdel af Ke'ilas Område.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
19 Ved Siden af ham istandsatte Øversten over Mizpa, Ezer, Jesuas Søn, en anden Strækning lige ud for Opgangen til Tøjhuset i Hro'en'
Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta.
20 Efter ham istandsatte Baruk, Zabbajs Søn, op ad Bjerget en Strækning fra Krogen til Indgangen til Ypperstepræsten El-jasjibs Hus.
Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
21 Efter ham istandsatte Meremot, en Søn af Hakkoz's Søn Urija, en Strækning fra Indgangen til Eljasjibs Hus til Gavlen.
Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.
22 Efter ham arbejdede Præsterne, Mændene fra Omegnen.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
23 Efter dem arbejdede Binjamin og Hassjub ud for deres Huse. Efter ham arbejdede Azarja, en Søn af Ma'aseja, en Søn af Ananja, ved Siden af sit Hus.
Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
24 Efter ham istandsatte Binnuj, Henadads Søn, en Strækning fra Azarjas Hus til Krogen og til Hjørnet.
Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta.
25 Efter ham arbejdede Palal, Uzajs Søn, lige ud for Krogen og det Tårn, der springer frem fra det øvre kongelige Hus ved Fængselsgården. Efter ham arbejdede Pedaja, Par'osj's Søn,
Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
26 til Stedet ud for Vandporten mod Øst og det fremspringende Tårn.
na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza.
27 Efter ham istandsatte Folkene fra Tekoa en Strækning fra Stedet ud for det store, fremspringende Tårn til Ofels Mur. (På Ofel boede Tempeltrællene).
Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.
28 Over for Hesteporten arbejdede Præsterne, hver lige ud for sit Hus.
Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
29 Efter dem arbejdede Zadok, Immers Søn, ud for sit Hus. Efter ham arbejdede Østportens Vogter Sjemaja, Sjekanjas Søn.
Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
30 Efter ham istandsatte Hananja, Sjelemjas Søn, og Hanun, Zalafs sjette Søn, en Strækning. Efter ham arbejdede Mesjullam, Berekjas Søn, ud for sit Kammer.
Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
31 Efter ham arbejdede Malkija, en af Guldsmedene, hen til Tempeltrællenes Hus. Og Kræmmeme istandsatte Stykket ud for Mifkadporten og hen til Tagbygningen ved Hjørnet.
Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
32 Og mellem Tagbygningen ved Hjørnet og Fåreporten arbejdede Guldsmedene og Kræmmerne.
Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.

< Nehemias 3 >