< ᏉᎳ ᏓᏓᏏ ᎤᏬᏪᎳᏁᎸᎯ 3 >

1 ᏕᎭᏅᏓᏗᏍᏗᏍᎨᏍᏗ ᏧᏃᎯᏳᏗ ᎨᏒ ᏄᏂᎬᏫᏳᏌᏕᎩ ᎠᎴ ᏗᎨᎦᏁᎶᏗ ᎨᏒᎢ, ᎤᏃᎯᏳᎯᏍᏛ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗ ᎨᏒᎢ, ᏂᎪᎯᎸᏉ ᎤᎾᏛᏅᎢᏍᏗ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗ ᎨᏒ ᏂᎦᎥᏉ ᎣᏍᏛ ᏧᏂᎸᏫᏍᏓᏁᏗᏱ.
Wakumbushe watu kuwastahi watawala na wenye mamlaka, kuwatii na kuwa tayari kwa kila namna kutenda mambo yote mema.
2 ᎩᎶ ᎤᏐᏅ ᎤᏂᏃᎮᏗᏱ ᏂᎨᏒᎾ, ᏧᎾᏘᏲᏌᏘ ᏂᎨᏒᎾ ᎢᏳᎾᎵᏍᏙᏗᏱ, ᎤᎾᏓᏅᏘᏍᎩᏂ ᎢᏳᎾᎵᏍᏙᏗᏱ, ᎬᏂᎨᏒ ᎢᏳᏅᏁᏗᏱ ᎾᏂᎥᏉ ᎠᏂᎦᏔᎲ ᎤᏣᏘ ᎤᎾᏓᏅᏘᏳ ᎨᏒᎢ.
Waambie wasimtukane mtu yeyote; bali waishi kwa amani na masikizano, wawe daima wapole kwa kila mtu.
3 ᎢᎬᏒᏰᏃ ᎾᏍᏉ ᎢᎸᎯᏳ ᏥᎨᏒ ᎢᎩᏁᎫ ᎨᏒᎩ, ᏂᎪᎯᏳᏒᎾ, ᎢᎩᎵᏓᏍᏔᏅᎯ, ᎪᎱᏍᏗ ᏕᏓᏛᏁᎲᎩ ᏧᏓᎴᏅᏛ ᎠᏚᎸᏅᏗ ᎨᏒ ᎠᎴ ᎣᏍᏛ ᎠᏓᏓᏅᏓᏗᏍᏗᏍᎩ ᎨᏒᎢ, ᎤᏲ ᎨᏒ ᎠᎴ ᎠᏛᏳᎨᏗ ᎢᏕᎲᎩ, ᎢᎩᏂᏆᏘᏍᏗ, ᎠᎴ ᏗᏓᏓᏂᏆᏘᎯ ᎨᏒᎩ.
Maana, wakati mmoja sisi tulikuwa wapumbavu, wakaidi na wapotovu. Tulikuwa watumwa wa tamaa na anasa za kila aina. Tuliishi maisha ya uovu na wivu; watu walituchukia nasi tukawachukia.
4 ᎠᏎᏃ ᎿᎭᏉ ᎤᏁᎳᏅᎯ ᎢᎩᏍᏕᎵᏍᎩ ᎤᏓᏅᏘᏳ ᎨᏒ ᎠᎴ ᏴᏫ ᏚᎨᏳᏒ ᎤᎦᏄᎪᏨ,
Lakini wakati wema na upendo wa Mungu, Mwokozi wetu, ulipofunuliwa,
5 ᎥᏝ ᏚᏳᎪᏛ ᏗᎦᎸᏫᏍᏓᏁᏗ ᎨᏒ ᎬᏗ ᎠᏴ ᎾᏍᎩ ᏕᎩᎸᏫᏍᏓᏁᎸᎢ, ᎾᏍᎩᏯᏍᎩᏂ ᎤᏓᏙᎵᏣᏘᏳ ᎨᏒ ᎢᎩᏍᏕᎸᎲᎩ ᎤᏮᏔᏅᎩ ᏔᎵᏁ ᎠᏕᏗ ᎨᏒ ᎤᎬᏩᎵ ᎠᏙᏑᎴᏗᏱ, ᎠᎴ ᎦᎸᏉᏗᏳ ᎠᏓᏅᏙ ᎤᏓᏁᏟᏴᏍᏗ ᎨᏒᎢ;
alituokoa. alituokoa si kwa sababu ya jambo lolote jema tulilotenda sisi, bali alituokoa kwa sababu ya huruma yake, kwa njia ya Roho Mtakatifu anayetujalia tuzaliwe upya na kuwa na maisha mapya kwa kutuosha kwa maji.
