< Y Checho Y Apostoles Sija 13 >

1 YA estaba güije gui ilesia guiya Antioquia, profeta sija yan maestro, sija: Barnabé, yan si Simeon ni y mafanaan Niger, yan si Lucio, taotao Sirene, yan si Manaen, ni y chamapogsae yan Herodes tetrarca, yan si Saulo.
Sasa katika kanisa la Antiokia, palikuwa na baadhi ya manabii na walimu. Walikua Barnaba, Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaeni( ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi wa mkoa), na Sauli.
2 Ya mientras sija sumesetbe y Señot, yan manayuyunat, y Espiritu Santo ilegña: Abatta guiya guajo Barnabé yan Saulo para y checho anae guinin juagange sija.
Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema, “Niteengeeni pembeni Barnaba na Sauli, waifanye kazi niliyo waitia.”
3 Ayonae anae esta manayunat yan manmanayuyut yan japolo y canaeñija gui jilo ayo sija, jatago sija na ufanjanao.
Baada ya Kanisa kufunga, kuomba, na kuweka mikono yao juu ya watu hawa, wakawaacha waende.
4 Ya manmatago sija pot y Espiritu Santo, ya manunog para Seleusia; ya desde ayo mumamaya para Chipre.
Kwa hiyo Barnabas na Sauli walimtii Roho Mtakatifu na walitelemka kuelekea Seleukia; Kutoka huko walisafiri baharini kuelekea kisiwa cha Kipro.
5 Ya anae mangaegue gui Salamina, japredica y sinangan Yuus gui sinagogan y Judiosija: ya mañisijaja locue yan si Juan ni y sumesetbe sija.
Walipokuwa katika mji wa Salami, walilitangaza neno la Mungu katika Masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.
6 Ya anae jajanagüe todo inanaco y isla asta Pafo, jasoda un taotao na cacana, fatso na profeta, Judio, na y naanña si Bar-Jesus:
Walipokwenda katika kisiwa chote mpaka Pafo, walikuta mtu fulani mchawi, Myahudi nabii wa uongo, ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu.
7 Ni y estaba yan y magalajen y tano, si Sergio Paulo, gaetiningo na taotao; ya jaaagang si Barnabé yan Saulo, sa malago na ujungog y sinangan Yuus.
Mchawi huyu alishirikiana na Liwali Sergio Paulus, aliyekuwa mtu mwenye akili. Mtu huyu aliwaalika Barnaba na Sauli, kwa sababu alihitaji kusikia neno la Mungu.
8 Lao manquinentra as Elymas, taotao na cacana (taegüine nae comequilegña y naanña), jaaliligao na unamabira guinin jinenggue y magalaje.
Lakini Elima “yule mchawi” (hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa) aliwapinga; alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani.
9 Ayonae si Saulo ni y naanña locue Pablo, bula ni y Espiritu Santo, inaatanja güe,
Lakini Sauli aliyeitwa Paulo, alikuwa amejazwa na Roho Mtakatikfu, akamkazia macho
10 Ya ilegña: O bula jao todo dinague, yan tinaelaye, jago lajin anite, jago enemigun todo y tininas, ada ti pumapara jao unnataelaye y tinas na chalan y Señot?
na akasema “Ewe mwana wa Ibilisi, umejazwa na aina zote za udanganyifu na udhaifu. Wewe ni adui wa kila aina ya haki. Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?
11 Ya pago estagüiya y canae y Señot gui jilomo, ya unbachet ya ti unlie y atdao pot un tiempo. Ya enseguidas podong gui jiloña y nublado ya jomjom, ya jumanao manaligao jaye uminantiene y canaeña para uinesgaejongüe.
Sasa tazama, mkono wa Bwana upo juu yako, na utakuwa kipofu. Hautaliona Jua kwa muda” mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas; alianza kuzunguka pale akiomba watu wamwongoze kwa kumshika mkono.
12 Ya anae jalie y magalaje jafa y mafatinas, jajonggue ya ninasenmanman ni y finanagüen y Señot.
Baada ya liwali kuona kilichotokea, aliamini, kwa sababu alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.
13 Ya anae si Pablo yan y mangachongña jadingo Pafo, ya mumamaya ya manmato Petga guiya Pamfilia, ya si Juan jumanao guiya sija ya tumalo guato Jerusalem.
Sasa Paulo na rafiki zake walisafiri majini kutoka Pafo na wakafika Perge katika Pamfilia. Lakini Yohana aliwaacha na kurudi Yerusalemu.
14 Lao sija manmalofan inanaco guinin Petga, manmato Antioquia guiya Pisidia; ya manjalom gui sinagoga gui sabado na jaane ya manmatachong.
Paulo na rafiki yake walisafiri kutoka Perge na wakafika Antiokia ya Pisidia. Huko walikwenda katika sinagogi siku ya Sabato na kukaa chini.
15 Ya anae munjayan jataetae y lay yan y profeta sija, y magas y sinagoga ninafamnaagange sija ilegñija: Jamyo mañelo, yaguin guaja jafa na finijo para insangane y taotao sija, sangan.
