< Y Checho Y Apostoles Sija 21 >

1 YA anae susede na manadingojam, manmaudaejam gui batco, ya manmatojam gui tinas na chalan para Coos, ya y inagpaña na jaane manmatojam Rodas, ya desde ayo asta Pátara.
Tulipokwisha agana nao, tulipanda meli tukaenda moja kwa moja mpaka Kosi. Kesho yake tulifika Rodo, na kutoka huko tulikwenda Patara.
2 Ya inseda un batco na jumajanao para Finesia, ya manmaudaejam, ya manjanaojam.
Huko, tulikuta meli iliyokuwa inakwenda Foinike, hivyo tulipanda, tukasafiri.
3 Ya anae intutujon lumie Chipre inpelo gui acagüe, ya manjanaojam asta Siria, ya manmatojam Tiro: sa para umadescatga güije y batco.
Baada ya kufika mahali ambapo tuliweza kuona Kupro, tulipitia upande wake wa kusini tukaelekea Siria. Tulitia nanga katika mji wa Tiro ambapo ile meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake.
4 Ya anae manmañodajam güije disipulo, mañagajam siete na jaane; ya ilegñija as Pablo pot y Espiritu, na chaña jumajanao julo Jerusalem.
Tulikuta waumini huko, tukakaa pamoja nao kwa muda wa juma moja. Waumini hao wakawa waongea kwa nguvu ya Roho, wakamwambia Paulo asiende Yerusalemu.
5 Ya anae inquimple todo esta ayo sija na jaane, manjanaojam ya insigue y jinanaomame, ya manmaosgaejonjam ni y asaguanñija yan y famaguonñija, asta qui manjuyongjam gui siuda: ya mandimojam gui oriyan tase ya manmanayuyutjam.
Lakini muda wetu ulipokwisha tuliondoka. Wote pamoja na wanawake na watoto wao walitusindikiza mpaka nje ya mji. Tulipofika pwani, sote tulipiga magoti tukasali.
6 Ya, anae manadingojam, uno y otro, manmaudaejam gui batco, ya sija manalo guato guiya sija.
Kisha tuliagana; sisi tukapanda meli nao wakarudi makwao.
7 Ya anae inquimple y jinanaomame desde Tiro, manmatojam Tolemaida, ya insaluda y mañelo, ya mañagajam güije yan sija un jaane.
Sisi tuliendelea na safari yetu kutoka Tiro tukafika Tolemai ambapo tuliwasalimu ndugu zetu, tukakaa nao siku moja.
8 Ya y inagpaña, jame ni y mangachong Pablo, manjanaojam, ya manmatojam Sesarea; ya manjalomjam gui guima Felipe y ebangelista ni y uno gui siete, ya mañagajam güije yan güiya.
Kesho yake tuliondoka tukaenda Kaisarea. Huko Kaisarea tulikwenda nyumbani kwa mhubiri Filipo. Yeye alikuwa mmoja wa wale saba waliochaguliwa kule Yerusalemu.
9 Ya ayo na taotao, guaja cuatro jagaña na vitgen na manmanprofetisa.
Alikuwa na binti watatu ambao walikuwa na kipaji cha unabii.
10 Ya mientras mañagajam güije megae na jaane, mato papa guinin Judea un profeta na y naanña Agabo.
Baada ya kukaa huko siku kadhaa, nabii mmoja aitwaye Agabo alifika kutoka Yudea.
11 Ya anae mato guiya jame, jachule y senturon Pablo, ya jagode güe canaeña yan y adengña, ya ilegña: Taegüine ilegña y Espiritu Santo: Taegüineja magodeña y gaeiyo este na senturon, ni y Judios ni mangaegue Jerusalem, ya umaentrega gui canae Gentiles.
Alitujia, akachukua mkanda wa Paulo, akajifunga mikono na miguu, akasema “Roho Mtakatifu asema hivi: Wayahudi kule Yerusalemu watamfunga namna hii mtu mwenye ukanda na kumtia mikononi mwa watu wa mataifa.”
12 Ya anae injingog este sija, parejoja jame yan ayo y mañasaga güije na lugat, matayuyut güe na chaña jumajanao julo Jerusalem.
Tuliposikia hayo, sisi na wale watu wengine waliokuwa hapo tulimsihi Paulo asiende Yerusalemu.
13 Ayonae manope si Pablo ilegña: Jafa na manatanges jamyo, ya inyamag y corasonjo? sa esta listoyo ti para jumagodeja, lao asta jumatae guiya Jerusalem, pot y naan Jesucristo.
Lakini yeye alijibu, “Mnataka kufanya nini? Mnataka kuvunja moyo wangu kwa machozi? Niko tayari siyo tu kutiwa ndani kule Yerusalemu, ila hata kufa kwa ajili ya Bwana Yesu.”
14 Ya anae timalago manamañaña, manbastajam ilegmame: Y minalago y Señot umafatinas.
Tuliposhindwa kumshawishi tulinyamaza, tukasema tu: “Mapenzi ya Bwana yafanyike”
15 Ya despues di ayo sija na jaane, inchile y güinajanmame ya manjanaojam papa Jerusalem.
Baada ya kukaa pale kwa muda, tulifunga mizigo yetu, tukaendelea na safari kwenda Yerusalemu.
