< 詩篇 18 >

1 【凱旋感恩歌】 上主的僕人達味作,向上主唱了這篇詩歌: 上主,我的力量,我愛慕你。
Nakupenda, Yahwe, nguvu yangu.
2 上主,你是我的磐石、我的保障,我的避難所;你是我的天主,我一心依靠的磐石;你是我的護盾,我救恩的角,我的堡壘。
Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, yeye ambaye aniwekae kweye usalama; yeye ni Mungu wangu, mwamba wangu; ninapata kimbilio kwake. Yeye ni ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
3 我一呼求應受頌揚的上主,我便會從仇敵的手中得救。
Nitamuita Yahwe kwa sababu anastahili kusifiwa, na nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
4 死亡的狂瀾環圍著我,凶惡的險波驚嚇著我,
Kamba za mauti zilinizunguka, na mafuriko yakimbiayo yalinielemea.
5 陰府的繩韁纏繞著我,喪命的羅網拘絆著我。 (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka; mitego ya mauti ilininasa. (Sheol h7585)
6 我在急難難當中呼求了上主,向我的天主求助;他由殿中聽我禱告,我的聲音進入祂的耳鼓。
dhiki yangu nilimuita Yahwe; Niliita msaada kwa Mungu. Naye alisikia sauti yangu kutoka hekaluni mwake; kuita kwangu msaada kulienda mpaka uweponi mwake; na kuingia masikioni pake.
7 因為上主憤怒填胸,大地立即戰慄震驚,山基陵根搖撼移動。
Kisha nchi ikatikisika na kutetemeka; misingi ya milima pia ilitetemeka na kutikiswa kwa sababu Mungu alikuwa amekasirika.
8 由祂的鼻孔湧出濃煙,由祂的口中噴出烈焰,由祂身上射出火炭。
Moshi ulifuka kutoka kwenye pua zake, na moto mkali ulitokea mdomoni mwake. Makaa yaliwashwa kwa moto huo.
9 祂使諸天低垂,親自降臨,在祂的腳下面密布濃雲。
Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
10 祂乘坐革魯賓飛揚;藉著風的翼羽翱翔。
Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
11 祂四周以黑暗作帷帳,以含雨的濃雲為屏障。
Yahwe alilifanya giza kuwa hema likimzunguka yeye, wingu la mvua zito katika mbingu.
12 閃電在祂前輝煌,紅炭發出了火光。
Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
13 上主由高天發出雷鳴,至高者吼出祂的呼聲。
Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.
14 祂射出羽箭,將人驅散;祂發出閃電,使人逃竄。
Yeye aliifyatua mishale yake na kuwatawanya adui zake; na radi nyingi zenye mwanga alizitawanya katika maeneo tofauti tofauti.
15 上主的呵斥一呼,鼻孔的怒氣一出,滄海的海底出現,大地的地基露綻。
Ndipo mifereji ya maji ilitokea; misingi ya dunia ikadhihirishwa kwa mlio wa pigo lako, Yahwe kwa sauti ya pumzi ya pua zako.
16 祂由高處伸手將我拉住,祂由洪水之中將我提出;
Yeye alishuka chini kutokea juu; akanishikilia mimi! Akanivuta nje ya maji yafurikayo.
17 救我脫離了我的敵手,擺脫了強於我的仇讎。
Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu, kutoka kwa wale ambao walinichukia mimi, kwa kuwa walikuwa na nguvu sana kuliko mimi.
18 他們在我困厄之日襲擊我,然而上主卻作了我的城堡;
Wao walikuja kinyume na mimi katika siku ile ya dhiki yangu lakini Mungu alikuwa msaada wangu!
19 祂引領我步入廣闊的平原,祂因喜愛我而給了我救援。
Yeye aliniweka huru katika eneo pana la wazi; yeye aliniokoa kwa sababu alipenezwa nami.
20 上主照我的正義酬答了我,按我隻手的清白賞報了我;
Yahwe amenitunuku mimi kwa sababu ya haki yangu; yeye amenirejesha mimi kwa sababu mikono yangu ilikuwa misafi.
21 因我遵行了上主的道路,沒有作惡背棄我的天主。
Kwa kuwa nimezitunza njia za Yahwe na sijafanya uovu wa kumgeuka Mungu wangu.
22 祂的一切法令常在我的眼前,祂的任何誡命我總沒有棄損;
Kwa kuwa amri zake zote za haki zimekuwa mbele yangu; kama asemavyo, sijaenda kinyume nazo.
23 我在祂前常保持成全,我自知防範各種罪愆。
Pia nimekuwa sina hatia mbele zake, na nimejiweka mwenyewe mbali na dhambi.
24 因此,上主我在祂眼前的正道,並我隻手的清白給了我賞報。
Hivyo Yahwe amenirejesha kwa sababu ya haki yangu, na kwa sababu mikono yangu ilikuwa safi mbele ya macho yake.
25 仁慈的人,你待他仁慈;正直的人,你待他正直;
Kwa yeyote aliye mwaminifu, jionyeshe wenyewe kuwa mwaminifu; kwa mtu asiye na lawama, jionyeshe mwenyewe kuwa usiye na lawama.
26 純潔的人,你待他純潔;乖戾的人,你待他乖戾。
Kwa yeyote aliye msafi, jionyeshe mwenyewe safi; bali ni mjanja kwa yeyote aliye geuzwa.
