< 创世记 9 >

1 神赐福给挪亚和他的儿子,对他们说:“你们要生养众多,遍满了地。
Kisha Mungu akambariki Nuhu na wanawe, na kuwaambia, “Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi.
2 凡地上的走兽和空中的飞鸟都必惊恐,惧怕你们,连地上一切的昆虫并海里一切的鱼都交付你们的手。
Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai juu ya nchi, juu ya kila ndege wa angani, juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi, na juu ya samaki wote wa baharini. Vimetolewa katika mikono yenu.
3 凡活着的动物都可以作你们的食物。这一切我都赐给你们,如同菜蔬一样。
Kila kitu kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula kwa ajili yenu. Kama nilivyo wapa mimea, sasa nawapa kila kitu.
4 惟独肉带着血,那就是它的生命,你们不可吃。
Lakini msile nyama pamoja na uhai wake - yaani damu yake - ndani yake.
5 流你们血、害你们命的,无论是兽是人,我必讨他的罪,就是向各人的弟兄也是如此。
Lakini kwa ajili ya damu yenu, uhai uliomo katika damu yenu nitataka malipo. Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka. Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.
6 凡流人血的,他的血也必被人所流,因为 神造人是照自己的形象造的。
Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa, kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu.
7 你们要生养众多,在地上昌盛繁茂。”
Na hivyo nanyi zaeni na kuongezeka, sambaeni katika inchi yote na muongezeke juu yake.”
8 神晓谕挪亚和他的儿子说:
Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye, akisema,
9 “我与你们和你们的后裔立约,
“Kwa ajili yangu, sikiliza! Ninakwenda kulithibitisha agano langu pamoja nawe na uzao wenu baada yenu,
10 并与你们这里的一切活物—就是飞鸟、牲畜、走兽,凡从方舟里出来的活物—立约。
na kwa kila kiumbe hai kilicho pamoja nawe, pamoja na ndege, mnyama wa kufugwa, na kila kiumbe cha nchi pamoja nawe, kuanzia kwa wote waliotoka kwenye safina, mpaka kwa kila kiumbe hai juu ya nchi.
11 我与你们立约,凡有血肉的,不再被洪水灭绝,也不再有洪水毁坏地了。”
Kwa sababu hii ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi, kwamba hapatatokea kuangamizwa kwa mwenye mwili kwa njia ya maji ya gharika. Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi.”
12 神说:“我与你们并你们这里的各样活物所立的永约是有记号的。
Mungu akasema, “na hii ndiyo ishara ya agano ambalo ninafanya kati yangu na ninyi pamoja na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi, kwa vizazi vyote vya baadaye:
13 我把虹放在云彩中,这就可作我与地立约的记号了。
Nimeweka upinde wangu wa mvua katika wingu, na itakuwa ndiyo ishara ya agano kati yangu na nchi.
14 我使云彩盖地的时候,必有虹现在云彩中,
Hata itakuwa nitakapoleta wingu juu ya nchi na upinde wa mvua ukaonekana katika wingu,
15 我便记念我与你们和各样有血肉的活物所立的约,水就再不泛滥、毁坏一切有血肉的物了。
ndipo nitakumbuka agano langu, ambalo ni kati yangu na ninyi na kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili. Maji hayatafanyika tena gharika kuharibu wote wenye mwili.
16 虹必现在云彩中,我看见,就要记念我与地上各样有血肉的活物所立的永约。”
Upinde wa mvua utakuwa katika mawingu na nitauona, ili kukumbuka agano la milele kati ya Mungu na kila kiumbe hai cha wote wenye mwili ambacho kiko juu ya nchi.”
17 神对挪亚说:“这就是我与地上一切有血肉之物立约的记号了。”
Kisha Mungu akamwambia Nuhu, “Hii ni ishara ya agano ambalo nimelithibitisha kati yangu na wenye mwili wote ambao wako juu ya nchi.”
18 出方舟挪亚的儿子就是闪、含、雅弗。含是迦南的父亲。
Wana wa Nuhu ambao walitoka katika safina walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi. Na Hamu akamzaa kanaani.
19 这是挪亚的三个儿子,他们的后裔分散在全地。
Watatu hawa walikuwa ndio wana wa Nuhu, na kutokea kwa hawa nchi yote ikajaa watu.
20 挪亚作起农夫来,栽了一个葡萄园。
Nuhu akaanza kuwa mkulima, na akapanda mizabibu.
21 他喝了园中的酒便醉了,在帐棚里赤着身子。
Akanywa sehemu ya divai na akalewa. Akawa amelala hemeani uchi.
22 迦南的父亲含看见他父亲赤身,就到外边告诉他两个弟兄。
Kisha Hamu, baba yake na Kanaani, akaona uchi wa baba yake na akawaambia ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 于是闪和雅弗拿件衣服搭在肩上,倒退着进去,给他父亲盖上;他们背着脸就看不见父亲的赤身。
Kwa hiyo Shemu na Yafethi wakachukua kanzu wakaitanda juu ya mabega yao, na wakatembea kinyumenyume na wakaufunika uchi wa baba yao. Nyuso zao zikiwa zimegeuka nyuma upande mwingine, kwa hiyo hawakuona uchi wa baba yao.
24 挪亚醒了酒,知道小儿子向他所做的事,
Nuhu alipozinduka kutoka katika ulevi wake, alijua ni jambo gani mtoto wake mdogo amemfanyia.
25 就说: 迦南当受咒诅, 必给他弟兄作奴仆的奴仆;
Hivyo akasema, “Alaaniwe Kanaani. Na awe mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake.”
26 又说: 耶和华—闪的 神是应当称颂的! 愿迦南作闪的奴仆。
Akasema pia, Yahwe, Mungu wa Shemu, abarikiwe, Kanaani na awe mtumwa wake.
27 愿 神使雅弗扩张, 使他住在闪的帐棚里; 又愿迦南作他的奴仆。
Mungu na apanuwe mipaka ya Yafethi, na afanye makazi yake katika hema za Shemu. Kanaani na awe mtumwa wake.”
28 洪水以后,挪亚又活了三百五十年。
Baada ya gharika, Nuhu aliishi miaka miatatu na hamsini.
29 挪亚共活了九百五十岁就死了。
Siku zote za Nuhu zilikuwa ni miaka mia tisa na hamsini, na kisha alikufa.

< 创世记 9 >