< Psalmi 18 >

1 Učitelju zbora. Od Jahvina sluge Davida koji Jahvi ispjeva ovu pjesmu u onaj dan kad ga Jahve oslobodi iz ruku neprijatelja Ljubim te, Jahve, kreposti moja!
Nakupenda, Yahwe, nguvu yangu.
2 Jahve, hridino moja, utvrdo moja spase moj; Bože moj, pećino moja kojoj se utječem, štite moj, snago spasenja moga, tvrđavo moja!
Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, yeye ambaye aniwekae kweye usalama; yeye ni Mungu wangu, mwamba wangu; ninapata kimbilio kwake. Yeye ni ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
3 Zazvat ću Jahvu, hvale predostojna, i od dušmana bit ću izbavljen.
Nitamuita Yahwe kwa sababu anastahili kusifiwa, na nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
4 Valovi smrti okružiše mene, prestraviše me bujice pogubne.
Kamba za mauti zilinizunguka, na mafuriko yakimbiayo yalinielemea.
5 Užad Podzemlja sputiše me, smrtonosne zamke padoše na me: (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka; mitego ya mauti ilininasa. (Sheol h7585)
6 u nevolji zazvah Jahvu i Bogu svome zavapih. Iz svog Hrama zov mi začu, i vapaj moj mu do ušiju doprije.
dhiki yangu nilimuita Yahwe; Niliita msaada kwa Mungu. Naye alisikia sauti yangu kutoka hekaluni mwake; kuita kwangu msaada kulienda mpaka uweponi mwake; na kuingia masikioni pake.
7 I zemlja se potrese i uzdrhta, uzdrmaše se temelji gora, pokrenuše se, jer On gnjevom planu.
Kisha nchi ikatikisika na kutetemeka; misingi ya milima pia ilitetemeka na kutikiswa kwa sababu Mungu alikuwa amekasirika.
8 Iz nosnica mu dim se diže, iz usta mu oganj liznu, ugljevlje živo od njega plamsa.
Moshi ulifuka kutoka kwenye pua zake, na moto mkali ulitokea mdomoni mwake. Makaa yaliwashwa kwa moto huo.
9 On nagnu nebesa i siđe, pod nogama oblaci mu mračni.
Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
10 Na keruba stade i poletje; na krilima vjetra zaplovi.
Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
11 Ogrnu se mrakom kao koprenom, prekri se tamnim vodama i oblacima tmastim,
Yahwe alilifanya giza kuwa hema likimzunguka yeye, wingu la mvua zito katika mbingu.
12 od blijeska pred licem njegovim užga se ugljevlje plameno.
Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
13 Jahve s neba zagrmje, Svevišnjega glas se ori.
Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.
14 Odape strijele i dušmane rasu, izbaci munje i na zemlju ih obori.
Yeye aliifyatua mishale yake na kuwatawanya adui zake; na radi nyingi zenye mwanga alizitawanya katika maeneo tofauti tofauti.
15 Morska se dna pokazaše, i temelji svijeta postaše goli od strašne prijetnje Jahvine, od olujna daha gnjeva njegova.
Ndipo mifereji ya maji ilitokea; misingi ya dunia ikadhihirishwa kwa mlio wa pigo lako, Yahwe kwa sauti ya pumzi ya pua zako.
16 On pruži s neba ruku i mene prihvati, iz silnih voda on me izbavi.
Yeye alishuka chini kutokea juu; akanishikilia mimi! Akanivuta nje ya maji yafurikayo.
17 Od protivnika moćnog mene oslobodi, od dušmana mojih jačih od mene.
Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu, kutoka kwa wale ambao walinichukia mimi, kwa kuwa walikuwa na nguvu sana kuliko mimi.
18 Navališe na me u dan zlosretni, ali me Jahve zaštiti,
Wao walikuja kinyume na mimi katika siku ile ya dhiki yangu lakini Mungu alikuwa msaada wangu!
19 na polje prostrano izvede me, spasi me jer sam mu mio.
Yeye aliniweka huru katika eneo pana la wazi; yeye aliniokoa kwa sababu alipenezwa nami.
20 Po pravednosti mojoj Jahve mi uzvrati, po čistoći ruku mojih on me nagradi,
Yahwe amenitunuku mimi kwa sababu ya haki yangu; yeye amenirejesha mimi kwa sababu mikono yangu ilikuwa misafi.
21 jer čuvah putove Jahvine, od Boga se svoga ne udaljih.
Kwa kuwa nimezitunza njia za Yahwe na sijafanya uovu wa kumgeuka Mungu wangu.
22 Odredbe njegove sve su mi pred očima, zapovijedi njegove nisam odbacio,
Kwa kuwa amri zake zote za haki zimekuwa mbele yangu; kama asemavyo, sijaenda kinyume nazo.
23 do srži odan njemu sam bio, čuvam se grijeha svakoga.
Pia nimekuwa sina hatia mbele zake, na nimejiweka mwenyewe mbali na dhambi.
24 Jahve mi po pravdi mojoj vrati, čistoću ruku mojih vidje.
Hivyo Yahwe amenirejesha kwa sababu ya haki yangu, na kwa sababu mikono yangu ilikuwa safi mbele ya macho yake.
25 S prijateljem ti si prijatelj, poštenu poštenjem uzvraćaš.
Kwa yeyote aliye mwaminifu, jionyeshe wenyewe kuwa mwaminifu; kwa mtu asiye na lawama, jionyeshe mwenyewe kuwa usiye na lawama.
