< San Lucas 1 >

1 POT y guaja megae y umapolo y canaeñija para ufannaregla y cuentos nu y ayo na güinaja na esta guefmaasegura gui entalo jame,
Wengi wamejitahidi kuweka katika mpangilio simulizi kuhusu masuala ambayo yametimizwa kati yetu,
2 Jaftaemanoja ninaejam ni guine y tutujoña y testigojam ni y malie, nu y yan y ministrojam y sinangan;
kama walivyotupatia sisi, ambao tangu mwanzo ni mashahidi wa macho na watumishi wa ujumbe.
3 Y jinasoco mauleg locue nu guajo, sa juguefegaga sinengcabales todo y güinaja guine y tutujonña, na jutuguie jao pot y inaregla, jago guesmagas na Teofilo;
Hivyo nami pia, baada ya kuchuguza kwa uangalifu chanzo cha mambo haya yote tokea mwanzo - nimeona ni vema kwangu pia kukuandikia katika mpangilio wake - mheshimiwa sana Theofilo.
4 Para untungo sija y magajet ayosija mano nae unresibe y finanagüe.
Ili kwamba uweze kujua ukweli wa mambo uliyofundishwa.
5 Guaja gui jaanin Herodes, ray guiya Judea, un pale, naanña si Sacharias, y clasen Abias; y asaguaña guinin sija jagan Aaron ya y naaña si Elisabet.
Katika siku za Herode, mfalme wa Yudea, palikuwa na kuhani fulani aliyeitwa Zekaria, wa ukoo wa Abiya. Mke wake alitoka kwa binti za Haruni, na jina lake aliitwa Elizabeti.
6 Este na dos mauleg gui sanmenan Yuus, jajananao gui todo y lay yan y tinago Señot, ti lalatdiyon.
Wote walikuwa wenye haki mbele za Mungu; walitembea bila lawama katika amri zote na maagizo ya Bwana.
7 Ya taya patgonñija; sa si Elisabet tifáfañago; yan y dos megae jaaniñija.
Lakini hawakuwa na mtoto, kwasababu Elizabethi alikuwa tasa, na kwa wakati huu wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Ya jumuyong, anae mañeñetbe si Sacharias, gui ofisio y pale gui menan Yuus, gui chechon y clasiña,
Sasa ilitokea kwamba Zakaria alikuwa katika uwepo wa Mungu, akiendelea na wajibu wa kikuhani katika utaratibu wa zamu yake.
9 Jaftaemanoja y costumbren y ofisio y pale, y chechoña na jumalom gui guimayuus ya jasonggue y paopao.
Kulingana na desturi ya kuchagua ni kuhani yupi atakayehudumu, alikuwa amechaguliwa kwa kura kuingia katika hekalu la Bwana na hivyo angefukiza uvumba.
10 Ya todo y linajyan taotao mangaegue gui sanjiyong manmananaetae gui oran paopao.
Kundi lote la watu lilikuwa likiomba nje wakati wa kufukizwa kwa ufumba.
11 Ya mato guiya güiya y angjet y Señot, na gaegue gui agapa y attat y paopao.
Sasa malaika wa Bwana alimtokea na kasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia.
12 Ya inestotba si Sacharias anae jalie, ya mato minaañao gui jiloña.
Zakaria alitishika alipomuona; hofu ikamwangukia.
13 Lao y angjet ilegña nu güiya: Sacharias, chamo maaañao; sa y tinaetaemo este majungog; ya y asaguamo as Elisabet ufañago y patgon laje, ya umafanaan naanña si Juan.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope Zakaria, kwasababu maombi yako yamesikika. Mke wako Elizabeth atakuzalia mwana. Jina lake utamwita Yohana.
14 Ya uguaja jao minagof yan alegria; ya y megae umagof nu y mafañaguña.
Utakuwa na furaha na uchangamfu, na wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
15 Sa udangculo güe gui menan Señot; ya ti uguimen bino ni metgot na guinem ya ubulagüe Espiritu Santo, guinin y tiyan nanaña.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana. Hatakunywa divai au kinywaji kikali, na atakuwa amejazwa na Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.
16 Ya megae gui famaguon Israel, ujabira nu y Señot, Yuusñija.
Na watu wengi wa Israel watageuzwa kwa Bwana Mungu wao.
