< ᎣᏍᏛ ᎧᏃᎮᏛ ᎹᎦ ᎤᏬᏪᎳᏅᎯ 13 >

1 ᎦᏄᎪᎮᏃ ᎤᏛᏅ-ᏗᎦᎳᏫᎢᏍᏗᏱ, ᎠᏏᏴᏫ ᎾᏍᎩ ᎬᏩᏍᏓᏩᏗᏙᎯ ᎯᎠ ᏄᏪᏎᎴᎢ, ᏔᏕᏲᎲᏍᎩ, ᎬᏂᏳᏉ Ꮎ ᏂᏕᎤᏍᏗ ᏅᏯ ᎠᎴ ᏂᏕᎤᏍᏗ ᏓᏓᏁ-ᎸᎢ?
Yesu alipokuwa anatoka Hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake alimwambia, “Mwalimu, tazama jinsi mawe haya na majengo haya yalivyo ya ajabu!”
2 ᏥᏌᏃ ᎤᏁᏨ ᎯᎠ ᏄᏪᏎᎴᎢ, ᏕᎯᎪᏩᏗᏍᎪ ᎯᎠ ᎾᏍᎩ ᏤᏆ ᏓᏓᏁᎸᎢ? ᎥᏝ ᏌᏉ ᏅᏯ ᎧᏃᎯᏴᎯ ᏱᎨᏎᏍᏗ ᏱᏚᏓᏌᏝᎮᏍᏗ, ᎾᏍᎩ ᏂᎪᎲᏔᏅᎾ ᏱᎨᏎᏍᏗ.
Yesu akamwambia, “Je, unayaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitabomolewa.”
3 ᎣᎵᏩᏲᏃ ᎤᏌᎯᎸ ᎤᏬᎸᎢ, ᎤᏛᏅᏗᎦᎳᏫᎢᏍᏗᏱ ᎠᏓᏁᎸ ᏧᏳᎪᏗ, ᏈᏓ, ᎠᎴ ᏥᎻ, ᎠᎴ ᏣᏂ, ᎠᎴ ᎡᏂᏗ, ᎤᏅᏒ ᎨᏒ ᎬᏩᏛᏛᏁᎢ, ᎯᎠ ᏄᏂᏪᏎᎢ,
Yesu alipokuwa ameketi juu ya mlima wa Mizeituni akielekea Hekalu, Petro, Yakobo, Yohane na Andrea wakamwuliza kwa faragha,
4 ᏍᎩᏃᎲᏏ, ᎢᎳᎩᏳ ᎾᏍᎩ ᎯᎠ ᏅᏓᎦᎵᏍᏔᏂ? ᎠᎴ ᎦᏙ ᎤᏰᎸᏛ ᎨᏎᏍᏗ ᎾᎯᏳ ᎯᎠ ᎾᏍᎩ ᏂᎦᏛ ᎤᎵᏰᎢᎶᎯᏍᏗ ᎨᏒᎢ?
“Twambie mambo haya yatatukia lini? Ni ishara gani itakayoonyesha kwamba mambo haya karibu yatimizwe?”
5 ᏥᏌᏃ ᏚᏁᏤᎸ, ᎤᎴᏅᎮ ᎯᎠ ᏄᏪᏎᎢ, ᎢᏤᏯᏔᎮᏍᏗ, ᏞᏍᏗ ᎩᎶ ᏥᏥᎶᏄᎮᎵ.
Yesu akaanza kuwaambia, “Jihadharini msije mkadanganywa na mtu.
6 ᎤᏂᏣᏖᏍᏗᏰᏃ ᎠᏴ ᏓᏆᏙᏍᏛ ᎠᏂᎷᎯᏍᏗᏍᎨᏍᏗ, ᎯᎠ ᎾᏂᏪᏍᎨᏍᏗ, ᎠᏴ ᎾᏍᎩ; ᎠᎴ ᎤᏂᏣᏖᏍᏗ ᏓᏂᎶᏄᎮᏍᎨᏍᏗ.
Maana wengi watakuja wakilitumia jina langu, wakisema, Mimi ndiye! nao watawapotosha watu wengi.
