< Amos 9 >

1 Herren så jeg; han stod ved alteret og sagde: Til Søjlehovedet slår jeg, så Dørens Tærskel ryster. Jeg rammer dem alle i Hovedet, de sidste dræber jeg med Sværd; ingen af dem skal undfly, ingen af dem skal reddes.
Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
2 Bryder de ind i Dødsriget, min Hånd skal hente dem der; stiger de op til Himlen, jeg styrter dem ned derfra; (Sheol h7585)
Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol h7585)
3 skjuler de sig på Karmels Top, jeg finder og henter dem der; gemmer de sig for mig på Havsens Bund, jeg byder Slangen bide dem der;
Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
4 vandrer de som Fanger for deres Fjender, jeg byder Sværdet dræbe dem der. Jeg fæster mit Øje på dem til Ulykke, ikke til Lykke.
Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
5 Herren, Hærskarers HERRE, som rører ved Jorden, så den skælver, så alle, som bor på den, sørger, så den stiger overalt som Nilen og synker som Ægyptens Flod,
Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
6 han, som bygged sin Højsal i Himlen, som fæstned sit Hvælv på Jorden, kalder ad Havets Vande og gyder dem ud over Jorden, HERREN er hans Navn.
yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
7 Er I mig ej som Ætiopiens Børn, Israeliter, lyder det fra HERREN; har jeg ikke ført Israel op fra Ægyptens Land, Filisterne fra Kaftor, Aram fra Kir?
“Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
8 Se, den Herre HERRENs Øjne er vendt mod det syndige Rige, og jeg udsletter det af Jorden. Dog vil jeg ikke helt udslette Jakobs Hus, lyder det fra HERREN;
“Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
9 thi se, jeg byder, at Israels Hus skal sigtes blandt alle Folkene, som man sigter med Sold, uden at et Korn falder til Jorden.
“Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
10 For Sværdet skal alle Syndere i mit Folk dø, de, som siger: "Os når Ulykken ikke; den kommer ikke over os."
Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
11 På hin dag rejser jeg Davids faldne Hytte; jeg tætter dens Revner, opfører, hvad der sank i Grus, og bygger den som i gamle Dage,
“Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
12 så de tager Edoms Rest i Eje og alle de Folk, over hvilke mit Navn er nævnt, lyder det fra HERREN, som fuldbyrder dette.
ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
13 Se, Dage skal komme, lyder det fra HERREN, da Plovmand følger Høstmand i Hælene og Drueperser Sædemand, da Bjergene drypper med Most og alle Høje flyder.
“Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
14 Da vender jeg mit Folk Israels skæbne, og de skal bygge de ødelagte byer og bo deri, de skal plandte vingåre og drikke vinen, anlægge haver og spise frugten.
Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
15 Jeg planter dem i deres jord, og de skal aldrig mere rykkes op af deres jord, som jeg gav dem, siger herren din Gud.
Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.

< Amos 9 >