< Ezekiel 14 >

1 Nogle af Israels ældste kom til mig og satte sig lige over for mig.
Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu.
2 Så kom HERRENs Ord til mig således;
Ndipo neno la Bwana likanijia kusema:
3 Menneskesøn! Disse Mænd har lukket deres Afgudsbilleder ind i deres Hjerte og stillet det, der blev dem Årsag til Skyld, for deres Ansigt - skulde jeg lade mig rådspørge af dem?
“Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote?
4 Tal derfor med dem og sig: Så siger den Herre HERREN: Hver den af Israels Hus, som lukker sine Afgudsbilleder ind i sit Hjerte og sættet det, der blev dem Årsag til Skyld, for sit Ansigt og så kommer til Profeten, ham vil jeg, HERREN, selv svare trods hans mange Afgudsbilleder
Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi Bwana nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu.
5 for at gribe Israels Hus i Hjertet, fordi de faldt fra mig med alle deres Afgudsbilleder.
Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’
6 Sig derfor til Israels Hus: Så siger den Herre HERREN: Vend om, vend eder bort fra eders Afgudsbilleder og vend eders Ansigt bort fra alle eders Vederstyggeligheder!
“Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo!
7 Thi hver den af Israels Hus og af de fremmede, der bor i Israel, som skiller sig fra mig og lukker sine Afgudsbilleder ind i sit Hjerte og sætter det, der blev ham Årsag til Skyld, for sit Ansigt og så kommer til Profeten, for at denne skal rådspørge mig for ham, ham vil jeg, HERREN, selv svare;
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi Bwana nitamjibu mwenyewe.
8 jeg retter mit Åsyn mod den mand og gør ham til Tegn og Mundheld og udrydder ham af mit Folk; og I skal kende, at jeg er HERREN.
Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.
9 Men lader Profeten sig lokke til at sige et Ord, så er det mig, HERREN, der har lokket ham, og jeg udrækker min Hånd imodham og udrydder ham af mit Folk Israel.
“‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi Bwana nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli.
10 De skal begge bære deres Skyld, Spørgeren og Profeten skal være lige skyldige,
Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake.
11 for at Israels Hus ikke mere skal fare vild fra mig og blive urent ved alle sine Overtrædelser; da skal de være mit Folk, og jeg vil være deres Gud, lyder det fra den Herre HERREN.
“‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema Bwana Mwenyezi.’”
12 HERRENs Ord kom til mig således:
Neno la Bwana likanijia kusema,
13 Menneskesøn! Når et Land troløst synder imod mig, og jeg udrækker min Hånd imod det og bryder Brødets Støttestav for det og sender Hungersnød over det og udrydder Folk og Fæ,
“Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao,
14 og disse tre Mænd var i dets Mtidte: Noa, Daniel og Job, så skulde kun de tre redde deres Liv ved deres Retfærdighed, lyder det fra den Herre HERREN.
hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema Bwana Mwenyezi.
15 Eller lader jeg Rovdyr fare igennem Landet og gøre det folketomt, så det bliver øde og ingen tør gå derigennem for de vilde Dyr,
“Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori,
16 og disse tre Mænd var i dets Midte - så sandt jeg lever, lyder det fra den Herre HERREN: De skulde ikke redde deres Sønner eller Døtre; de selv alene skulde reddes, men Landet måtte blive øde.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa.
17 Eller lader jeg Sværdet komme over dette Land og siger: "Sværdet skal fare igennem Landet!" og udrydder Folk og Fæ deraf,
“Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao,
18 og disse tre Mænd var i dets Midte - så sandt jeg lever, lyder det fra den Herre HERREN: De skulde ikke redde deres Sønner eller Døtre; de selv alene skulde reddes.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa.
19 Eller sender jeg Pest over dette Land og udgyder min Harme over det med Blod og udrydder Folk og Fæ deraf,
“Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao,
20 og Noa, Daniel og Job var i dets Midte - så sandt jeg lever, lyder det fra den Herre HERREN: De skulde ikke redde Søn eller Datter; de selv alene skulde redde deres Liv ved deres Retfærdighed.
hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao.
21 Men så siger den Herre HERREN: Og dog, når jeg sender mine fire grumme Straffedomme, Sværd, Hunger, Rovdyr og Pest, over Jerusalem for at udrydde Folk og Fæ deraf,
“Kwa maana hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao!
22 se, da skal der levnes en Flok undslupne, som fører Sønner og Døtre ud derfra; se, de skal drage hid til eder, og I skal se deres Færd og Gerninger; da skal I trøste eder over den Ulykke, jeg har bragt over Jerusalem, alt det, jeg har bragt over det.
Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake.
23 De skal være eder en Trøst, når I ser deres Færd og Gerninger, og I skal skønne, at jeg ikke uden Grund gjorde alt, hvad jeg lod det times, lyder det fra den Herre HERREN.
Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ezekiel 14 >