6 ᎾᏍᎩ ᎤᏧᏈᏍᏗ ᏥᎩᏐᏅᏰᎵ, ᏥᏌ ᎦᎶᏁᏛ ᎢᎩᏍᏕᎵᏍᎩ ᎢᏳᏩᏂᏌᏛ;
Mungu alitumiminia Roho Mtakatifu bila kipimo kwa njia ya Yesu Kristo, Mwokozi wetu,
7 ᎾᏍᎩ ᎬᏩᎦᏘᏯ ᎤᏓᏙᎵᏍᏗ ᎨᏒ ᏗᎦᏚᏓᎴᏍᏔᏅᎯ ᎨᏒᎢ, ᎾᏍᎩ ᎾᏍᎩᏯ ᎤᎵᏍᏆᏗᏍᏗ ᏂᎨᏒᎾ ᎬᏂᏛ ᎢᎦᏤᎵ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗᏱ ᎾᏍᎩᏯ ᎤᏚᎩ ᎢᎬᏒᎢ. (aiōnios g166)
ili kwa neema yake tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na kuupokea uzima wa milele tunaoutumainia. (aiōnios g166)
8 ᎤᏙᎯᏳᎯᏯ ᎢᎦᏪᏛ; ᎠᎴ ᎾᏍᎩ ᎯᎠ ᏧᏓᎴᏅᏛ ᎠᏆᏚᎵᎭ ᏣᏍᏓᏱᏗᏍᏗᏱ, ᎾᏍᎩ Ꮎ ᎤᏁᎳᏅᎯ ᎤᏃᎯᏳᏅᎯ ᎤᎾᎦᏌᏯᏍᏙᏗᏱ ᏂᎪᎯᎸᏉ ᎣᏍᏛ ᏧᏂᎸᏫᏍᏓᏁᏗᏱ. ᎯᎠ ᎾᏍᎩ ᎣᏏᏳ ᎠᎴ ᎬᏩᎾᎵᏍᏕᎸᏙᏗ ᏴᏫ.
Jambo hili ni kweli. Ninakutaka uyatilie mkazo mambo haya, ili wale wanaomwamini Mungu, wawe na hamu ya kuutumia wakati wao katika kutenda mema, ambayo ni mambo mazuri na ya manufaa kwa watu.
9 ᎤᎵᏍᎦᏂᏍᏛᏍᎩᏂ ᎧᏃᎮᎸᏗ ᎨᏒ ᎠᎴ ᎤᎾᏓᏁᏟᏴᏒᏒᎢ, ᎠᎴ ᏗᏘᏲᏍᏗ ᎨᏒᎢ, ᎠᎴ ᎠᏗᏒᏍᏗ ᎨᏒ ᏗᎧᎿᎭᏩᏛᏍᏗ ᎤᎬᏩᎵ ᏕᎭᏓᏅᏒᎮᏍᏗ, ᎬᏩᎾᏓᏍᏕᎸᏗᏰᏃ ᏂᎨᏒᎾ ᎠᎴ ᎠᏎᏉᏉ ᎾᏍᎩ.