7 ᎢᏣᏛᎩᏍᎨᏍᏗᏃ ᏓᏅᏩ, ᎠᎴ ᎠᏂᏃᎮᎵᏙᎲ ᏓᏅᏩ, ᏞᏍᏗ ᏱᏣᏕᏯᏔᏁᎮᏍᏗ; ᎾᏍᎩᏰᏃ ᎠᏎ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗ; ᎤᎵᏍᏆᏗᏍᏗᏱᏍᎩᏂ ᎨᏒ ᎠᏏ ᎨᏎᏍᏗ.
Mtakaposikia juu ya vita na fununu za vita, msifadhaike. Mambo hayo lazima yatokee, lakini mwisho wenyewe ungali bado.
8 ᏧᎾᏓᎴᏛᏰᏃ ᏴᏫ ᏙᏛᎾᎴᏂ ᏙᏛᎾᏓᏡᏔᏂ, ᎠᎴ ᎠᏰᎵ ᏕᎪᏢᏩᏗᏒ ᏙᏛᎾᏓᏡᏔᏂ; ᎠᎴ ᎦᏙᎯ ᏓᎵᏖᎸᏂᏙᎮᏍᏗ, ᎠᎴ ᏓᎪᏄᎶᏏᏙᎮᏍᏗ ᎠᎴ ᎤᏕᏯᏙᏗ ᏂᎦᎵᏍᏔᏂᏙᎮᏍᏗ; ᎯᎠ ᎾᏍᎩ ᎠᏓᎴᏂᏍᎬ ᎠᎩᎵᏯ.
Taifa moja litapigana na taifa lingine; utawala mmoja utapigana na utawala mwingine; kila mahali kutakuwa na mitetemeko ya ardhi na njaa. Mambo haya ni kama tu maumivu ya kwanza ya kujifungua mtoto.
9 ᎠᏗᎾ ᎢᏤᏯᏔᎮᏍᏗ; ᏓᏂᎳᏫᎥᏰᏃ ᏕᎨᏥᏲᏍᎨᏍᏗ; ᏧᏂᏔᏫᎢᏍᏗᏱᏃ ᏕᏥᎵᎥᏂᎮᏍᏗ; ᎠᎴ ᏄᏂᎬᏫᏳᏌᏕᎩ ᎠᎴ ᎤᏂᎬᏫᏳᎯ ᎠᏂᏅ ᏤᏣᏖᏃᎯᏍᏗ ᎨᏎᏍᏗ ᎠᏴ ᎨᏒ ᏅᏗᎦᎵᏍᏙᏗᏍᎨᏍᏗ, ᎾᏍᎩ ᎪᎯᏳᏗᏍᎩ ᏧᏂᎦᏘᎴᎩ.
“Lakini ninyi jihadharini. Maana watu watawapelekeni mahakamani, na kuwapigeni katika masunagogi. Mtapelekwa mbele ya watawala na wafalme kwa sababu yangu ili mpate kunishuhudia kwao.
10 ᎣᏍᏛᏃ ᎧᏃᎮᏛ ᎢᎬᏱ ᏂᎬᎾᏛ ᏧᏁᏩᏗᏒ ᏴᏫ ᎠᎵᏥᏙᏗ ᎨᏎᏍᏗ.
Lakini lazima kwanza Habari Njema ihubiriwe kwa mataifa yote.
11 ᎠᎴ ᎿᎭᏉ ᏕᏣᏘᏁᎨᏍᏗ, ᎠᎴ ᏕᏥᏲᏍᎨᏍᏗ, ᏞᏍᏗ ᎢᎬᏱ ᎦᏰᎯ ᏱᏤᎵᎯᏍᎨᏍᏗ ᎢᏥᏪᏍᏗᏱ ᎢᏥᏁᎢᏍᏗᏱ, ᎠᎴ ᏞᏍᏗ ᎢᎬᏱ ᎦᏰᎯ ᏱᏣᏓᏅᏖᏍᎨᏍᏗ; ᏄᏍᏛᏍᎩᏂ ᏫᎯᏳ ᎨᏒ ᎡᏥᏁᎸ ᎾᏍᎩ ᎢᏥᏁᎨᏍᏗ; ᎥᏝᏰᏃ ᏂᎯ ᏱᏣᏁᎪᎢ, ᎦᎸᏉᏗᏳᏍᎩᏂ ᎠᏓᏅᏙ.
