< 約翰福音 17 >

1 耶穌說了這話,就舉目望天,說:「父啊,時候到了,願你榮耀你的兒子,使兒子也榮耀你;
Yesu aliyasema mambo haya; kisha akainua macho yake kuelelea mbinguni na akasema, “Baba, saa imewadia; mtukuze mwanao ili na mwana naye akutukuze wewe -
2 正如你曾賜給他權柄管理凡有血氣的,叫他將永生賜給你所賜給他的人。 (aiōnios g166)
kama vile ulivyompatia mamlaka juu ya vyote vyenye mwili ili awape uzima wa milele wale wote uliompatia. (aiōnios g166)
3 認識你-獨一的真神,並且認識你所差來的耶穌基督,這就是永生。 (aiōnios g166)
Huu ndio uzima wa milele: kwamba wakujue wewe, Mungu wa kweli na wa pekee, na yeye uliyemtuma, Yesu Kristo. (aiōnios g166)
4 我在地上已經榮耀你,你所託付我的事,我已成全了。
Nilikutukuza hapa duniani, na kuikamilisha kazi uliyonipa niifanye.
5 父啊,現在求你使我同你享榮耀,就是未有世界以先,我同你所有的榮耀。
Sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja na wewe mwenyewe kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ya ulimwengu kuumbwa.
6 「你從世上賜給我的人,我已將你的名顯明與他們。他們本是你的,你將他們賜給我,他們也遵守了你的道。
Nililifunua jina lako kwa watu ulionipa hapa duniani. Walikuwa watu wako; lakini ulinikabidhi mimi. nao wamelishika neno lako.
7 如今他們知道,凡你所賜給我的,都是從你那裏來的;
Sasa wanajua kuwa kila kitu ulichonipa mimi kinatoka kwako,
8 因為你所賜給我的道,我已經賜給他們,他們也領受了,又確實知道,我是從你出來的,並且信你差了我來。
kwa maneno yale uliyonipatia mimi— Nimekwisha wapatia wao maneno hayo. Waliyapokea na kweli wakajua ya kuwa mimi nimetoka kwako, na wakaamini kuwa wewe ndiye uliyenituma.
9 我為他們祈求,不為世人祈求,卻為你所賜給我的人祈求,因他們本是你的。
Ninawaombea wao. Siuombei ulimwaengu bali wale ulionipa kwa kuwa wao ni wako.
10 凡是我的,都是你的;你的也是我的,並且我因他們得了榮耀。
Vitu vyote ambavyo ni vyangu ni vyako, na vile ulivyonavyo wewe ni vyangu; nami ninatukuzwa katika hivyo.
11 從今以後,我不在世上,他們卻在世上;我往你那裏去。聖父啊,求你因你所賜給我的名保守他們,叫他們合而為一像我們一樣。
Mimi simo tena ulimwenguni, bali wao wamo ulimwenguni, nami sasa naja kwako. Baba Mtakatifu, watunze kwa jina lako lile ulilonipa sisi ili wao nao wawe na umoja, kama vile mimi na wewe tulivyo na umoja.
12 我與他們同在的時候,因你所賜給我的名保守了他們,我也護衛了他們;其中除了那滅亡之子,沒有一個滅亡的,好叫經上的話得應驗。
Nilipokuwa nao, niliwalinda kwa jina ulilonipa; Niliwalinda, na hakuna hata mmoja wao aliyepotea isipokuwa mwana wa upotevu, ili kwamba maandiko yatimie.
13 現在我往你那裏去,我還在世上說這話,是叫他們心裏充滿我的喜樂。
Sasa ninakuja kwako; lakini ninasema haya ulimwenguni ili kwamba furaha yangu ikamilishwe ndani yao wenyewe.
14 我已將你的道賜給他們。世界又恨他們;因為他們不屬世界,正如我不屬世界一樣。
Nimewapa neno lako; ulimwengu imewachukia kwa sababu wao si wa ulimwengu, kama vile mimi nisivyokuwa wa ulimwengu
15 我不求你叫他們離開世界,只求你保守他們脫離那惡者。
Siwaombei kwamba uwatoe ulimwenguni bali uwalinde na yule mwovu.
16 他們不屬世界,正如我不屬世界一樣。
Wao si wa dunia kama vile mimi nisivyokuwa wa ulimwenguni.
17 求你用真理使他們成聖;你的道就是真理。
Uwaweke wakfu kwako mwenyewe katika Kweli; neno lako ndiyo kweli.
18 你怎樣差我到世上,我也照樣差他們到世上。
Ulinituma ulimwenguni, nami nimewatuma ulimwenguni.
19 我為他們的緣故,自己分別為聖,叫他們也因真理成聖。
Kwa ajili yao mimi mwenyewe ninajitoa kwako ili kwamba na wao wajitoe kwako kwa ile kweli.
20 「我不但為這些人祈求,也為那些因他們的話信我的人祈求,
Si hawa tu ninaowaombea, bali na wale watakaoamini kupitia neno lao
21 使他們都合而為一。正如你父在我裏面,我在你裏面,使他們也在我們裏面,叫世人可以信你差了我來。
ili kwamba wao nao wawe na umoja, kama vila wewe Baba, ulivyo ndani yangu nami ndani yako. Nawaombea ili kwamba wao pia waweze kuwa ndani yetu ili ulimwengu uweze kuamini kuwa wewe ndiye uliyenituma.
22 你所賜給我的榮耀,我已賜給他們,使他們合而為一,像我們合而為一。
Utukufu ule ulionipa mimi - nimewapa wao, ili kwamba waweze kuwa na umoja, kama vile sisi tulivyo umoja -
23 我在他們裏面,你在我裏面,使他們完完全全地合而為一,叫世人知道你差了我來,也知道你愛他們如同愛我一樣。
Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili waweze kukamilishwa katika umoja; ili ulimwengu ujue kuwa hakika wewe ndiye uliyenituma, na kuwapenda, kama vile wewe ulivyonipenda, mimi.
24 父啊,我在哪裏,願你所賜給我的人也同我在那裏,叫他們看見你所賜給我的榮耀;因為創立世界以前,你已經愛我了。
Baba, kile ulichonipa mimi - Natamani kwamba wao pia waweze kuwa pamoja nami mahali nilipo ili waweze kuona utukufu wangu, ule ulionipa: kwa kuwa wewe ulinipenda mimi kabla ya kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.
25 公義的父啊,世人未曾認識你,我卻認識你;這些人也知道你差了我來。
Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua wewe, lakini mimi nakujua wewe; na wanajua kwamba ulinituma.
26 我已將你的名指示他們,還要指示他們,使你所愛我的愛在他們裏面,我也在他們裏面。」
Nililifanya jina lako lijulikane kwao, na nitalifanya lijulikane ili kwamba lile pendo ambalo kwalo ulinipenda mimi liweze kuwa ndani yao, na mimi niweze kuwa ndani yao.”

< 約翰福音 17 >