Lakini jiepushe na ubishi wa kipumbavu, ugomvi na mabishano juu ya Sheria. Mambo hayo hayana faida yoyote na ni ya bure tu.
10 ᎩᎶ ᏗᎦᎴᏅᏗᏍᎩ ᏌᏉ ᎠᎴ ᏔᎵ ᎢᏯᎨᏯᏔᏅᎯ ᎨᏎᏍᏗ ᎡᏥᏲᎢᏎᎸᎭ;
Mtu anayesababisha mafarakano mpe onyo la kwanza na la pili, kisha achana naye.
11 ᎢᏥᎦᏔᎮᏍᏗ ᎾᏍᎩ Ꮎ ᏱᏄᏍᏗ ᎩᎶ ᎤᎪᎸᏛ ᎨᏒᎢ, ᎠᎴ ᎤᏍᎦᏅᏨᎢ, ᎤᏩᏒᏉ ᏓᏓᏚᎪᏓᏁᎲᎢ.
Wajua kwamba mtu wa namna hiyo amepotoka kabisa, na dhambi zake zathibitisha kwamba amekosea.
12 ᎢᏳᏃ ᎠᏘᎹ ᏥᏅᏒᎭ ᏫᏣᎷᏤᏗᏱ, ᎠᎴ ᏗᎩᎦ, ᎭᏟᏂᎬᏁᎸᎭ ᎾᎪᏆᎵ ᏍᎩᎷᏤᏗᏱ; ᎾᎿᎭᏰᏃ ᏓᏇᎪᏔᏅ ᎠᏆᎪᎳᏗᏴᏗᏱ.
Baada ya kumtuma kwako Artema au Tukiko, fanya bidii kuja Nikopoli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
13 ᏥᎾ ᏗᎧᎿᎭᏩᏛᏍᏗ ᏗᎪᏏᏏᏍᎩ ᎠᎴ ᎠᏉᎳ ᎭᏟᏂᎬᏁᎸᎭ ᎩᏍᏕᎸᏗᏱ ᎠᎾᎢᏒᎢ, ᎾᏍᎩ ᎪᎱᏍᏗ ᏄᏂᏂᎬᏎᎲᎾ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗᏱ.
Jitahidi kumsaidia mwana sheria Zena na Apolo ili waweze kuanza ziara zao na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji.
14 ᎠᎴ ᎾᏍᏉ ᏗᎦᏤᎵᎦ ᏩᎾᏕᎶᏆ ᏂᎪᎯᎸ ᎣᏍᏛ ᏧᏂᎸᏫᏍᏓᏁᏗᏱ ᎾᏍᎩ ᎤᏚᎸᏗ ᏂᎦᎵᏍᏗᏍᎬ ᎪᎱᏍᏗ ᎬᏔᏂᏓᏍᏗ, ᎾᏍᎩ ᎠᏂᏁᏉᏍᎩ ᎢᏳᎾᎵᏍᏙᏗᏱ.
Ni lazima watu wetu wajifunze kuutumia wakati wao katika kutenda mema ili wasaidie katika mahitaji ya kweli, na maisha yao yawe ya kufaa.
15 ᏂᎦᏛ ᎠᏂ ᏃᎦᏛᏅᎢ ᏫᎨᏣᏲᎵᎦ. ᏕᎯᏲᎵᎸᎭ ᎾᏍᎩ Ꮎ ᎨᎩᎨᏳᎯ ᎪᎯᏳᏗ ᎨᏒ ᏅᏗᎦᎵᏍᏙᏗᏍᎬᎢ. ᎬᏩᎦᏘᏯ ᎤᏓᏙᎵᏍᏗ ᎨᏒ ᎢᏤᎳᏗᏙᎮᏍᏗ ᏂᏥᎥᎢ. ᎡᎺᏅ.
Watu wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu katika imani. Nawatakieni nyote neema ya Mungu.

< ᏉᎳ ᏓᏓᏏ ᎤᏬᏪᎳᏁᎸᎯ 3 >