< Apostelenes gerninger 4 >

1 Men medens de talte til Folket, kom Præsterne og Høvedsmanden for Helligdommen og Saddukæerne over dem,
Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakizungumza na watu, makuhani na mlinzi wa hekalu na masadukayo waliwaendea.
2 da de harmedes over, at de lærte Folket og i Jesus forkyndte Opstandelsen fra de døde.
Walikuwa wameudhika sana kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
3 Og de lagde Hånd på dem og satte dem i Forvaring til den følgende Dag; thi det var allerede Aften.
Waliwakamata na kuwaweka gerezani hadi asubuhi iliyofuata, kwani tayari ilikuwa jioni.
4 Men mange af dem, som havde hørt Ordet, troede, og Tallet på Mændene blev omtrent fem Tusinde.
Lakini watu wengi waliokuwa wamesikia ujumbe waliamini; na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini walikadiliwa kuwa elfu tano.
5 Men det skete Dagen derefter, at deres Rådsherrer og Ældste og skriftkloge forsamlede sig i Jerusalem,
Hata ilipofika asubuhi siku iliyofuata, kwamba wakuu wao, wazee na waandishi, kwa pamoja walikusanyika Yerusalemu.
6 ligeså Ypperstepræsten Annas og Kajfas og Johannes og Alexander og alle, som vare af ypperstepræstelig Slægt.
Anasi kuhani mkuu alikuwepo, na Kayafa, na Yohana, na Iskanda, na wote waliokuwa ni ndugu wa kuhani mkuu.
7 Og de stillede dem midt iblandt sig og spurgte: "Af hvad Magt eller i hvilket Navn have I gjort dette?"
Walipokuwa wamewaweka Petro na Yohana katikati yao, waliwauliza, “Kwa uwezo gani, au kwa jina gani mmefanya hili?”
8 Da sagde Peter, fyldt med den Helligånd, til dem: "I Folkets Rådsherrer og Ældste!
Kisha, Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akawaambia, “Ninyi wakuu wa watu, na wazee,
9 Når vi i Dag forhøres angående denne Velgerning imod en vanfør Mand, om hvorved han er bleven helbredt;
kama sisi siku ya leo tunahojiwa kuhusu tendo jema lililofanywa kwa mtu huyu mgonjwa - kwa namna gani mtu huyu alifanywa mzima?
10 da skal det være eder alle og hele Israels Folk vitterligt, at ved Jesu Kristi Nazaræerens Navn, hvem I have korsfæstet, hvem Gud har oprejst fra de døde, ved dette Navn er det, at denne står rask her for eders Øjne,
Hebu lijulikane hilo kwenu na kwa watu wote katika Israel, kwamba kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye mlimsulibisha, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, ni kwa njia yake kwamba mtu huyu anasimama hapa mbele yenu akiwa mwenye afya.
11 Han er den Sten, som blev agtet for intet af eder, I Bygningsmænd, men som er bleven til en Hovedhjørnesten.
Yesu Kristo ni jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilidharau, lakini ambalo limefanywa kuwa jiwe kuu la pembeni.
12 Og der er ikke Frelse i nogen anden; thi der er ikke noget andet Navn under Himmelen, givet iblandt Mennesker, ved hvilket vi skulle blive frelste."
Hakuna wokovu katika mtu mwingine awaye yote. Kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa watu, ambalo kwa hilo tunaweza kuokolewa.”
13 Men da de så Peters og Johannes Frimodighed og kunde mærke, at de vare ulærde Mænd og Lægfolk, forundrede de sig, og de kendte dem, at de havde været med Jesus.
Sasa walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na wakagundua kwamba walikuwa ni watu wakawaida wasio na elimu, walishangaa, wakafahamu kwamba Petro na Yohana wamekuwa pamoja na Yesu.
14 Og da de så Manden, som var helbredt, stå hos dem, havde de intet at sige derimod.
Kwa sababu walimwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuwa na kitu cha kusema dhidi ya hili.
15 Men de bøde dem at træde ud fra Rådet og rådførte sig med hverandre og sagde:
Lakini walipokuwa wamekwisha kuwaamuru mitume waondoke mbele ya mkutano wa baraza, walizungumza wao kwa wao.
16 "Hvad skulle vi gøre med disse Mennesker? thi at et vitterligt Tegn er sket ved dem, det er åbenbart for alle dem, som bo i Jerusalem, og vi kunne ikke nægte det.
Walisema, tutawafanyaje watu hawa? Ni kweli kwamba muujiza wa ajabu umefanyika kupitia wao unajulikana na kila mmoja anayeishi Yerusalemu; hatuwezi kulikataa hilo.
17 Men for at det ikke skal komme videre ud iblandt Folket, da lader os true dem til ikke mere at tale til noget Menneske i dette Navn."
Lakini, ili kwamba jambo hili lisienee miongoni mwa watu, hebu tuwaonye wasinene tena kwa mtu yeyote kwa jina hili.
18 Og de kaldte dem ind og forbøde dem aldeles at tale eller lære i Jesu Navn.
Waliwaita Petro na Yohana ndani na kuwaamuru kamwe wasinene wala kufundisha kwa jina la Yesu.
19 Men Peter og Johannes svarede og sagde til dem: "Dømmer selv. om det er ret for Gud at lyde eder mere end Gud.
Lakini Petro na Yohana walijibu na kuwaambia, “Kama ni sahihi machoni pa Mungu kuwatii ninyi kuliko Mungu, hukumuni wenyewe.