Nao watakapowatieni nguvuni na kuwapeleka mahakamani, msiwe na wasiwasi juu ya yale mtakayosema; saa ile itakapofika, semeni chochote mtakachopewa, maana si ninyi mtakaosema, bali Roho Mtakatifu.
12 ᎠᎾᎵᏅᏟᏃ ᏚᏲᏍᎨᏍᏗ ᎠᎾᎵᏅᏟ ᎤᏲᎱᎯᎯᏍᏗᏱ; ᎠᏍᎦᏯᏃ ᎤᏪᏥ ᏚᏲᏍᎨᏍᏗ; ᎠᎴ ᏗᎨᎦᏅᎩ ᏓᎾᎴᎲᏍᎨᏍᏗ ᏧᏂᎦᏴᎵᎨ ᏓᎾᏡᏗᏍᎨᏍᏗ, ᎠᎴ ᎾᏍᎩ ᎾᏅᏂᏏᏍᎨᏍᏗ ᏕᎨᏥᎢᎮᏍᏗ.
Ndugu atamsaliti ndugu yake auawe; baba atamsaliti mwanae; watoto watawashambulia wazazi wao na kuwaua.
13 ᎠᎴ ᏂᎦᏗᏳ ᏴᏫ ᎨᏥᏍᎦᎩ ᎨᏎᏍᏗ ᎠᏴ ᏧᏆᏙᎥ ᏅᏗᎦᎵᏍᏙᏗᏍᎨᏍᏗ; ᎩᎶᏍᎩᏂ ᎬᎵᏍᏆᏗᏍᎩ ᏗᎧᎿᎭᏩᏕᎩ, ᎾᏍᎩ ᎠᏥᏍᏕᎸᏗ ᎨᏎᏍᏗ.
Watu wote watawachukieni ninyi kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.
14 ᎢᏥᎪᏩᏘᏍᎨᏍᏗᏍᎩᏂ ᎤᏍᎦᎢᏍᏗ ᎠᏛᏗᏍᎩ ᏕᏂᎵ ᎠᏙᎴᎰᏍᎩ ᎤᏁᎢᏍᏔᏅᎯ, ᎦᏙᎨᏍᏗ ᎾᎿᎭᎬᏩᎴᏗ ᏂᎨᏒᎾ, ( ᎩᎶ ᎠᎪᎵᏰᏍᎨᏍᏗ ᎪᎵᎨᏍᏗ, ) ᎿᎭᏉ ᏧᏗᏱ ᎠᏂᏂ ᎠᎾᎵᏒᎭ ᏙᏦᏓᎸ ᏩᏂᎶᏒᎭ.
“Mtakapoona Chukizo Haribifu limesimama mahali ambapo si pake, (msomaji na atambue maana yake!) Hapo watu walioko Yudea wakimbilie milimani.
15 ᎠᎴ ᎩᎶ ᎦᏌᎾᎵ ᎤᎩᎴᏍᏗ, ᏞᏍᏗ ᏴᏗᏠᎠᏍᎨᏍᏗ ᎠᏓᏁᎸ ᏫᏯᏴᎯᎮᏍᏗ, ᎠᎴ ᏞᏍᏗ ᎾᎿᎭᏫᏯᏴᎯᎮᏍᏗ ᏭᎩᏍᏗᏱ ᎪᎱᏍᏗ ᎤᎿᎭᎥ ᎦᏁᎸᎢ.
Mtu aliye juu ya paa la nyumba asishuke kuingia nyumbani mwake kuchukua kitu.
16 ᎠᎴ ᎩᎶ ᏠᎨᏏ ᎡᏙᎯ ᏞᏍᏗ ᏴᏗᎤᏨᏎᏍᏗ ᎤᏄᏬ ᏳᏁᏐᎴᏍᏗ.
Aliye shambani asirudi nyuma kuchukua vazi lake.
