< Y Checho Y Apostoles Sija 4 >

1 YA anae manguecuentos yan y taotao sija, y magas na mamale yan y magas y templo, yan y Saduseosija, manmato guiya sija,
Wakati Petro na Yohana walipokuwa wakizungumza na watu, makuhani na mlinzi wa hekalu na masadukayo waliwaendea.
2 Ya guesinestotba, sa sija jafananagüe y taotao sija, ya japredidica y quinajulo guinin y manmatae, pot si Jesus.
Walikuwa wameudhika sana kwa sababu Petro na Yohana walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu.
3 Ya manmapolo canae gui jiloñija, ya manmapreso asta y inagpaña, sa estaba esta pupuenge.
Waliwakamata na kuwaweka gerezani hadi asubuhi iliyofuata, kwani tayari ilikuwa jioni.
4 Lao megae sija y jumungog y sinangan majonggue; ya y numeron y taotao sija, buente sinco mit.
Lakini watu wengi waliokuwa wamesikia ujumbe waliamini; na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini walikadiliwa kuwa elfu tano.
5 Ya y inagpaña güije, y magasñija yan y manamco, yan y escriba sija mandaña guiya Jerusalem;
Hata ilipofika asubuhi siku iliyofuata, kwamba wakuu wao, wazee na waandishi, kwa pamoja walikusanyika Yerusalemu.
6 Yan mangaegue si Annas, magas y mamale, yan si Caefas, yan si Juan, yan si Alejandro, yan ayosija parientes y magas mamale,
Anasi kuhani mkuu alikuwepo, na Kayafa, na Yohana, na Iskanda, na wote waliokuwa ni ndugu wa kuhani mkuu.
7 Ya anae munjayan japlanta sija gui talo, jafaesen: Pot jafa na ninasiña, pat jaye na naan na infatinas este?
Walipokuwa wamewaweka Petro na Yohana katikati yao, waliwauliza, “Kwa uwezo gani, au kwa jina gani mmefanya hili?”
8 Ya si Pedro, bula ni y Espiritu Santo, ilegña nu sija: Jamyo ni y magas y taotao, yan y manamco guiya Israel,
Kisha, Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu, akawaambia, “Ninyi wakuu wa watu, na wazee,
9 Yaguin manmachaguejam pago na jaane pot y mauleg finatinas para y malango na taotao, sa jafa muna manajomlo;
kama sisi siku ya leo tunahojiwa kuhusu tendo jema lililofanywa kwa mtu huyu mgonjwa - kwa namna gani mtu huyu alifanywa mzima?
10 Intingo todo jamyo, yan todo y taotao guiya Israel, na pot y naan Jesucristo, y Nasareno, ni y inatane gui quiluus, ni y ninacajulo as Yuus guinin y manmatae; pot güiyaja este na taotao na tumojgue gui menan miyo ya jomlo.
Hebu lijulikane hilo kwenu na kwa watu wote katika Israel, kwamba kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye mlimsulibisha, ambaye Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, ni kwa njia yake kwamba mtu huyu anasimama hapa mbele yenu akiwa mwenye afya.
11 Güiya yuje na acho y innataebale jamyo ni y manmanjatsa, na jumuyong cabesan esquina.
Yesu Kristo ni jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilidharau, lakini ambalo limefanywa kuwa jiwe kuu la pembeni.
12 Ya ni uguaja satbasion gui otro; sa taya otro naan gui papa y langet, manmanae y taotao sija, para usiña utafansatbo.
Hakuna wokovu katika mtu mwingine awaye yote. Kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa watu, ambalo kwa hilo tunaweza kuokolewa.”
13 Ya anae malie y minatatngan Pedro yan Juan, ya jinasonñija na manaetiningo ya manlanga na taotao, ninafanmanman, ya ayonae matungo na guinin mañisija yan si Jesus.