20 Thi vi kunne ikke lade være at tale om det, som vi have set og hørt."
Maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.”
21 Men de truede dem end mere og løslode dem, da de ikke kunde udfinde, hvorledes de skulde straffe dem, for Folkets Skyld; thi alle priste Gud for det, som var sket.
Baada ya kuwaonya sana Petro na Yohana, waliwaacha waende. Hawakuweza kupata sababu yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetendeka.
22 Thi den Mand, på hvem dette Helbredelsestegn var sket, var mere end fyrretyve År gammel.
Mtu aliyekuwa amepokea muujiza wa uponyaji alipata kuwa na umri zaidi ya miaka arobaini.
23 Da de nu vare løsladte, kom de til deres egne og fortalte dem alt, hvad Ypperstepræsterne og de Ældste havde sagt til dem.
Baada ya kuwaacha huru, Petro na Yohana walikuja kwa watu wao na kuwataarifu yote ambayo makuhani wakuu na wazee walikuwa wamewaambia.
24 Men da de hørte dette, opløftede de endrægtigt Røsten til Gud og sagde: "Herre, du, som har gjort Himmelen og Jorden og Havet og alle Ting, som ere i dem,
Walipoyasikia, walipaza sauti zao kwa pamoja kwa Mungu na kusema, “Bwana, wewe uliyeumba mbingu na dunia na bahari na kila kitu ndani yake,
25 du, som har sagt ved din Tjener Davids Mund: "Hvorfor fnyste Hedninger, og Folkeslag oplagde forfængelige Råd?
wewe ambaye, kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema, “Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?
26 Jordens Konger rejste sig, og Fyrsterne samlede sig til Hobe imod Herren og imod hans Salvede."
Wafalme wa dunia wamejipanga pamoja, na watawala wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya masihi wake.”
27 Ja, de have i Sandhed forsamlet sig i denne Stad imod din hellige Tjener Jesus, hvem du har salvet, både Herodes og Pontius Pilatus tillige med Hedningerne og Israels Folkestammer
Ni hakika, wote Herode na Pontio Pilato, pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika kwa pamoja katika mji huu dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimpaka mafuta.
28 for at gøre det, som din Hånd og dit Råd forud havde bestemt skulde ske.
Walikusanyika kwa pamoja kufanya yote ambayo mkono wako na mapenzi yako yaliyaamuru tangu awali kabla hayajatokea.
29 Og nu, Herre! se til deres Trusler, og giv dine Tjenere at tale dit Ord med al Frimodighed,
Sasa, Bwana, yaangalie matisho yao, na ukawajaalie watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri wote. Ili
30 idet du udrækker din Hånd til Helbredelse, og der sker Tegn og Undere ved din hellige Tjeners Jesu Navn."
kwamba unaponyosha mkono wako kuponya, ishara na maajabu viweze kutokea kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”
31 Og da de havde bedt, rystedes Stedet, hvor de vare forsamlede; og de bleve alle fyldte med den Helligånd, og de talte Guds Ord med Frimodighed.
Walipomaliza kuomba, eneo ambalo walikusanyika kwa pamoja likatikiswa, na wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, na walinena neno la Mungu kwa ujasili.
32 Men de troendes Mængde havde eet Hjerte og een Sjæl; og end ikke een kaldte noget af det, han ejede, sit eget; men de havde alle Ting fælles.
Idadi kubwa ya wale walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja: na hakuna hata mmoja wao aliyesema kwamba chochote alichomiliki kilikuwa cha kwake mwenyewe; badala yake walikuwa na vitu vyote shirika.
33 Og med stor Kraft aflagde Apostlene Vidnesbyrdet om den Herres Jesu Opstandelse, og der var stor Nåde over dem alle.
Kwa nguvu kubwa mitume walikuwa wakiutangaza ushuhuda wao kuhusu ufufuo wa Bwana Yesu, na neema kubwa ilikuwa juu yao wote.
34 Thi der var end ikke nogen trængende iblandt dem; thi alle de, som vare Ejere af Jordstykker eller Huse, solgte dem og bragte Salgssummerne
Hapakuwa na mtu yeyote miongoni mwao aliyepungukiwa na mahitaji, kwa sababu watu wote waliokuwa na hati za viwanja au nyumba, waliviuza na kuleta pesa ya vitu waliyokuwa wameuza
35 og lagde dem for Apostlenes Fødder; men der blev uddelt til enhver, efter hvad han havde Trang til.
na kuviweka chini ya miguu ya mitume. Na mgawanyo ulifanywa kwa kila muumini, kulingana na kila mmoja alivyokuwa na hitaji.
36 Og Josef, som af Apostlene fik Tilnavnet Barnabas, (det er udlagt: Trøstens Søn), en Levit, født på Kypern
Yusufu, mlawi, mtu kutoka Kipro, alipewa jina la Barnabasi na mitume (hiyo ikitafasiriwa, ni mwana wa faraja).
37 som ejede en Jordlod, solgte den og bragte Pengene og lagde dem for Apostlenes Fødder.
Akiwa na shamba, aliliuza na akaleta fedha, akaziweka chini ya miguu ya mitume.

< Apostelenes gerninger 4 >