< 1 Mosebog 10 >

1 Dette er Noas Sønner, Sem, Kam og Jafets Slægtebog. Efter Vandfloden fødtes der dem Sønner.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 Jafets Sønner: Gomer, Magog. Madaj, Javan, Tubal, Mesjek og Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 Gomers Sønner: Asjkenaz, Rifaf og Togarma.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 Javans Sønner: Elisja, Tarsis. Kittæerne og Rodosboerne;
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 fra dem nedstammer de fjerne Strandes Folk. Det var Jafets Sønner i deres Lande, hver med sit Tungemål, efter deres Slægter og i deres Folkeslag.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 Kams Sønner: Kusj, Mlizrajim, Put og Hana'an.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 Kusj's Sønner: Seba, Havila, Sabta, Ra'ma og Sabteka. Ra'mas Sønner: Saba og Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 Og Kusj avlede Nimrod, som var den første Storhersker på Jorden.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 Han var en vældig Jæger for HERRENs Øjne; derfor siger man: "En vældig Jæget for HERRENs Øjne som Nimrod."
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 Fra først af omfattede hans Rige Babel, Erelk, Akkad og Kalne i Sinear;
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 fra dette Land drog han til Assyrien og byggede Nineve, Rehobot- Ir, Kela
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 og Resen mellem Nineve og Kela, det er den store By.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 Mizrajim avlede Luderne, Anamerne, Lehaberne, Naftuherne,
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 Patruserne, Kasluherne, fra hvem Filisterne udgik, og Kaftorerne.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 Kana'an avlede Zidon, hans førstefødte, Het,
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 Jebusiterne, Amoriterne, Girgasjiterne,
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 Hivviterne, Arkiterne, Siniterne,
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 Arvaditerne, Zemariterne og Hamatiterne; men senere bredte Kana'anæernes Slægter sig,
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 så at Kana'anæernes Område strakte sig fra Zidon i Retning af Gerar indtil Gaza, i Retning af Sodoma, Gomorra, Adma, og Zebojim indtil Lasja.
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 Det var Kams Sønner efter deres Slægter og Tungemål i deres Lande og Folk.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 Men også Sem, alle Ebersønnernes Fader, Jafets ældste Broder, fødtes der Sønner.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 Sems Sønner: Elam, Assur, Arpaksjad, Lud og Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 Arams Sønner: Uz, Hul, Geter og Masj.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 Arpaksjad avlede Sjela; Sjela avlede Eber;
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 Eber fødtes der to Sønner; den ene hed Peleg, thi på hans Tid adsplittedes Jordens Befolkning, og hans Broder hed Joktan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 Joktan avlede Almodad, Sjelef, Hazarmavet, Jera,
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 Hadoram, Uzal, Dikla,
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 Obal, Abimael, Saba,
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 Ofir, Havila og Jobab. Alle disse var Joktans Sønner,
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 og deres Bosteder strækker sig fra Mesja i Retning af Sefar, Østens Bjerge.
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 Det var Sems Sønner efter deres Slægter og Tungemål i deres Lande og Folk.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 Det var Noas Sønners Slægter efter deres Nedstamning, i deres Folk; fra dem nedstammer Folkene, som efter Vandfloden bredte sig på Jorden.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< 1 Mosebog 10 >