16 Ya manjame locue yan palo disipulon Sesarea, ya manmangongone un Mnason iya Chipre, y bijo na disipulo ya infanjame mañaga.
Wengine kati ya wale wafuasi wa Kaisarea walienda pamoja nasi, wakatupeleka nyumbani kwa Mnasoni ambaye tulikuwa tunakwenda kukaa naye kwa muda. Mnasoni alikuwa mwenyeji wa Kupro na alikuwa amekuwa muumini kwa siku nyingi.
17 Ya anae manmatojam Jerusalem, mangosmagof y mañelo jaresibejam.
Tulipofika Yerusalemu, ndugu waumini walitupokea vizuri sana.
18 Ya y inagpaña, manjanaojam yan si Pablo para as Santiago: ya todo y manamco manestaba.
Kesho yake Paulo alikwenda pamoja nasi kumwamkia Yakobo, na wazee wote wa kanisa walikuwako pia.
19 Ya anae munjayan jasaluda sija, jasanganen adumidide ni y finatinas Yuus gui entalo Gentiles pot y chechoña.
Baada ya kuwasalimu, Paulo aliwapa taarifa kamili kuhusu yote Mungu aliyokuwa ametenda kati ya mataifa kwa njia ya utumishi wake.
20 Ya anae jajungog sija, maalaba y Señot, ya ilegñija nu güiya: Unlie chelujo cuantos miles na Judios y manmanjonggue, yan maneggo ni y tinago:
Waliposikia hayo, walimtukuza Mungu. Kisha wakamwambia Paulo, “Ndugu, unaweza kuona kwamba kuna maelfu ya Wayahudi ambao sasa wamekuwa waumini na wote hao wanashika kwa makini Sheria ya Mose.
21 Ya matungo guinin jago, na unfanagüe todo y Judios ni y mangaegue gui Gentiles, na ujafañuja gui as Moises, ilegmo, na munga manmasirconsida y famaguonñija, ni ujadalalag y costumbre.
Wamepata habari zako kwamba umekuwa ukiwafundisha Wayahudi wanaoishi kati ya mataifa mengine kuwa wasiijali Sheria ya Mose, wasiwatahiri watoto wao na kwamba wasizifuate mila za Wayahudi.
22 Ya jafa nae umafatinas? Magajet na ujajungog na mato jao.
Sasa, mambo yatakuwaje? Ni dhahiri kuwa watapata habari kwamba umekwisha wasili hapa.
23 Enao mina fatinas este y insangane jao: Guajajam cuatro na taotao na manmanpromesa;
Basi, fanya kama tunavyokushauri. Tunao hapa watu wanne ambao wameweka nadhiri.
24 Cone sija, ya unnagasgas jao yan sija, ya unfangata pot sija ya ufanmadasae ilunñija; ya todo utiningo na ayo sija y matungo pot jago taya guaja; lao jago locue dalalag jaftaemano y tinago, ya unadaje y lay.
Jiunge nao katika ibada ya kujitakasa, ukalipe na gharama zinazohusika, kisha wanyolewe nywele zao. Hivyo watu wote watatambua kwamba habari zile walizoambiwa juu yako hazina msingi wowote, na kwamba wewe binafsi bado unaishi kufuatana na maagizo ya Sheria za Mose.
25 Ya pot y Gentiles ni y manmanjonggue, esta intigue na innafagpo, na chañija umadadaje ni uno güine; solo ujaadajeja sija güije na güinaja y manmaofrese y idolos, yan y jâgâ, y mamuno, yan y inábale.
Kuhusu wale watu wa mataifa mengine ambao wamekuwa waumini, tumekwisha wapelekea barua tukiwaambia mambo tuliyoamua: wasile chochote kilichotambikiwa miungu ya uongo, wasinywe damu, wasile nyama ya mnyama aliyenyongwa, na wajiepushe na uasherati.”
26 Ayonae si Pablo jacone y taotao sija, ya y inagpaña na jaane janagasgas güe yan sija, jumalom gui templo para usangan y macumplen y jaanen y managasgas, asta qui ufanmaofrese y inefrese cada uno guiya sija.
Basi, kesho yake Paulo aliwachukua wale watu akafanya ibada ya kujitakasa pamoja nao. Kisha akaingia Hekaluni kutoa taarifa kuhusu mwisho wa siku za kujitakasa na kuhusu dhabihu itakayotolewa kwa ajili ya kila mmoja wao.
27 Ya anae esta cana mamagpo y siete na jaane, ni Judios ni y mangaegue Asia, anae malie güe gui templo, janafangalamten todo y taotao contra güiya.