17 Ya ujanaogüe gui menan y mataña nu y espiritu yan y ninasiñan Elias, para unanalo y corasonñija y mañaena guiya y famaguon, yan y manchátmatago ni y tiningo y manunas; para ufamauleg nu y Señot y taotao, ni y esta fanmauleg para güiya.
Atakwenda mbele za uso wa Bwana katika roho na nguvu ya Eliya. Atafanya hivi ili kurejesha mioyo ya baba kwa watoto, ili kwamba wasiotii wataenenda katika hekima ya wenye haki. Atafanya hivi kuweka tayari kwa Bwana watu ambao wameandaliwa kwa ajili yake.”
18 Ya ilegña si Sacharias nu y angjet: Jaftaemano jutungo este? sa guajo bijoyo ya y asaguajo megae jaaniña.
Zakaria akamwambia malaika, “Nitawezaje kujua hili? Kwasababu mimi ni mzee na mke wangu miaka yake imekuwa mingi sana.”
19 Ya manope y angjet ya ilegña nu güiya: Guajo si Gabriel, na gaegue yo tumotojgue gui menan Yuus; ya guajo esta matago na jucuentusejao, ya junaejao ni este mauleg na sinangan.
Malaika akajibu na kumwambia, “Mimi ni Gabrieli, ambaye husimama mbele za Mungu. Nilitumwa kukwambia, kukuletea habari hii njema.
20 Ya estagüe, na jago udojao ya ti siña uncuentos, asta y jaane nae este macumple estesija; sa y ti unjongue y sinanganjo, ni umacumple y tiempoña.
Na tazama, hutaongea, utakuwa kimya, hutaweza kuongea mpaka siku ile mambo haya yatakapotokea. Hii ni kwasababu ulishindwa kuamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati mwafaka.”
21 Ya y taotao sija manmannanangga as Sacharias, ya ninafanmanman ni y inapmamña gui guimayuus.
Sasa watu walikuwa wakimsubiri Zakaria. Walishangazwa kwamba alikuwa anatumia muda mwingi hekaluni.
22 Ya anae jumuyong, ti siña umadingane sija; ya matungo na manlie un linie gui guimayuus; lao güiya sigue di fumatinas y señatja; ya sumaga udo.
Lakini alipotoka nje, hakuweza kuongea nao. Wakatambua kwamba alikuwa amepata maono alipokuwa hekaluni. Aliendelea kuonesha ishara na alibaki kimya.
23 Ya anae esta munjayan y jaanin y ministroña, jumanao para y guimaña.
Ikatokea kwamba siku za huduma yake zilipokwisha aliondoka kurudi nyumbani kwake.
24 Ya despues di ayo sija na jaane mapotgue y asaguaña as Elisabet, ya janana sinco na meses, ya ilegña:
Baada ya Zakaria kurudi nyumbani kutoka kwenye huduma yake hekaluni, mke wake akawa mjamzito. Naye hakutoka nyumbani mwake kwa muda wa miezi mitano. Akasema,
25 Taemanoja y Señot jafatinas para guajo, este sija na jaane nae jaatanyo para unajanao y mamajlaojo gui entalo taotao sija.
“Hili ndilo amabalo Bwana amefanya kwangu aliponitazama kwa upendeleo ili kuiondoa aibu yangu mbele za watu.”
26 Y mina saes na mes, y angjet Gabriel esta tumago guine as Yuus, para un siuda guiya Galilea, ni y naanña y Nasaret,
Sasa, katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeti, Mungu alimwambia malaika Gabrieli kwenda kwenye mji wa Galilaya uitwao Nazareti,
27 Guiya un bitgen, nobia y un laje naanña si José, familian David; ya y naan y bitgen si Maria.
kwa bikra aliyekuwa ameposwa na mwanaume ambaye jina lake lilikuwa Yusufu. Yeye alikuwa wa ukoo wa Daudi, na jina la bikra huyo lilikuwa Mariamu.
28 Ya jumalom manu nae estaba güe, ya ilegña: Jafa tatatmana jao na guefmaborese jao; y Señot gaegue guiya
Akaja kwake na akasema, “Salaam, wewe uliyepokea neema kuu! Bwana amependezwa nawe.”
