< ᏉᎳ ᏓᏓᏏ ᎤᏬᏪᎳᏁᎸᎯ 3 >

1 ᏕᎭᏅᏓᏗᏍᏗᏍᎨᏍᏗ ᏧᏃᎯᏳᏗ ᎨᏒ ᏄᏂᎬᏫᏳᏌᏕᎩ ᎠᎴ ᏗᎨᎦᏁᎶᏗ ᎨᏒᎢ, ᎤᏃᎯᏳᎯᏍᏛ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗ ᎨᏒᎢ, ᏂᎪᎯᎸᏉ ᎤᎾᏛᏅᎢᏍᏗ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗ ᎨᏒ ᏂᎦᎥᏉ ᎣᏍᏛ ᏧᏂᎸᏫᏍᏓᏁᏗᏱ.
Wakumbushe watu kuwanyenyekea watawala na kuwatii wenye mamlaka, wawe tayari kutenda kila lililo jema.
2 ᎩᎶ ᎤᏐᏅ ᎤᏂᏃᎮᏗᏱ ᏂᎨᏒᎾ, ᏧᎾᏘᏲᏌᏘ ᏂᎨᏒᎾ ᎢᏳᎾᎵᏍᏙᏗᏱ, ᎤᎾᏓᏅᏘᏍᎩᏂ ᎢᏳᎾᎵᏍᏙᏗᏱ, ᎬᏂᎨᏒ ᎢᏳᏅᏁᏗᏱ ᎾᏂᎥᏉ ᎠᏂᎦᏔᎲ ᎤᏣᏘ ᎤᎾᏓᏅᏘᏳ ᎨᏒᎢ.
Wasimnenee mtu yeyote mabaya, wasiwe wagomvi, bali wawe wapole, wakionyesha unyenyekevu kwa watu wote.
3 ᎢᎬᏒᏰᏃ ᎾᏍᏉ ᎢᎸᎯᏳ ᏥᎨᏒ ᎢᎩᏁᎫ ᎨᏒᎩ, ᏂᎪᎯᏳᏒᎾ, ᎢᎩᎵᏓᏍᏔᏅᎯ, ᎪᎱᏍᏗ ᏕᏓᏛᏁᎲᎩ ᏧᏓᎴᏅᏛ ᎠᏚᎸᏅᏗ ᎨᏒ ᎠᎴ ᎣᏍᏛ ᎠᏓᏓᏅᏓᏗᏍᏗᏍᎩ ᎨᏒᎢ, ᎤᏲ ᎨᏒ ᎠᎴ ᎠᏛᏳᎨᏗ ᎢᏕᎲᎩ, ᎢᎩᏂᏆᏘᏍᏗ, ᎠᎴ ᏗᏓᏓᏂᏆᏘᎯ ᎨᏒᎩ.
Maana sisi wenyewe wakati fulani tulikuwa wajinga, wasiotii, tukiwa watumwa wa tamaa mbaya na anasa za kila aina. Tuliishi katika uovu na wivu, tukichukiwa na kuchukiana sisi kwa sisi.