17 ᎠᎴ ᎤᏲᎢᏳ ᎢᏳᎾᎵᏍᏓᏁᏗ ᏗᏂᏁᎵᏛ, ᎠᎴ ᏧᏂᏍᏓᎢ ᎾᎯᏳ ᎨᏎᏍᏗ.
Ole wao waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!
18 ᎠᎴ ᎢᏣᏓᏙᎵᏍᏗᏍᎨᏍᏗ ᎢᏥᏔᏲᎯᎮᏍᏗ ᎪᎳ ᎢᏣᎵᏍᏗᏱ ᏂᎨᏒᎾ ᎢᏳᎵᏍᏙᏗᏱ.
Ombeni ili mambo hayo yasitukie nyakati za baridi.
19 ᎾᎯᏳᏰᏃ ᎨᏎᏍᏗ ᎠᎩᎵᏯ ᎡᎮᏍᏗ, ᎾᏍᎩ ᎪᏢᏅᎢ ᎾᏍᎩ ᎤᏁᎳᏅᎯ ᏧᏬᏢᏁ ᏅᏓᎬᏩᏓᎴᏅᏛ ᎪᎯ ᎢᏯᏍᏗ ᎥᏝ ᎾᏍᎩ ᎢᏳᏍᏗ ᏳᏕᏃᎢ, ᎥᏝ ᎠᎴ ᎤᏕᏗ ᏱᎨᏎᏍᏗ.
Maana wakati huo kutakuwa na dhiki ambayo haijatokea tangu Mungu alipoumba ulimwengu mpaka leo, wala haitatokea tena.
20 ᎠᎴ ᎤᎬᏫᏳᎯ ᏂᏚᎪᎳᏛᎾ ᏱᎨᏎ ᎾᎯᏳ ᎢᎦ, ᎥᏝ ᎤᏇᏓᎵ ᏱᎦᏰᏥᏍᏕᎸᎮᎢ; ᎨᎦᏑᏰᏛᏍᎩᏂ ᏅᏗᎦᎵᏍᏙᏗᎭ, ᎾᏍᎩ ᏧᏑᏰᏛ ᎨᏒᎢ, ᎾᏍᎩ ᏚᎪᎳᏛ ᎾᎯᏳ ᎢᎦ.
Kama Bwana asingepunguza siku hizo, hakuna binadamu ambaye angeokolewa. Lakini kwa ajili ya wateule wake, Bwana amezipunguza siku hizo.
21 ᎿᎭᏉᏃ ᎢᏳ ᎩᎶ ᎯᎠ ᏂᏥᏪᏎᎸᎭ, ᎬᏂᏳᏉ ᎠᏂ ᎦᎶᏁᏛ; ᎠᎴ ᎬᏂᏳᏉ ᎾᎿᎭᏂ; ᏞᏍᏗ ᎢᏦᎢᏳᏅᎩ;
“Basi mtu akiwaambieni, Tazama, Kristo yupo hapa! au Yupo pale! msimsadiki.
22 ᎦᎶᏁᏛᏰᏃ ᎤᎾᏤᎸᎯ ᎠᎴ ᎠᎾᏙᎴᎰᏍᎩ ᎤᎾᏤᎸᎯ ᏛᏂᎾᏄᎪᏥ, ᎠᎴ ᎠᏂᎾᏄᎪᏫᏍᎨᏍᏗ ᎤᏰᎸᏛ ᎠᎴ ᎤᏍᏆᏂᎪᏗ, ᎾᏍᎩ ᏧᏂᎶᏄᎮᏗᏱ, ᎢᏳᏃ ᏰᎵ ᏱᎩ, ᎾᏍᏉ ᎨᎦᏑᏰᏛ.
Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo, watafanya ishara na maajabu, ili kuwapotosha wateule wa Mungu, kama ikiwezekana.
23 ᏂᎯᏍᎩᏂ ᎢᏤᏯᏔᎮᏍᏗ; ᎬᏂᏳᏉ ᏂᎦᏛ ᏂᏨᏃᏁᎸ.
Lakini ninyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea.