Wakati siku hizo saba zilipokaribia kuisha, Wayahudi waliokuwa wametoka katika mkoa wa Asia walimwona Paulo Hekaluni. Wakachochea hasira kati ya kundi lote la watu, wakamtia nguvuni
28 Ya managang ilegñija: Taotao Israel, fanmanayuda: Estagüe yuje na taotao y jafananagüe todo y taotao manoja guato contra y pueblo, yan y lay, yan este na lugat: yan janafanjalom y Gentiles gui templo, ya janataelaye este na lugat.
wakipiga kelele: “Wananchi wa Israeli, msaada, msaada! Huyu ndiye yule mtu anayewafundisha watu kila mahali mambo yanayopinga watu wa Israeli, yanayopinga Sheria ya Mose na mahali hapa patakatifu. Hata sasa amewaingiza watu wa mataifa mengine Hekaluni na kupatia najisi mahali hapa patakatifu.”
29 (Sa guinin malie güe antes yan si Trófimo, un taotao Efeso, gui siuda, ya jinasoñija na si Pablo cumone jalom gui templo.)
Sababu ya kusema hivyo ni kwamba walikuwa wamemwona Trofimo mwenyeji, wa Efeso, akiwa pamoja na Paulo mjini, wakadhani kwamba Paulo alikuwa amemwingiza Hekaluni.
30 Ya todo manatborotao y siuda, yan todo y taotao manmalago, ya macone si Pablo, ya manajuyong gui templo; ya enseguidas manmajuchom y petta.
Mji wote ulienea ghasia; watu wakaja kutoka pande zote, wakamkamata Paulo, wakamburuta, wakamtoa nje ya Hekalu na papo hapo milango ya Hekalu ikafungwa.
31 Ya anae manjajanao para umapuno si Pablo, mato notisia gui magas y inetnon, na todo iya Jerusalem man atborotao.
Walikuwa tayari kumuua, lakini habari zilimfikia mkuu wa jeshi la Kiroma kuwa Yerusalemu yote ilikuwa imejaa ghasia.
32 Ya enseguidas mangone sendalo sija yan capitan, ya manmalago guato guiya sija; ya anae malie y magas y inetnon yan y sendalo sija, manbasta masaulag si Pablo.
Mara, mkuu wa jeshi akawachukua askari na jemadari, akalikabili lile kundi la watu. Nao walipomwona mkuu wa jeshi na askari, wakaacha kumpiga Paulo.
33 Ayonae y magas y inetnon jumijot, ya quinene güe, ya manago na umagode dos na cadena: ya mamaesen jaye güe, yan jafa finatinasña.
Mkuu wa jeshi alimwendea Paulo, akamtia nguvuni na kuamuru afungwe minyororo miwili. Kisha akauliza, “Ni mtu gani huyu, na amefanya nini?”
34 Ya palo manaagang un inagang, ya y palo, otro inagang, gui entre y linajyan taotao: ya anae ti siña tumungo y magajet pot y atboroto, manago na umacone guato gui castiyo.
Wengine katika lile kundi la watu walikuwa wanapayuka kitu hiki na wengine kitu kingine. Kwa sababu ya ghasia hiyo, mkuu wa jeshi hakufaulu kujua kisa kamili. Hivyo, aliamuru watu wake wampeleke Paulo ndani ya ngome.
35 Ya anae mato gui guaot, sa macocone ni y sendalo sija, pot y finijom y linajyan taotao;
Paulo alipofika kwenye ngazi, askari walilazimika kumbeba kwa sababu ya fujo za watu.
36 Sa manatateja y linajyan taotao, ya manaagangja ilegñija: Fañuja yan guiya.
Kwa maana kundi kubwa la watu walimfuata wakipiga kelele, “Muulie mbali!”
37 Ya anae para umacone si Pablo gui castiyo, ilegña nu y magas inetnon: Siñajit cumuentos? ya ilegña: Untungo Griego?
Walipokuwa wanamwingiza ndani ya ngome, Paulo alimwomba mkuu wa jeshi akisema, “Naweza kukwambia kitu?” Yule mkuu wa jeshi akamjibu, “Je unajua Kigiriki?
38 Ti jago ayo y taotao Egipto, ni y antes di este sija na jaane unfatinas jatsamiento, ya uncone guato gui desierto cuatro mil na taotao ni y manpegno?
Kwani wewe si yule Mmisri ambaye hivi majuzi alianzisha uasi na kuwaongoza majahili elfu nne hadi jangwani?”
39 Lao si Pablo ilegña: Guajo Judioyo, taotao Tarso, siuda Silisia—taotao un siuda ti diquique: ya jutayuyut jao na unpoloyo ya jucuentuse y taotao sija.
Paulo akajibu, “Mimi ni Myahudi, mzaliwa wa Tarso katika Kilikia; mimi ni raia wa mji maarufu. Tafadhali, niruhusu niongee na watu.
40 Ya anae ninae lisensia, tumojgue si Pablo gui guaot, ya jaseñas y taotao sija ni y canaeña. Ya anae manmamatquilo jacuentuse sija ni cuentos Hebrea, ilegña:
Yule mkuu wa jeshi akamruhusu. Hivyo Paulo alisimama juu ya ngazi, akawapungia mkono wale watu na walipokaa kimya, akaanza kuongea nao kwa Kiebrania.

< Y Checho Y Apostoles Sija 21 >