Sasa walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na wakagundua kwamba walikuwa ni watu wakawaida wasio na elimu, walishangaa, wakafahamu kwamba Petro na Yohana wamekuwa pamoja na Yesu.
14 Ya anae malie y taotao ni y manajomlo na mañisija manojgue, taya jafa siña ujasangan contra ayo.
Kwa sababu walimwona yule mtu aliyeponywa amesimama pamoja nao, hawakuwa na kitu cha kusema dhidi ya hili.
15 Lao anae jatago sija na ufanjuyong gui dinaña, manasangane entre sija,
Lakini walipokuwa wamekwisha kuwaamuru mitume waondoke mbele ya mkutano wa baraza, walizungumza wao kwa wao.
16 Ilegñija: Jafa tafatinas ni este sija na taotao? sa magajet na afamao na milagro mafatinas pot sija, ya manmamatungo esta ni todo ayo sija y mañasaga Jerusalem; ya ti siña tapune.
Walisema, tutawafanyaje watu hawa? Ni kweli kwamba muujiza wa ajabu umefanyika kupitia wao unajulikana na kila mmoja anayeishi Yerusalemu; hatuwezi kulikataa hilo.
17 Lao trabia mientras ti chachago matalaña gui entalo y taotao sija; nije taencatga sija, ya chañija fanmañangangane ni este na naan desde pago.
Lakini, ili kwamba jambo hili lisienee miongoni mwa watu, hebu tuwaonye wasinene tena kwa mtu yeyote kwa jina hili.
18 Ya jaagang sija, ya jaencatga na senchañija sumasangan, ni ufanmamanagüe ni y naan Jesus.
Waliwaita Petro na Yohana ndani na kuwaamuru kamwe wasinene wala kufundisha kwa jina la Yesu.
19 Lao si Pedro yan Juan manope ilegñija: Jusga, cao tunas gui menan Yuus na inosgueña jamyo qui si Yuus;
Lakini Petro na Yohana walijibu na kuwaambia, “Kama ni sahihi machoni pa Mungu kuwatii ninyi kuliko Mungu, hukumuni wenyewe.
20 Sa tisiña inpelo na ti insangan y liniimame yan y jiningogmame.
Maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo ambayo tumeyaona na kuyasikia.”
21 Ya anae esta jaencatga sija mas, jasotta, sa taya siña jafa ujasoda para ujacastiga, pot causa y taotaosija; sa todo mumalag si Yuus pot ayo y mafatinas.
Baada ya kuwaonya sana Petro na Yohana, waliwaacha waende. Hawakuweza kupata sababu yoyote ya kuwaadhibu, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsifu Mungu kwa kile kilichokuwa kimetendeka.
22 Sa y taotao ni y anae mafatinas este y milagron y jinelo, mas di cuarenta años inamcoña.
Mtu aliyekuwa amepokea muujiza wa uponyaji alipata kuwa na umri zaidi ya miaka arobaini.
23 Ya anae masotta na ujanao, manjanao para y mangachongñija, ya jasangane todo ni y mansinangane sija ni y magas mamale yan y manamco.
Baada ya kuwaacha huru, Petro na Yohana walikuja kwa watu wao na kuwataarifu yote ambayo makuhani wakuu na wazee walikuwa wamewaambia.
24 Ya anae jajungog sija ayo, jajatsa y inagangñija para as Yuus, ilegñija: O Señot, jago Yuus, ni y fumatinas y langet, yan y tano, yan y tase, yan todo y mangae gui sanjalomñija;
Walipoyasikia, walipaza sauti zao kwa pamoja kwa Mungu na kusema, “Bwana, wewe uliyeumba mbingu na dunia na bahari na kila kitu ndani yake,
25 Ni y pot Espiritu Santo ni y pachot y tentagomo as David ilegmo: Sa jafa y Gentiles na manlalalo, ya y taotao sija manmanjaso ni y taebale na güinaja?
wewe ambaye, kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema, “Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?