24 ᎾᎯᏳᏍᎩᏂ ᎨᏎᏍᏗ, ᎤᎶᏐᏁᏍᏗ ᎾᏍᎩ ᎠᎩᎵᏯ, ᏅᏙ ᎢᎦ ᎡᎯ ᏛᎵᏏᎲᏏ, ᎠᎴ ᏅᏙ ᏒᏃᏱ ᎡᎯ ᎥᏝ ᎢᎦ ᏳᏖᏍᏕᏗ;
“Basi, siku hizo baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza na mwezi hautaangaza.
25 ᎠᎴ ᏃᏈᏏ ᎠᏂᎧᎸ ᎦᎸᎶᎢ ᎠᏂᏅᎪᎠᏍᎨᏍᏗ, ᎠᎴ ᎤᏂᏣᏖ ᎦᎸᎶ ᏣᏂᎧᎳ ᏛᎾᎵᏖᎸᏂ.
Nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu za mbingu zitatikiswa.
26 ᎿᎭᏉᏃ ᏛᏂᎪᎯ ᏴᏫ ᎤᏪᏥ ᏣᎢᏎᏍᏗ ᎤᎶᎩᎸᎢ, ᎤᏄᏬᏍᏕᏍᏗ ᎤᏣᏘ ᎤᎵᏂᎩᏗᏳ ᎨᏒ ᎠᎴ ᎦᎸᏉᏗᏳ ᎨᏒᎢ.
Hapo watamwona Mwana wa Mtu akija katika mawingu kwa nguvu nyingi na utukufu.
27 ᎿᎭᏉᏃ ᏙᏓᎦᏅᏏ ᏧᏤᎵ ᏗᏂᎧᎿᎭᏩᏗᏙᎯ, ᎠᎴ ᏙᏓᎦᏟᏌᏂ ᎨᎦᏑᏰᏛ ᏧᏤᎵᎦ ᏫᏙᏛᏯᏅᎯ ᏅᎩ ᏂᏙᏗᎦᎶᏍᎬ ᎤᏃᎴ, ᎡᎶᎯ ᏭᎵᏍᏘᏂᎸ ᏅᏓᏳᏓᎴᏅᏛ ᎦᎸᎶᏃ ᏭᎵᏍᏘᏂᎸ ᏫᎦᎷᎩ.
Kisha atawatuma malaika wake; atawakusanya wateule wake kutoka pande zote nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
28 ᎢᏣᏕᎶᏆᏃ ᏒᎦᏔ-ᎢᏳᏍᏗ ᏡᎬ ᏓᏟᎶᏍᏛᎢ; ᎤᏩᏂᎦᎸ ᎿᎭᏉ ᎤᏓᎨ ᏂᎦᎵᏍᏓ, ᎠᎴ ᏥᎦᎵᏍᏚᎲᏍᎪᎢ, ᎢᏥᎦᏔᎰ ᎪᎩ ᎾᎥᏂᏳ ᎨᏒᎢ;
“Kwa mtini jifunzeni mfano huu: Mara tu matawi yake yanapoanza kuwa laini na kuchanua majani, mnajua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
29 ᎾᏍᎩᏯ ᎾᏍᏉ ᏂᎯ, ᎿᎭᏉ ᎢᏥᎪᏩᏘᏍᎨᏍᏗ ᎯᎠ ᎾᏍᎩ ᏂᎦᎵᏍᏔᏂᏙᎲᎢ, ᎢᏥᎦᏔᎮᏍᏗ ᎾᎥᏂᏳ ᎨᏒᎢ, ᎦᎶᎯᏍᏗᏱᏉ ᎨᏒᎢ.
Hali kadhalika nanyi mtakapoona mambo hayo yakitendeka, jueni kwamba Mwana wa Mtu yuko karibu sana.
30 ᎤᏙᎯᏳᎯᏯ ᎯᎠ ᏂᏨᏪᏎᎮ, ᎯᎠ ᎾᏍᎩ ᎪᎯ ᏣᏁᎭ ᎥᏝ ᏴᏛᏂᎶᏐᏂ ᎬᏂ ᎯᎠ ᎾᏍᎩ ᏂᎦᏗᏳ ᏂᎦᎵᏍᏔᏅᎭ.
Nawaambieni kweli, kizazi hiki hakitapita kabla ya mambo hayo yote kutukia.
