< Psalmi 94 >

1 Bože osvetniče, Jahve, Bože osvetniče, pokaži se.
Ee Bwana, ulipizaye kisasi, Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa.
2 Ustani ti što sudiš zemlju, po zasluzi plati oholima!
Ee Mhukumu wa dunia, inuka, uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili.
3 Dokle će bezbošci, Jahve, dokle će se bezbošci hvastati?
Hata lini, waovu, Ee Bwana, hata lini waovu watashangilia?
4 Dokle će brbljati, drsko govoriti, dokle će se bezakonici hvastati?
Wanamimina maneno ya kiburi, watenda mabaya wote wamejaa majivuno.
5 Tlače narod tvoj, Jahve, i baštinu tvoju pritišću;
Ee Bwana, wanawaponda watu wako, wanawaonea urithi wako.
6 kolju udovicu i pridošlicu, sirotama život oduzimlju
Wanamchinja mjane na mgeni, na kuwaua yatima.
7 i govore: “Jahve ne vidi! Ne opaža Bog Jakovljev!”
Nao husema, “Bwana haoni, Mungu wa Yakobo hafahamu.”
8 Shvatite, lude u narodu: bezumni, kad ćete se urazumiti?
Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima?
9 Onaj što uho zasadi da ne čuje? Koji stvori oko da ne vidi?
Je, aliyeweka sikio asisikie? Aliyeumba jicho asione?
10 Onaj što odgaja narode da ne kazni - Onaj što ljude uči mudrosti?
Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu? Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa?
11 Jahve poznaje namisli ljudske: one su isprazne.
Bwana anajua mawazo ya mwanadamu; anajua kwamba ni ubatili.
12 Blago onom koga ti poučavaš, Jahve, i učiš Zakonu svojemu:
Ee Bwana, heri mtu anayeadhibishwa na wewe, mtu unayemfundisha kwa sheria yako,
13 da mu mir udijeliš od nesretnih dana, dok se grob kopa zlikovcu.
unampa utulivu siku za shida, mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa kwa ajili ya mwovu.
14 Jer neće Jahve odbaciti naroda svojega i svoje baštine neće napustiti;
Kwa kuwa Bwana hatawakataa watu wake, hatauacha urithi wake.
15 jer će se pravo dosuditi pravednosti i za njom će ići svi čestiti srcem.
Hukumu itasimamishwa tena kwenye haki, wote walio na mioyo minyofu wataifuata.
16 Tko će ustati za me protiv zlotvora? Tko će se zauzeti za me protiv zločinaca?
Ni nani atakayeinuka dhidi ya mwovu kwa ajili yangu? Ni nani atakayenikinga dhidi ya watenda maovu?
17 Da mi Jahve ne pomaže, brzo bih sišao u mjesto tišine.
Kama Bwana asingelinisaidia upesi, ningelikuwa ninaishi katika ukimya wa kifo.
18 Čim pomislim: “Noga mi posrće”, dobrota me tvoja, o Jahve, podupire.
Niliposema, “Mguu wangu unateleza,” Ee Bwana, upendo wako ulinishikilia.
19 Kad se skupe tjeskobe u srcu mome, tvoje mi utjehe dušu vesele.
Wakati wasiwasi ulipokuwa mwingi ndani yangu, faraja yako ilinipa furaha nafsini mwangu.
20 Zar je bezbožno sudište u savezu s tobom kad nevolje stvara pod izlikom zakona?
Je, kiti cha utawala wa udhalimu kitajiunga nawe, ule utawala uletao taabu kutokana na sheria zake?
21 Nek' samo pritišću dušu pravednog, nek' osuđuju krv nedužnu:
Huungana kuwashambulia wenye haki, kuwahukumu kufa wasio na hatia.
22 Jahve mi je utvrda, Bog - hrid utočišta moga.
Lakini Bwana amekuwa ngome yangu, na Mungu wangu amekuwa mwamba ninaoukimbilia.
23 Platit će im bezakonje njihovo, njihovom će ih zloćom istrijebiti, istrijebit će ih Jahve, Bog naš.
Yeye atawalipa kwa ajili ya dhambi zao na atawaangamiza kwa ajili ya maovu yao; Bwana Mungu wetu atawaangamiza.

< Psalmi 94 >