29 Lao pot este na sinangan, ninaestotba güe, ya jajajaso na jaftaemano este na sinaluda.
Lakini maneno ya malaika yalimchanganya na hakuelewa kwa nini malaika alisema salaam hii ya ajabu kwake.
30 Entonses y angjet ilegña nu güiya: Maria, chamo maaañao; sa unsoda y finaborese gui menan Yuus.
Malaika akamwambia, “Usiogope, Mariamu, maana umepata neema kutoka kwa Mungu.
31 Ya estagüe, na unmapotgue gui tiyanmo ya unfañago un patgon laje, ya umafanaan y naaaña si Jesus.
Na tazama, utabeba mimba katika tumbo lako na utazaa mwana. Nawe utamwita jina lake 'Yesu.'
32 Ya udangculo güe, ya umafanaan Lajin Gueftaquilo: ya y Señot Yuus ufannae güe y tronon David tataña.
Atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 Ya ugobietna gui guima Jacob siesiempreja; ya y raenoña ugagaegue taejinecog. (aiōn g165)
Atatawala juu ya ukoo wa Yakobo milele na ufalme wake hautakuwa na mwisho. (aiōn g165)
34 Entonses si Maria ilegña ni y angjet: Jafa jumuyong este? sa ti jutungo laje.
Mariamu akamwambia malaika, hili litatokea kwa namna gani, maana sijawahi kulala na mwanaume yeyote?
35 Ya manope y angjet, ya ilegña nu güiya: Y Espiritu Santo umamaela guiya jago, ya y ninasiña y Gueftaquilo jafatinas y anineng gui jilomo; enaomina ayo na Santos na umafañago, umafanaan Lajin Yuus.
Malaika akajibu na akamwambia, “Roho Mtakatifu atakujia juu yako, na nguvu ya Aliye Juu Sana itakuja juu yako. Kwa hiyo, mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu.
36 Ya, estagüe, si Elisabet, parentesmo, locue güiya mapotgue un laje gui inamcoña; ya este y mina saes na mes nu güiya na mafanaan tifáfañago.
Na tazama, ndugu yako Elizabeti anaujauzito wa mwana kwenye umri wake wa uzee. Huu ni mwezi wa sita kwake, ambaye alikuwa anaitwa mgumba.
37 Sa y sinangan Yuus, taya uno na taeninasiña.
Maana hakuna lisilowezekana kwa Mungu.”
38 Entonses si Maria ilegña: Estagüe y tentagon Señot; ufatinas guiya guajo taemanoja y sinanganmo. Ya y angjet mapos guiya güiya.
Mariamu akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana. Acha iwe hivyo kwangu sawa sawa na ujumbe wako.” Kisha malaika akamwacha.
39 Ya ayo na jaane sija, cajulo si Maria ya jumanao gusise para un tano taquilo, guiya un siudan Juda;
Ndipo katika siku hizo Mariamu aliondoka na kwa haraka alikwenda katika nchi ya vilima, kwenye mji katika nchi ya Yudea.
40 Ya jumalom gui guima Sacharias ya jasaluda si Elisabet.
Alikwenda nyumbani mwa Zekaria na akamsalimia Elizabeti.
41 Ya jumuyong taegüije na anae jajungog si Elisabet y sinaludan Maria, y patgon tumayog gui jalom tiyanña; si Elisabet bula Espiritu Santo,
Sasa, ilitokea kwamba Elizabeti aliposikia salamu ya Mariamu, mtoto tumboni mwake akaruka, na Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu.
42 Ya umagang ni dangculo na inagang ya ilegña: Dichosojao gui entalo y famalaoan, ya dichoso y tinegchan tiyanmo.
Akapaza sauti yake na kusema kwa sauti kuu, “umebarikiwa wewe zaidi miongoni mwa wanawake, na mtoto aliyemo tumboni mwako amebarikiwa.
43 Ya guine manu este guiya guajo, na mato guiya guajo y nanan y Señotto.
Na imekuwaje kwangu kwamba, mama wa Bwana wangu ilipasa aje kwangu?