31 ᎦᎸᎶ ᎠᎴ ᎡᎶᎯ ᏛᏂᎶᏐᏂ; ᎠᏴᏍᎩᏂ ᎠᎩᏁᏨ ᎥᏝ ᏴᏓᎦᎶᏐᏂ.
Mbingu na dunia zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
32 ᎾᎯᏳᏍᎩᏂ ᎢᎦ ᎨᏒ ᎠᎴ ᎢᏳ ᎧᎳᏩᏗᏒ ᎥᏝ ᎩᎶ ᏯᎦᏔᎭ, ᎥᏝ ᎾᏍᏉ ᏗᏂᎧᎿᎭᏩᏗᏙᎯ ᎦᎸᎳᏗ ᎠᏁᎯ, Ꮭ ᎾᏉᏃ ᎤᏪᏥ, ᎠᎦᏴᎵᎨᏍᎩᏂ ᎤᏩᏒ.
“Lakini hakuna mtu ajuaye siku au saa hiyo itakuja lini; wala malaika wa mbinguni, wala Mwana; Baba peke yake ndiye ajuaye.
33 ᎢᏤᏯᏔᎮᏍᏗ, ᎢᏥᏯᏫᏍᎨᏍᏗ ᎠᎴ ᎢᏣᏓᏙᎵᏍᏗᏍᎨᏍᏗ; ᎥᏝᏰᏃ ᏱᏥᎦᏔᎭ ᎢᏳ ᎨᏒᎢ.
Muwe waangalifu na kesheni, maana hamjui wakati huo utafika lini.
34 [ ᏴᏫᏰᏃ ᎤᏪᏥ ] ᎾᏍᎩᏯᏉ ᎠᏍᎦᏯ ᏣᏂᎩᏍᎪ ᎢᎸᎯᏢ ᏤᎪᎢ, ᎾᏍᎩ ᏥᎬᏕᎪ ᎦᏁᎸᎢ, ᎠᎴ ᎠᏂᎦᏘᏯ ᏥᏂᏕᎬᏁᎰ ᏧᏅᏏᏓᏍᏗ, ᎠᎴ ᎠᏂᏏᏴᏫᎭ ᏧᏂ ᎸᏫᏍᏓᏁᏗ ᏥᏓᏁᎰᎢ, ᎠᎴ ᎦᎶᎯᏍᏗᏱ ᎠᎦᏘᏯ ᏥᎧᏁᏤᎰ ᎤᏯᏫᏗᏱ.
Itakuwa kama mtu anayeondoka nyumbani kwenda safari akiwaachia watumishi wake madaraka, kila mmoja na kazi yake; akamwambia mlinzi wa mlango awe macho.
35 ᎾᏍᎩ ᎢᏳᏍᏗ ᎢᏥᏯᏫᏍᎨᏍᏗ; ᎥᏝᏰᏃ ᏱᏥᎦᏔᎭ ᎢᏳᏉ ᎤᎷᎯᏍᏗᏱ ᎦᏁᎳ, ᎤᏒᎢ, ᎠᎴ ᏒᏃᏱ ᎠᏰᎵ, ᎠᎴ ᏣᏔᎦ ᎠᏂᏴᎬᎢ, ᎠᎴ ᏑᎾᎴᎢ;
Kesheni, basi, kwa maana hamjui mwenye nyumba atarudi lini; huenda ikawa jioni, usiku wa manane, alfajiri au asubuhi.
36 ᏱᎦᎷᎩᏰᏃ ᏯᏰᎶᎢᏍᏓ, ᏴᏥᏩᏛᏓ ᎢᏥᎵᎾᎥᎢ.
Kesheni ili akija ghafla asije akawakuta mmelala.
37 ᎾᏍᎩᏃ ᎯᎠ ᏂᎯ ᏥᏂᏨᏪᏎᎭ, ᎾᏍᎩ ᏂᎦᏛᏉ ᏂᎦᏥᏪᏎᎭ-ᎢᏥᏯᏫᏍᎨᏍᏗ.
Ninayowaambieni ninyi, nawaambia wote: Kesheni!”

< ᎣᏍᏛ ᎧᏃᎮᏛ ᎹᎦ ᎤᏬᏪᎳᏅᎯ 13 >