< San Mateo 6 >

1 ADAJE ya chamiyo fumatitinas y limosnanmiyo gui menan y taotao sija, para infanlinie; sa yaguin ti taegüenao, taya premionmiyo gui tatanmiyo ni gaegue gui langet.
“Jihadharini msije mkafanya matendo yenu mema mbele ya watu kusudi mwonekane nao. La sivyo, Baba yenu aliye mbinguni hatawapeni tuzo.
2 Yaguin unfatitinas y limosnamo, chamo na catitiye trompeta gui menamo taegüije y jafatitinas y hipocrita sija gui sinagoga, yan y plasa para uguaja minalagñija nu y taotao sija. Magajet jusangane jamyo na esta guaja premioñija.
“Basi, unapomsaidia maskini, usijitangaze. Usifanye kama wanafiki wafanyavyo katika masunagogi na njiani ili watu wawasifu. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
3 Lao jago, yaguin unfatitinas y limosnamo, chamo natutungo y canaemo acagüe jafa checho y canaemo agapa.
Lakini wewe unapomsaidia maskini, fanya hivyo kwamba hata rafiki yako asijue ufanyalo.
4 Para ugaegue y limosnamo gui secreto, sa y tatamo ni jalilie gui secreto, güiya umapase jao gui publico.
Toa msaada wako kwa siri, na Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
5 Ya yaguin manaetaejao, munga taegüije y hipocrita, sa sija yanñija manmanaetae gui sinagoga yan y esquinan chalan manotojgue para ufanmalie nu y taotao sija. Magajet na esta guaja premioñija.
“Mnaposali, msifanye kama wanafiki. Wao hupenda kusimama na kusali katika masunagogi na katika pembe za njia ili watu wawaone. Kweli nawaambieni, hao wamekwisha pata tuzo lao.
6 Lao jago, yaguin manaetaejao, jalom gui aposentomo, ya juchum y pettamo, ya taetaye y tatamo ni y gaegue gui secreto; sa y tatamo ni y jalilie gui secreto, güiya umapase jao gui publico.
Lakini wewe unaposali, ingia chumbani mwako, funga mlango, kisha umwombe Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika, atakutuza.
7 Yan manaetaejao chamo sumasangan un sinangan megae na biaje na taebale, taegüije y Gentiles; jinasoñija na ufanmajungog pot y megae sinanganñija.
“Mnaposali, msipayuke maneno kama watu wasiomjua Mungu. Wao hudhani kwamba Mungu atawasikiliza ati kwa sababu ya maneno mengi.
8 Chamiyo fumatitinas taegüije iya sija; sa y tatanmiyo jatungoja jafa innesesita antes qui ingagao güe.
Msiwe kama wao. Baba yenu anajua mnayoyahitaji hata kabla ya kumwomba.
9 Lao an manmanaetae jamyo taegüine: Tatanmame na gaegue jao gui langet: umatuna y naanmo.
Basi, hivi ndivyo mnavyopaswa kusali: Baba yetu uliye mbinguni: Jina lako litukuzwe.
10 Umamaela y raenomo, umafatinas y minalagomo jaftaemano gui langet taegüijija gui tano;
Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.
11 Naejam pago nu y cada jaane na agonmame;
Utupe leo chakula chetu tunachohitaji.
12 Ya asiijam nu y dibenmame, taegüije yan inasisie y dumidibejam sija;
Utusamehe makosa yetu, kama nasi tunavyowasamehe waliotukosea.
13 Ya chamojam pumópolo na infanbasnag gui tentasion, lao nafanlibrejam nu y taelaye; sa iyomo y raeno, yan y ninasiña, yan y minalag para taejinecog na jaane; Amen.
Usitutie katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. is Baadhi ya makala za zamani zina; Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.
14 Sa yaguin inasie y umisagüe jamyo: maninasiija locue jamyo as tatanmiyo ni gaegue gui langet.
“Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi pia.
15 Lao yaguin ti unasie ayo sija y umisagüe jamyo, ti infaninasie locue ni tatanmiyo nu y isaomiyo.
Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu.
16 Yaguin umayuyunatjao, munga taegüije y hipocrita nu y triste na mata, jaago y matañija, para ufanmatungo ni taotao sija na manayunat. Magajet jusangane jamyo, na esta guaja premioñija.
“Mnapofunga, msiwe na huzuni kama wanafiki. Wao hukunja nyuso zao wapate kuonekana na watu kuwa wanafunga. Nawaambieni hakika, hao wamekwisha pata tuzo lao.
17 Lao jago, yaguin umayunat jao, palalae y ilumo, ya unfagase y matamo;
Wewe lakini unapofunga, paka kichwa chako mafuta, nawa uso wako,
18 Para munga malilie nu y taotao sija na umayuyunat jao, lao si tatamoja ni y gaegue gui secreto; ya si tatamo, ni jalilie gui secreto, güiya uninapase gui publico.
ili mtu yeyote asijue kwamba unafunga, ila ujulikane tu kwa Baba yako asiyeonekana. Naye Baba yako aonaye yaliyofichika atakutuza.
