< 诗篇 29 >

1 大卫的诗。 神的众子啊,你们要将荣耀、能力归给耶和华, 归给耶和华!
Zaburi ya Daudi. Mpeni Bwana, enyi mashujaa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
2 要将耶和华的名所当得的荣耀归给他, 以圣洁的妆饰敬拜耶和华。
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
3 耶和华的声音发在水上; 荣耀的 神打雷, 耶和华打雷在大水之上。
Sauti ya Bwana iko juu ya maji; Mungu wa utukufu hupiga radi, Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.
4 耶和华的声音大有能力; 耶和华的声音满有威严。
Sauti ya Bwana ina nguvu; sauti ya Bwana ni tukufu.
5 耶和华的声音震破香柏树; 耶和华震碎黎巴嫩的香柏树。
Sauti ya Bwana huvunja mierezi; Bwana huvunja vipande vipande mierezi ya Lebanoni.
6 他也使之跳跃如牛犊, 使黎巴嫩和西连跳跃如野牛犊。
Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama, Sirioni urukaruke kama mwana nyati.
7 耶和华的声音使火焰分岔。
Sauti ya Bwana hupiga kwa miali ya umeme wa radi.
8 耶和华的声音震动旷野; 耶和华震动加低斯的旷野。
Sauti ya Bwana hutikisa jangwa; Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
9 耶和华的声音惊动母鹿落胎, 树木也脱落净光。 凡在他殿中的,都称说他的荣耀。
Sauti ya Bwana huzalisha ayala, na huuacha msitu wazi. Hekaluni mwake wote wasema, “Utukufu!”
10 洪水泛滥之时,耶和华坐着为王; 耶和华坐着为王,直到永远。
Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika; Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
11 耶和华必赐力量给他的百姓; 耶和华必赐平安的福给他的百姓。
Bwana huwapa watu wake nguvu; Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.

< 诗篇 29 >