26 Y ray sija gui tano manotojgue julo, ya y magalaje sija mandaña contra y Señot, yan contra si Cristoña.
Wafalme wa dunia wamejipanga pamoja, na watawala wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya masihi wake.”
27 Sa magajet na gui este siuda contra y santos na Tentagomo as Jesus, ni y unpalalae; todo si Herodes, yan Poncio Pilato, yan y Gentiles yan y taotao guiya Israel, mandaña,
Ni hakika, wote Herode na Pontio Pilato, pamoja na watu wa mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika kwa pamoja katika mji huu dhidi ya mtumishi wako mtakatifu Yesu, ambaye ulimpaka mafuta.
28 Para ujafatinas jafa y tinancho antes y canaemo, yan y consejumo para ususede.
Walikusanyika kwa pamoja kufanya yote ambayo mkono wako na mapenzi yako yaliyaamuru tangu awali kabla hayajatokea.
29 Ya pago, O Señot, lie y amenasoñija: ya unnae y tentagomo sija, na contodo y minatatnga ujasangan y sinanganmo,
Sasa, Bwana, yaangalie matisho yao, na ukawajaalie watumishi wako kulinena neno lako kwa ujasiri wote. Ili
30 Mientras unjujuto mona y canaemo para umajomlo; ya para y señat yan mannamanman umafatinas pot y naan y santos na Tentagomo as Jesus.
kwamba unaponyosha mkono wako kuponya, ishara na maajabu viweze kutokea kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu.”
31 Ya anae munjayan manmanaetae, y lugat anae mandadaña mayengyong; ya todos manbula ni y Espiritu Santo, ya manmatatnga jasangan y sinangan Yuus.
Walipomaliza kuomba, eneo ambalo walikusanyika kwa pamoja likatikiswa, na wote wakajazwa na Roho Mtakatifu, na walinena neno la Mungu kwa ujasili.
32 Ya y inetnon güije sija ni y manmanjonggue, manunoja na corason yan unoja na ante: ni uno guiya sija ualog iyoña ayo y jasagagaye; lao todo y güinaja manparejo iyonñija.
Idadi kubwa ya wale walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja: na hakuna hata mmoja wao aliyesema kwamba chochote alichomiliki kilikuwa cha kwake mwenyewe; badala yake walikuwa na vitu vyote shirika.
33 Yan dangculo na ninasiña na manmannae y apostoles testimonio ni y quinajulo y Señot Jesus: ya megae na grasia gaegue gui jiloñija todos.
Kwa nguvu kubwa mitume walikuwa wakiutangaza ushuhuda wao kuhusu ufufuo wa Bwana Yesu, na neema kubwa ilikuwa juu yao wote.
34 Ya ni uno guiya sija nesesitao; sa todo ayo sija y mangaeiyo tano pat guma, jabende ya jachule y balen ayo y binendenñija,
Hapakuwa na mtu yeyote miongoni mwao aliyepungukiwa na mahitaji, kwa sababu watu wote waliokuwa na hati za viwanja au nyumba, waliviuza na kuleta pesa ya vitu waliyokuwa wameuza
35 Ya japolo gui adeng y apostoles sija: ya manmapapatte cada taotao jafataemano y janesesita.
na kuviweka chini ya miguu ya mitume. Na mgawanyo ulifanywa kwa kila muumini, kulingana na kila mmoja alivyokuwa na hitaji.
36 Ayonae si José, ni y mafanaan ni y apostoles Barnabé (ni y comoqueilegña, lajin consuelo) ni y Lebita, taotao Chipre,
Yusufu, mlawi, mtu kutoka Kipro, alipewa jina la Barnabasi na mitume (hiyo ikitafasiriwa, ni mwana wa faraja).
37 Guaja tanoña, ya jabende, ya jachule y salape, ya japolo gui adeng apostoles sija.
Akiwa na shamba, aliliuza na akaleta fedha, akaziweka chini ya miguu ya mitume.

< Y Checho Y Apostoles Sija 4 >