26 S čovjekom čistim ti si čist, a lukavca izigravaš,
Kwa yeyote aliye msafi, jionyeshe mwenyewe safi; bali ni mjanja kwa yeyote aliye geuzwa.
27 jer narodu poniženu spasenje donosiš, a ponižavaš oči ohole.
Kwa kuwa wewe huwaokoa watu walio taabishwa, lakini wewe huwashusha chini wale wenye majivuno, yaani macho yaliyo jinua!
28 Jahve, ti moju svjetiljku užižeš, Bože, tminu moju obasjavaš:
Kwa kuwa wewe huipa mwanga taa yangu; Yahwe Mungu wangu hutia mwanga giza langu.
29 s tobom udaram na čete dušmanske, s Bogom svojim preskačem zidine.
Kwa kuwa kwa kupitia wewe ninaweza kuruka juu ya kiwazo kilichowekwa; kupitia Mungu ninaweza kuruka juu ya ukuta.
30 Savršeni su puti Gospodnji, i riječ je Božja ognjem kušana. On, samo on, štit je svima koji se k njemu utječu.
Kama kwa Mungu: njia yake ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi! Yeye ni ngao kwa yeyote anaye kimbilia katika yeye.
31 Jer tko je Bog osim Jahve? Tko li je hridina osim Boga našega?
Kwa kuwa nani ni Mungu ispokuwa Yahwe? Nani ndiye mwamba ispokuwa Mungu wetu?
32 Taj Bog me snagom opasuje, stere mi put besprijekoran,
Ni Mungu anitiaye nguvu ndani yangu kama vile mkanda, ambaye humweka mtu mwenye lawama katika njia yake.
33 noge mi dade brze k'o u košute i postavi me na visine čvrste,
Yeye hunifanya miguu yangu kuwa myepesi kama mbawala na kuniweka mahali pa juu!
34 ruke mi za borbu uvježba i mišice da luk mjedeni napinju.
Yeye hufunza viganja vyangu kwa ajili ya vita na mikono yangu kupiga upinde wa shaba.
35 Daješ mi štit svoj koji spasava, tvoja me desnica drži, tvoja me brižljivost uzvisi.
Wewe umenipa mimi ngao ya wokovu. Mkono wako wa kuume umenisaidia, na neema yako imenifanya kuwa mkubwa.
36 Pouzdanje daješ mom koraku, i noge mi više ne posrću.
Wewe umetengeneza nafasi pana kwa ajili ya miguu yangu ili miguu yangu isiteleze.
37 Pognah svoje dušmane i dostigoh, i ne vratih se dok ih ne uništih.
Ninawashawishi adui zangu na kuwakamata; nami sikurudi nyuma mpaka walipo haribiwa.
38 Obaram ih, ne mogu se dići, padaju, pod nogama mi leže.
Niliwashambulia hata hawakuweza kuamka; nao wameangukia chini ya miguu yangu.
39 Ti me opasa snagom za borbu, a protivnike moje meni podloži.
Kwa kuwa unanitia nguvu kama mshipi kwa ajili ya vita; wewe unawaweka chini yangu wale ambao wanainuka kinyume na mimi.
40 Ti dušmane moje u bijeg natjera, i rasprših one koji su me mrzili.
Wewe ulinipa visogo vya maadui zangu; niliwaagamiza wale walio nichukia.
41 Vapiju u pomoć - nikog da pomogne; vapiju Jahvi - ne odaziva se.
Wao waliita msaada lakini hakuna aliye wasaidia; walimuita Yahwe, lakini hakuwaitikia.
42 Smrvih ih kao prah na vjetru, zgazih ih k'o blato na putu.
Niliwapiga wao katika vipande vidogo vidogo kama vile vumbi mbele ya upepo; niliwatupa nje kama udongo mtaani.
43 Ti me izbavi od bune u mom narodu, postavi me glavarom pogana, puk koji ne poznavah služi mi.
Wewe uliniokoa mimi kutoka katika migogoro ya watu. wewe umenifanya kichwa juu ya mataifa. Watu ambao sikuwahi kuwafahamu huntumikia.
44 Svaki moj šapat pokorno on sluša, sinovi tuđinci meni laskaju;
Pindi tu waliposikia kuhusu mimi, wao walinitii; wageni walilazimishwa kunisujudu.
45 sinovi tuđinski gube srčanost, izlaze dršćuć' iz svojih utvrda.
Wageni walitoka kwenye ngome yao wakitetemeka.
46 Živio Jahve! Blagoslovljena hridina moja! Neka se uzvisi Bog, spasenje moje!
Yahwe anaishi; mwamba wangu usifiwe. Ainuliwe Mungu wa wokovu wangu.
47 Bog koji mi daje osvetu i narode meni pokorava.
Yeye ni Mungu ambaye hutelekeza visasi kwa ajili yangu, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
48 Od dušmana me mojih izbavljaš i nad protivnike me moje izdižeš, ti mene od čovjeka silnika spasavaš.
Nimewekwa huru kutoka kwa adui zangu! wewe uliniinua juu ya wale walioinuka kunyume na mimi! Wewe uliniokoa kutoka kwa watu wenye vurugu.
49 Zato te slavim, Jahve, među pucima i psalam pjevam tvome Imenu:
Kwa hiyo nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya mataifa; Nitaliimbia sifa jina lako!
50 umnožio si pobjede kralju svojemu, pomazaniku svome milost si iskazao, Davidu i potomstvu njegovu navijeke.
Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na yeye huonyesha uaminifu wa agano lake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na ukoo wake milele.

< Psalmi 18 >