4 ᎠᏎᏃ ᎿᎭᏉ ᎤᏁᎳᏅᎯ ᎢᎩᏍᏕᎵᏍᎩ ᎤᏓᏅᏘᏳ ᎨᏒ ᎠᎴ ᏴᏫ ᏚᎨᏳᏒ ᎤᎦᏄᎪᏨ,
Lakini wema na upendo wa Mungu Mwokozi wetu ulipofunuliwa,
5 ᎥᏝ ᏚᏳᎪᏛ ᏗᎦᎸᏫᏍᏓᏁᏗ ᎨᏒ ᎬᏗ ᎠᏴ ᎾᏍᎩ ᏕᎩᎸᏫᏍᏓᏁᎸᎢ, ᎾᏍᎩᏯᏍᎩᏂ ᎤᏓᏙᎵᏣᏘᏳ ᎨᏒ ᎢᎩᏍᏕᎸᎲᎩ ᎤᏮᏔᏅᎩ ᏔᎵᏁ ᎠᏕᏗ ᎨᏒ ᎤᎬᏩᎵ ᎠᏙᏑᎴᏗᏱ, ᎠᎴ ᎦᎸᏉᏗᏳ ᎠᏓᏅᏙ ᎤᏓᏁᏟᏴᏍᏗ ᎨᏒᎢ;
alituokoa, si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyotenda, bali kwa sababu ya rehema zake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa mara ya pili na kwa kufanywa wapya kwa njia ya Roho Mtakatifu,
6 ᎾᏍᎩ ᎤᏧᏈᏍᏗ ᏥᎩᏐᏅᏰᎵ, ᏥᏌ ᎦᎶᏁᏛ ᎢᎩᏍᏕᎵᏍᎩ ᎢᏳᏩᏂᏌᏛ;
ambaye Mungu alitumiminia kwa wingi kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu,
7 ᎾᏍᎩ ᎬᏩᎦᏘᏯ ᎤᏓᏙᎵᏍᏗ ᎨᏒ ᏗᎦᏚᏓᎴᏍᏔᏅᎯ ᎨᏒᎢ, ᎾᏍᎩ ᎾᏍᎩᏯ ᎤᎵᏍᏆᏗᏍᏗ ᏂᎨᏒᎾ ᎬᏂᏛ ᎢᎦᏤᎵ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗᏱ ᎾᏍᎩᏯ ᎤᏚᎩ ᎢᎬᏒᎢ. (aiōnios g166)
ili kwamba, tukiisha kuhesabiwa haki kwa neema yake, tupate kuwa warithi tukiwa na tumaini la uzima wa milele. (aiōnios g166)
8 ᎤᏙᎯᏳᎯᏯ ᎢᎦᏪᏛ; ᎠᎴ ᎾᏍᎩ ᎯᎠ ᏧᏓᎴᏅᏛ ᎠᏆᏚᎵᎭ ᏣᏍᏓᏱᏗᏍᏗᏱ, ᎾᏍᎩ Ꮎ ᎤᏁᎳᏅᎯ ᎤᏃᎯᏳᏅᎯ ᎤᎾᎦᏌᏯᏍᏙᏗᏱ ᏂᎪᎯᎸᏉ ᎣᏍᏛ ᏧᏂᎸᏫᏍᏓᏁᏗᏱ. ᎯᎠ ᎾᏍᎩ ᎣᏏᏳ ᎠᎴ ᎬᏩᎾᎵᏍᏕᎸᏙᏗ ᏴᏫ.
Hili ni neno la kuaminiwa. Nami nataka uyasisitize mambo haya, ili wale ambao wamemwamini Mungu wapate kuwa waangalifu kujitoa kwa ajili ya kutenda mema wakati wote. Mambo haya ni mazuri tena ya manufaa kwa kila mtu.
9 ᎤᎵᏍᎦᏂᏍᏛᏍᎩᏂ ᎧᏃᎮᎸᏗ ᎨᏒ ᎠᎴ ᎤᎾᏓᏁᏟᏴᏒᏒᎢ, ᎠᎴ ᏗᏘᏲᏍᏗ ᎨᏒᎢ, ᎠᎴ ᎠᏗᏒᏍᏗ ᎨᏒ ᏗᎧᎿᎭᏩᏛᏍᏗ ᎤᎬᏩᎵ ᏕᎭᏓᏅᏒᎮᏍᏗ, ᎬᏩᎾᏓᏍᏕᎸᏗᏰᏃ ᏂᎨᏒᎾ ᎠᎴ ᎠᏎᏉᏉ ᎾᏍᎩ.
Lakini jiepushe na maswali ya kipuzi, mambo ya koo, mabishano na ugomvi kuhusu sheria, kwa sababu hayana faida, tena ni ubatili.