44 Sa estagüe, na anae mato y inagang y sinaludamo gui talangajo, y patgon, gui jalom tiyanjo, tumayog ni minagofña.
Kwa kuwa tazama, iliposikika masikoni mwangu sauti ya kusalimia kwako, mtoto tumboni mwangu akaruka kwa furaha.
45 Ya dichosogüe y jumonggue; sa uguaja y quinimple gui güinaja, ni esta masangane güe ni guinin y Señot.
Na amebarikiwe mwanamke yule ambaye aliamini ya kwamba ungetokea ukamilifu wa mambo yale aliyoambiwa kutoka kwa Bwana.”
46 Entonses ilegña si Maria: Janadangculo y antijo y Señot,
Mariamu akasema, nafsi yangu inamsifu Bwana,
47 Ya y espiritujo ninamagof gui as Yuus y Satbadotto.
na roho yangu imefurahi katika Mungu Mwokozi wangu.
48 Sa jaatan y dinespresiaoña y tentgoña; sa estagüe na desde pago jumafanaan dichosa ni todo y generasion.
Kwa maana ameiangalia hali ya chini ya mtumishi wake wa kike. Tazama, tangu sasa katika vizazi vyote wataniita mbarikiwa.
49 Sa ayo na guaja ninasiña, jafatinas guiya guajo dangculo na güinaja; ya santos y naanña.
Kwa maana yeye aliyemweza amefanya mambo makubwa kwangu, na jina lake ni takatifu.
50 Ya y minaaseña gaegue gui generasion taotao sija, gui jiloñija ni manmaañao nu güiya.
Rehema yake inadumu toka kizazi hata kizazi kwa wale wanao mheshimu yeye.
51 Ya pot y canaeña jafanue minetgot; janafañuja y sobetbio sija gui jinason y corasonñija.
Ameonesha nguvu kwa mkono wake; amewatawanya wale ambao walijivuna juu ya mawazo ya mioyo yao.
52 Ya jayute papa y magas gui tronoñija, ya jajatsa y manumitde.
Amewashusha chini wana wa wafalme toka katika viti vyao vya enzi na kuwainua juu walio na hali ya chini.
53 Ya y manñalang janafanbula ni y minauleg; ya y manmigüinaja janafanjanao yan y tae sinajguan.
Aliwashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 Ya jaayuda si Israel tentagoña, para ufanjaso y miñaase,
Ametoa msaada kwa Israeli mtumishi wake, ili kukumbuka kuonesha rehema
55 (Taemano y jasangane y mañaenata), as Abraham yan y semiyaña para todo y tiempo. (aiōn g165)
(kama alivyosema kwa baba zetu) kwa Abrahamu na uzao wake milele.” (aiōn g165)
56 Si Maria sumaga yan güiya calang tres meses ya despues jumanao asto iyasija.
Mariamu alikaa na Elizabeti yapata miezi mitatu hivi ndipo akarudi nyumbani kwake.
57 Ya si Elisabet jacumple y tiempo nae para ufañago; ya mañago un patgon laje.
Sasa wakati ulikuwa umewadia kwa Elizabeti kujifungua mtoto wake na akajifungua mtoto wa kiume.
58 Ya anae majungog ni tiguangña yan y parientesña, na si Yuus janadangculo y minaaseña guiya güiya; ya manmagof yan güiya.
Jirani zake na ndugu zake walisikia jinsi Bwana alivyoikuza rehema kwake, na wakafurahi pamoja naye.
59 Ya susede na y mina ocho na jaane manmato para umasircunsida y patgon: ya malagoñija umafanaan ni y naan tataña as Sacharias.
Sasa ilitokea siku ya nane kwamnba walikuja kumtahiri mtoto. Ingewapasa kumwita jina lake, “Zekaria,” kwa kuzingatia jina la baba yake,
60 Ya manope y nanaña ya ilegña: Aje, sa umafanaan si Juan.
Lakini mama yake akajibu na kusema, “Hapana; ataitwa Yohana.”
61 Ya ilegñija nu güiya: Taya gui manparientesmo mafanaan nu este na naan.
Wakamwambia, hakuna hata mmoja katika ndugu zako anayeitwa kwa jina hili.”
62 Ya maseñat y tataña, ya mafaesen jafa malagoña umafanaan.
Wakamfanyia ishara baba yake kuashiria yeye alitaka jina aitwe nani.
