< 2 Samuel 6 >

1 David samlede alt udsøgt Mandskab i Israel, 30000 Mand.
Tena Daudi akakusanya watu 30,000 wa Israeli waliochaguliwa.
2 Derpå brød David op med alle sine Krigere og drog til Ba'al i Juda for der at hente Guds Ark, over hvilken Hærskarers HERREs Navn er nævnet, han, som troner over Keruberne.
Yeye na watu wake wote wakatoka Baala ya Yuda kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka huko, linaloitwa kwa Jina, naam, jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, ambaye anaketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi walioko juu ya hilo Sanduku.
3 De satte da Guds Ark på en ny Vogn og førte den bort fra Abinadabs Hus på Højen, og Abinadabs Sønner Uzza og Ajo kørte Vognen,
Wakaweka hilo Sanduku la Mungu juu ya gari jipya la kukokotwa na kulileta kutoka nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiongoza hilo gari jipya la kukokotwa
4 således at Uzza gik ved Siden af og Ajo foran Guds Ark.
likiwa na Sanduku la Mungu juu yake, naye Ahio alikuwa anatembea akiwa mbele yake.
5 David og hele Israel legede af alle Kræfter for HERRENs Åsyn til Sang og til Citre, Harper, Pauker, Bjælder og Cymbler.
Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wanacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, zeze, matari, kayamba na matoazi.
6 Men da de kom til Nakons Tærskeplads, rakte Uzza Hånden ud og greb fat i Guds Ark, fordi Okserne snublede.
Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Nakoni, Uza akanyoosha mkono na kulishika Sanduku la Mungu kwa sababu maksai walijikwaa.
7 Da blussede HERRENS Vrede op mod Uzza, og Gud slog ham der, fordi han rakte Hånden ud mod Arken, og han døde på Stedet ved Siden af Guds Ark.
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza kwa sababu ya kitendo chake cha kukosa heshima, kwa hiyo Mungu akampiga akafia papo hapo kando ya Sanduku la Mungu.
8 Men David græmmede sig over, at HERREN havde tilføjet Uzza et Brud. Derfor kaldte man Stedet Perez-Uzza, som det hedder den Dag i Dag.
Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, hivyo hadi leo mahali hapo panaitwa Peres-Uza.
9 Og David grebes den Dag af Frygt for HERREN og sagde: "Hvor kan da HERRENs Ark komme hen hos mig!"
Daudi akamwogopa Bwana siku ile, akasema, “Ni jinsi gani Sanduku la Bwana litakavyoweza kunijia?”
10 Og David vilde ikke flytte HERRENs Ark hen hos sig i Davidsbyen, men lod den sætte ind i Gatiten Obed-Edoms Hus.
Hakuwa radhi kulichukua Sanduku la Bwana kwake katika Mji wa Daudi. Badala yake akalipeleka kwenye nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti.
11 HERRENs Ark blev så i Gatiten Obed-Edoms Hus tre Måneder, og HERREN velsignede Obed-Edom og hele hans Hus.
Sanduku la Bwana likabaki katika nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti, kwa miezi mitatu, naye Bwana akambariki pamoja na nyumba yake yote.
12 Da nu Kong David fik Underretning om, at HERREN for Guds Arks Skyld havde velsignet Obed-Edoms Hus og alt, hvad hans var, gik han hen og lod under Festglæde Guds Ark bringe op fra Obed-Edoms Hus til Davidsbyen.
Kisha Mfalme Daudi akaambiwa, “Bwana ameibariki nyumba ya Obed-Edomu pamoja na kila alicho nacho, kwa sababu ya Sanduku la Mungu.” Basi Daudi akateremka na kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka nyumba ya Obed-Edomu hadi Mji wa Daudi kwa shangwe.
13 Og da de, som bar HERRENs Ark, havde gået seks Skridt, ofrede han en Okse og en Fedekalv.
Wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Bwana walipokuwa wametembea hatua sita, Daudi alitoa dhabihu fahali na ndama aliyenoneshwa.
14 Og David dansede af alle Kræfter for HERRENs Åsyn, iført en linned Efod.
Daudi, akiwa amevaa kisibau cha kitani, alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote,
15 Således bragte David og hele Israel HERRENs Ark op under Festjubel og Hornblæsning.
wakati yeye na nyumba yote ya Israeli walipopandisha Sanduku la Bwana kwa shangwe na sauti za tarumbeta.
16 Men da HERRENs Ark kom til Davidsbyen, så Sauls Datter Mikal ud af Vinduet; og da hun så Kong David springe og danse for HERRENs Åsyn, ringeagtede hun ham i sit Hjerte.
Ikawa Sanduku la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za Bwana, akamdharau moyoni mwake.
17 De førte så HERRENs Ark ind og stillede den på Plads midt i det Telt, David havde rejst den, og David ofrede Brændofre og Takofre for HERRENs Åsyn.
Wakaleta Sanduku la Bwana na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
18 Og da David var færdig med Brændofrene og Takofrene, velsignede han Folket i Hærskarers HERREs Navn
Baada ya kumaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, Daudi akawabariki watu katika jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
19 og uddelte til alt Folket, til hver enkelt af hele Israels Mængde, både Mand og Kvinde, et Brød, et Stykke Kød og en Rosinkage; derpå gik alt Folket hver til sit.
Kisha akatoa mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu kwa kila mtu katika mkutano wote wa Waisraeli, wanaume kwa wanawake. Nao watu wote wakaenda nyumbani kwao.
20 Men da David vendte hjem for at velsigne sit Hus, gik Sauls Datter Mikal ham i Møde og sagde: "Hvor ærbart Israels Konge opførte sig i Dag, da han blottede sig for sine Undersåtters Trælkvinders Øjne, som letfærdige Mennesker plejer at gøre!"
Daudi aliporudi ili kuwabariki watu wa nyumbani mwake, Mikali binti Sauli akatoka nje kumlaki, akamwambia, “Tazama jinsi mfalme wa Israeli alivyojibainisha mwenyewe leo kwa kuvua mavazi yake machoni pa vijakazi wa watumishi wake, kama vile ambavyo mtu asiye na adabu angelifanya!”
21 David svarede Mikal: "For HERRENs Åsyn vil jeg lege, så sandt HERREN lever, som udvalgte mig fremfor din Fader og hele hans Hus, så han satte mig til Fyrste over HERRENs Folk Israel; jeg vil lege for HERRENs Åsyn,
Daudi akamwambia Mikali, “Nilifanya hivyo mbele za Bwana ambaye alinichagua mimi badala ya baba yako au mwingine yeyote kutoka nyumba yake wakati aliponiweka niwe mtawala juu ya Israeli, watu wa Bwana. Kwa hiyo nitacheza mbele za Bwana.
22 selv om jeg derved nedværdiges og synker endnu dybere i dine Øjne; men hos Trælkvinderne, du talte om, skal jeg vinde Ære!"
Nitakuwa asiye na heshima zaidi kuliko sasa, nami nitajishusha machoni pangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliosema habari zao nitaheshimiwa.”
23 Og Sauls Datter Mikal fik til sin Dødedag intet Barn.
Naye Mikali binti Sauli hakuwa na watoto mpaka siku ya kufa kwake.

< 2 Samuel 6 >