19 Chamiyo fannanaetnon güinaja para jamyo gui tano, mano nae y poliya yan y lamas uyinamag, yan y saque sija uyulang yan uchule;
“Msijiwekee hazina hapa duniani ambako nondo na kutu huharibu, na wezi huingia na kuiba.
20 Lao fannaetnon güinaja para jamyo gui langet, mano nae ni y poliya ni y lamas ti uyinamag, ya ni y saque sija ti uyulang yan ti uchule.
Jiwekeeni hazina mbinguni ambako nondo na kutu hawawezi kuiharibu, wala wezi hawaingii wakaiba.
21 Sa manoja nae gaegue y güinajanmiyo, ayoja nae gaegue locue y corasonmiyo.
Maana pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
22 Y candet y tataotao y atadog; yaguin y gasgas atadogmo, todo y tataotaomo ubula y manana.
“Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni zima, mwili wako wote utakuwa katika mwanga.
23 Lao yaguin y taelaye na atadogmo, todo y tataotaomo jomjom, Sa yaguin y manana ni y gaegue guiya jago jomjom, jafa na gosdangculo na jinemjom!
Lakini ikiwa jicho lako ni bovu, mwili wako wote utakuwa katika giza. Basi, ikiwa mwanga ulioko ndani yako ni giza, basi, hilo ni giza la kutisha mno.
24 Taya ni uno siña sumetbe dos amo; sa jachatlie y uno, ya jaguflie y otro; pat jadalalag y uno ya jadespresia y otro. Ti siña jamyo insetbe si Yuus yan y güinaja.
“Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili. Maana atamchukia mmoja na kumpenda huyo wa pili; au ataambatana na mmoja na kumdharau huyo mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali pamoja.
25 Enao mina jusangane jamyo: Chamiyo fanmanjajaso pot y jaaninmiyo; jafa para incano, pat jafa para inguimen; ni pot para innaminagago y tataotaomiyo. Ada ti bale mas y linâlâmo qui y nengcano, yan y tataotaomo qui y magago?
“Ndiyo maana nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula na kinywaji mnavyohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu. Je, maisha ni chakula tu au zaidi? Na mwili, je, si zaidi ya mavazi?
26 Atanja y pajaro gui langet; ti manmanananon, ni ti manmangongoco, ni ti manmanrecocoje jalom gui camalin; sa si tatamoja gui langet munafañochocho. Ada ti mangaebalotña jamyo qui sija?
Waangalieni ndege wa mwituni: hawapandi, hawavuni, wala hawana ghala yoyoye. Hata hivyo, Baba yenu wa mbinguni huwalisha. Je, ninyi si wa thamani kuliko hao?
27 Ya jaye guiya jamyo, yaguin manjaso, siña jataluye y linecaña un codo?
Ni nani miongoni mwenu kwa kuwa na wasiwasi sana anaweza kuuongeza muda wa maisha yake?
28 Ya jafa jamyo na manmanjajaso pot magago? Jasoja y lirio sija gui fangualuan, jaftaemano manlâlâñiñija; ti manmachochocho ya ti manmajijila.
“Na kuhusu mavazi, ya nini kuwa na wasiwasi? Tazameni maua ya porini jinsi yanavyostawi. Hayafanyi kazi wala hayasokoti.
29 Lao jusangane jamyo, na si Salomon yan todo y minalagña, ti minagago parejo yan uno güine sija.
Lakini nawaambieni, hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
30 Yanguin si Yuus janaminagago y chaguan gui fangualuan; sa pago gaegue, ya agupa machule ya mapolo gui jetno, ada ti mas jamyo inninaminagago, taotao jamyo na didide jinengguenmiyo?
Ikiwa basi Mungu hulivika hivyo jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatafanya zaidi kwenu ninyi? Enyi watu wenye imani haba!
31 Enao mina, chamiyo jumajaso umalog: Jafajit tacano, pat jafajit taguimen, pat jafajit magaguta?
“Basi, msiwe na wasiwasi: Tutakula nini, tutakunywa nini, tutavaa nini!
32 Sa todo este sija na güinaja, jaaliligao y Gentiles; ya y tatanmiyo gui langet jatungoja na innesesita todo este sija na güinaja.
Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote.
33 Lao aligao fenena y raenon Yuus, yan y tininasña; ya despues todo este sija na güinaja infanmataluye.
Bali, zingatieni kwanza Ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo mengine yote mtapewa kwa ziada.
34 Chamiyo jumajaso y para agupa, sa y para agupa güiyaja güe ujaso. Basta para y cada y jaane y inalulaye.
Basi, msiwe na wasiwasi juu ya kesho; kesho inayo yake. Matatizo ya siku moja yanawatosheni kwa siku hiyo.

< San Mateo 6 >