63 Ya mangagao un diquique na tabla ya jatugue ilegña: Si Juan naanña. Ya todo sija ninafanmanman.
Baba yake akahitaji kibao cha kuandikia, na akaandika, “Jina lake ni Yohana.” Wote wakashangazwa na hili.
64 Ya enseguidas mababa y pachotña, ya mapula y jilaña, ya cumuentos, jabendise si Yuus.
Ghafla mdomo wake ukafunguliwa na ulimi wake ukawa huru. Akaongea na kumsifu Mungu.
65 Ya guaja minaañao gui jiloñija todo y mañasaga gui oriyañija: ya gui todo y tano taquilo guiya Judea, masasangan este sija na sinangan.
Hofu ikawajia wote walioishi karibu nao. Mambo haya yakaenea katika nchi yote ya vilima vya Yudea.
66 Ya todosija y jumujungog jaadaje gui corasonñija ya ilegñija: Jafa jumuyong este na patgon? Sa y canae Yuus gaegue guiya güiya.
Na wote walioyasikia wakayatunza mioyoni mwao, wakisema, “Mtoto huyu kuwa wa namna gani?” Kwasababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 Ya si Sacharias, tataña, bula Espiritu Santo ya japrofetisa, ilegña:
Baba yake Zekaria alijazwa na Roho Mtakatifu na akatoa unabii, akisema,
68 Bendito y Señot, y Yuus y Israel; sa jabisita ya jafatinas y redension, para taotaoña,
“Asifiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa sababu amesaidia na alishughulikia wokovu kwa watu wake.
69 Ya janacajulo para jita un canggelon y satbasion, gui guima y tentagoña as David,
Ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya mtumishi wake Daudi, kutoka miongoi mwa mwa ukoo wa mtumishi wake Daudi,
70 (Taegüijija na jasasangan gui pachot y mañantos na profetaña, ni esta gaegue guinin tutujonña y tano), (aiōn g165)
kama alivyosema kwa kinywa cha manabii wake waliokuweko katika nyakati za kale. (aiōn g165)
71 Satbasion gui y enemiguta yan gui canae todo y chumatliijit;
Atatuoka kutoka kwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.
72 Para umafanue y minaaseña gui mañaenata, ya umajaso y santos na tratoña;
Atafanya hivi kuonesha rehema kwa baba zetu, na kukumbuka agano lake takatifu,
73 Y juramento ni manjula as Abraham ni tatata,
kiapo alichokisema kwa Abrahamu baba yetu.
74 Na güiya unaejit linibreta gui canae y enemiguta ya utasetbe güe sin minaañao,
Aliapa kuthibitha kwamba ingewezekana kumtumikia Yeye bila hofu, baada ya kuokolewa kutoka katika mikononi ya adui zetu.
75 Y sinantos yan y tinunas gui menaña todo y jaanita.
katika utakatifu na haki mbele zake siku zetu zote.
76 Ya, jago, patgon, unmafanaan profetan y Gueftaquilo; sa unjanao gui menan y Señot para unfamauleg y chalanña;
Ndiyo, na wewe mtoto, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana, kwa kuwa utaenenda mbele za uso wa Bwana ili kumwandalia njia, kuwaandaa watu kwa ajili ya ujio wake,
77 Para ufanamatungo y satbasion gui taotaoña ni y maasiin y isaoñija,
kuwafahamisha watu wake kwamba, wataokolewa kwa njia ya kusamehewa dhambi zao.
78 Pot causa y corason y minaaseña y Yuusta, anae y candit ogaan guinin taquilo, jabisitajit,
Hili litatokea kwa sababu ya huruma ya Mungu wetu, sababu ambayo jua tokea juu litatujia,
79 Para junae inina y manmatatachong gui jemjom yan y anineng y finatae; para ufanue y patasta gui chalan y pas.
kuangaza kwao wakaao gizani na katika uvuli wa mauti. Atafanya hivi kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”
80 Ya y patgon lumala ya mumetgot gui espiritu ya sumaga gui desierto asta y jaane anae esta matungo guiya Israel.
Sasa, yule mtoto akakua na kuwa mwenye nguvu rohoni na alikaa nyikani mpaka siku ya kujitokeza kwake kwa Israeli.

< San Lucas 1 >