27 卑微的人,你必要救起;傲慢的人,你必要輕視。
Kwa kuwa wewe huwaokoa watu walio taabishwa, lakini wewe huwashusha chini wale wenye majivuno, yaani macho yaliyo jinua!
28 上主,是你使我的燈籠放光,我主,是你把我的黑暗照亮。
Kwa kuwa wewe huipa mwanga taa yangu; Yahwe Mungu wangu hutia mwanga giza langu.
29 仗著你的助祐,我衝上了戰場;靠著我的天主,我跳過了城牆。
Kwa kuwa kwa kupitia wewe ninaweza kuruka juu ya kiwazo kilichowekwa; kupitia Mungu ninaweza kuruka juu ya ukuta.
30 天主的道路是完善的;上主的言語是精鍊的;凡是投奔祂的人,祂必作他的後盾。
Kama kwa Mungu: njia yake ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi! Yeye ni ngao kwa yeyote anaye kimbilia katika yeye.
31 除了上主以外,還有誰是天主?我們天主以外,還有誰是磐石?
Kwa kuwa nani ni Mungu ispokuwa Yahwe? Nani ndiye mwamba ispokuwa Mungu wetu?
32 是天主使我腰纏英武,使我的道路平坦無阻;
Ni Mungu anitiaye nguvu ndani yangu kama vile mkanda, ambaye humweka mtu mwenye lawama katika njia yake.
33 使我的雙腳敏捷與鹿蹄相同,使我能穩立於高山的危峰;
Yeye hunifanya miguu yangu kuwa myepesi kama mbawala na kuniweka mahali pa juu!
34 是祂教導我的手上陣進攻,使我伸出臂膊開張了銅弓。
Yeye hufunza viganja vyangu kwa ajili ya vita na mikono yangu kupiga upinde wa shaba.
35 你把救生的盾賜給了我,你的右手不斷扶持了我,使我日漸強大因你愛我。
Wewe umenipa mimi ngao ya wokovu. Mkono wako wa kuume umenisaidia, na neema yako imenifanya kuwa mkubwa.
36 你為我的腳步拓展了道路,我的雙腳總沒有顛簸躊躇。
Wewe umetengeneza nafasi pana kwa ajili ya miguu yangu ili miguu yangu isiteleze.
37 我追擊我的仇敵,並且把他們捕捉,決不返回,直到將他們除盡滅絕。
Ninawashawishi adui zangu na kuwakamata; nami sikurudi nyuma mpaka walipo haribiwa.
38 我將他們打得一敗塗地,叫他們在我的腳下倒斃。
Niliwashambulia hata hawakuweza kuamka; nao wameangukia chini ya miguu yangu.
39 你使我腰纏英武奮勇作戰,叫敵對我的人都向我就範;
Kwa kuwa unanitia nguvu kama mshipi kwa ajili ya vita; wewe unawaweka chini yangu wale ambao wanainuka kinyume na mimi.
40 使我的敵人在我前轉背逃竄,使我把一切仇恨我的人驅散。
Wewe ulinipa visogo vya maadui zangu; niliwaagamiza wale walio nichukia.
41 他們吶喊,卻沒有人救援,呼號上主,也得不到矜憐。
Wao waliita msaada lakini hakuna aliye wasaidia; walimuita Yahwe, lakini hakuwaitikia.
42 我粉碎他們像風吹的灰塵,我踐踏他們似道上的糞土。
Niliwapiga wao katika vipande vidogo vidogo kama vile vumbi mbele ya upepo; niliwatupa nje kama udongo mtaani.
43 你救我脫離了判亂的人民,又封立了我為列國的元勳,我不認識的民族,也都來給我服務。
Wewe uliniokoa mimi kutoka katika migogoro ya watu. wewe umenifanya kichwa juu ya mataifa. Watu ambao sikuwahi kuwafahamu huntumikia.
44 外邦的子民向我諂媚奉承,一聽到是我,即刻向我服膺。
Pindi tu waliposikia kuhusu mimi, wao walinitii; wageni walilazimishwa kunisujudu.
45 外方的子民驚惶失色,戰戰兢兢走出了堡壘。
Wageni walitoka kwenye ngome yao wakitetemeka.
46 上主萬歲! 願我的磐石備受讚頌!救我的天主備受尊崇!
Yahwe anaishi; mwamba wangu usifiwe. Ainuliwe Mungu wa wokovu wangu.
47 天主,是你為我伸冤復仇,求你使萬民都向我屈服;
Yeye ni Mungu ambaye hutelekeza visasi kwa ajili yangu, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
48 是你拯救我脫離我的仇敵,從凌駕我者的拳下,把我提起,救我免於向我施暴人的手裏。
Nimewekwa huru kutoka kwa adui zangu! wewe uliniinua juu ya wale walioinuka kunyume na mimi! Wewe uliniokoa kutoka kwa watu wenye vurugu.
49 上主,為此,我要在異民中稱謝你,我要對你的聖名讚不已:
Kwa hiyo nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya mataifa; Nitaliimbia sifa jina lako!
50 因為是你使你的君王大獲勝利,對你的受傅者:達味和他的後裔,廣施仁愛慈惠,至於無窮之世。
Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na yeye huonyesha uaminifu wa agano lake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na ukoo wake milele.

< 詩篇 18 >