10 ᎩᎶ ᏗᎦᎴᏅᏗᏍᎩ ᏌᏉ ᎠᎴ ᏔᎵ ᎢᏯᎨᏯᏔᏅᎯ ᎨᏎᏍᏗ ᎡᏥᏲᎢᏎᎸᎭ;
Mtu anayesababisha mafarakano, mwonye mara ya kwanza, kisha mwonye mara ya pili. Baada ya hapo, usihusike naye tena.
11 ᎢᏥᎦᏔᎮᏍᏗ ᎾᏍᎩ Ꮎ ᏱᏄᏍᏗ ᎩᎶ ᎤᎪᎸᏛ ᎨᏒᎢ, ᎠᎴ ᎤᏍᎦᏅᏨᎢ, ᎤᏩᏒᏉ ᏓᏓᏚᎪᏓᏁᎲᎢ.
Kwa kuwa unajua kwamba mtu kama huyo amepotoka na tena ni mwenye dhambi. Yeye amejihukumu mwenyewe.
12 ᎢᏳᏃ ᎠᏘᎹ ᏥᏅᏒᎭ ᏫᏣᎷᏤᏗᏱ, ᎠᎴ ᏗᎩᎦ, ᎭᏟᏂᎬᏁᎸᎭ ᎾᎪᏆᎵ ᏍᎩᎷᏤᏗᏱ; ᎾᎿᎭᏰᏃ ᏓᏇᎪᏔᏅ ᎠᏆᎪᎳᏗᏴᏗᏱ.
Mara nitakapomtuma Artema au Tikiko kwako, jitahidi kuja unione huko Nikopoli, kwa sababu nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
13 ᏥᎾ ᏗᎧᎿᎭᏩᏛᏍᏗ ᏗᎪᏏᏏᏍᎩ ᎠᎴ ᎠᏉᎳ ᎭᏟᏂᎬᏁᎸᎭ ᎩᏍᏕᎸᏗᏱ ᎠᎾᎢᏒᎢ, ᎾᏍᎩ ᎪᎱᏍᏗ ᏄᏂᏂᎬᏎᎲᎾ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗᏱ.
Fanya kila uwezalo uwasafirishe Zena yule mwanasheria na Apolo na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji katika safari yao.
14 ᎠᎴ ᎾᏍᏉ ᏗᎦᏤᎵᎦ ᏩᎾᏕᎶᏆ ᏂᎪᎯᎸ ᎣᏍᏛ ᏧᏂᎸᏫᏍᏓᏁᏗᏱ ᎾᏍᎩ ᎤᏚᎸᏗ ᏂᎦᎵᏍᏗᏍᎬ ᎪᎱᏍᏗ ᎬᏔᏂᏓᏍᏗ, ᎾᏍᎩ ᎠᏂᏁᏉᏍᎩ ᎢᏳᎾᎵᏍᏙᏗᏱ.
Watu wetu hawana budi kujifunza kutenda mema, ili waweze kuyakimu mahitaji ya kila siku, wasije wakaishi maisha yasiyokuwa na matunda.
15 ᏂᎦᏛ ᎠᏂ ᏃᎦᏛᏅᎢ ᏫᎨᏣᏲᎵᎦ. ᏕᎯᏲᎵᎸᎭ ᎾᏍᎩ Ꮎ ᎨᎩᎨᏳᎯ ᎪᎯᏳᏗ ᎨᏒ ᏅᏗᎦᎵᏍᏙᏗᏍᎬᎢ. ᎬᏩᎦᏘᏯ ᎤᏓᏙᎵᏍᏗ ᎨᏒ ᎢᏤᎳᏗᏙᎮᏍᏗ ᏂᏥᎥᎢ. ᎡᎺᏅ.
Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale wanaotupenda katika imani. Neema iwe nanyi nyote. Amen.

< ᏉᎳ ᏓᏓᏏ ᎤᏬᏪᎳᏁᎸᎯ 3 >