Baada ya kusoma sheria na manabii, viongozi wa sinagogi aliwatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mnao ujumbe wa kutia moyo watu hapa, semeni”
16 Ayonae si Pablo tumojgue julo ya mañeñas ni y canaeña, ilegña: Taotao Israel, yan jamyo ni y manmaañao as Yuus, ecungog.
Kwa hiyo Paulo alisimama na kuwapungia mkono; alisema, “Wanaume wa Israeli na enyi mnao mtii Mungu, sikilizeni.
17 Y Yuus este na taotao iya Israel, jaayeg y mañaenata, yan jajatsa y taotao sija anae mañasaga taegüije y taotao juyong guiya Egipto, ya ni y taquilo na canaeña jacone sija juyong güije.
Mungu wa hawa watu wa Israeli aliwachagua baba zetu na kuwafanya watu wengi walipokaa katika nchi Misri, na kwa mkono wake kuinuliwa aliwaongoza nje yake.
18 Ya y cuarenta años ni tiempo, jasungon ni y costumbreñija gui jalomtano.
Kwa miaka arobaini aliwavumilia katika jangwa.
19 Ya guinin mujayan jayulang siete na nasion gui tano Cananea, ya japatte y tanoñija guiya sija para y erensiañija nae mañasaga, como cuatro siento y sincuenta años;
Baada ya kuyaharibu mataifa saba katika nchi ya Kaanani, aliwapa watu wetu nchi yao kwa urithi.
20 Ya despues di ayo sija, manninae sija jues sija asta qui mato y profeta Samuel.
Matukio haya yote yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini. Baada ya vitu hivi vyote, Mungu aliwapa waamuzi mpaka Samweli Nabii.
21 Ya despues manmalago ray: ya manninae as Yuus as Saulo lajin Sis, un taotao gui tribon Benjamin para cuarenta años.
Baada ya haya, watu waliomba mfalme, hivyo Mungu aliwapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila la Benjamini, kuwa mfalme kwa miaka arobaini.
22 Yaanae jarechasa si Saulo, janacajulo guiya sija si David para rayñija. Sa si Yuus numae güe locue testimonio, ilegña: Guajo jusoda si David lajin Isai, un taotao na parejoja yan y corasonjo, ya güiya ucumple todo y malagojo.
Kisha baada ya Mungu kumuondoa katika ufalme, alimwinua Daudi kuwa mfalme wao. Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema, 'Nimempata Daudi mwana wa Yese kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu; ambaye atafanya kila kitu nipendacho.'
23 Ya y semiyan este na taotao nae, unacajulo si Yuus guiya Israel y Satbadot Jesus jaftaemanoja y promesa:
Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu Mungu ameiletea Israeli mkombozi, Yesu, kama alivyoahidi kufanya.
24 Ya si Juan finena prumedica, antes di y finatoña, y tinagpangen sinetsot para todo y taotao guiya Israel.
Hili lilianza kutokea, kabla ya Yesu kuja, Yohana kwanza alitangaza ubatizo wa toba kwa watu wote wa Israeli.
25 Ya anae jacumple si Juan y chechoña, ilegña: Jayeyo jinasonmimiyo? Ti guajo güe. Lao estagüe na mamamaela uno gui tateco, na ni y sapatos gui adengña ti dignoyo na jupula.
Naye Yohana alipokuwa akimalizia kazi yake, alisema, 'Mwanifikiri mimi ni nani? mimi si yule. Lakini sikilizeni, ajaye nyuma yangu, sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'
26 Mañelo lalaje, fumaguon y rasan Abraham, yan jayeja guiya jamyo y maañao as Yuus, sa para jamyo na matago y sinangan este na satbasion.
Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu, ni kwa ajili yetu kwamba ujumbe huu wa ukombozi umetumwa.
27 Pot ayo sija y mañasaga Jerusalem, yan y magasñija sa ti matungo si Yuus, ni y sinangan y profeta ni y jatataetaeja cada sabado, anae masentensia güe jacumple sija.
Kwa wale waishio Yerusalemu, na watawala wao, hawakumtambua kwa uhalisia, na wala hawakuutambua ujumbe wa manabii ambao husomwa kila Sabato; kwa hiyo walitimiliza ujumbe wa manabii kwa kumhukumu kifo Yesu.
28 Ya achogja ti jasoda sija jafa na causa guiya güiya na umapuno, lao magagao si Pilatos na umapuno.
Japokuwa hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake, walimwomba Pilato amuue.
29 Ya anae macumple todo ayo y esta matugue pot güiya, machule papa guinin y jayo, ya mapolo gui jalom y naftan.
Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye, walimshusha kutoka mtini na kumlaza kaburini.
30 Lao si Yuus munacajulo guinen y manmatae:
Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
31 Ya malie megae na jaane ni ayo sija y mangachochongña mangajulo guinin Galilea para Jerusalem, ni y pago testiguña sija gui taotao.
Alionekana kwa siku nyingi kwa wale waliokwenda pamoja naye kutoka Galilaya kuelekea Yerusalemu. Watu hawa sasa ni mashahidi wa watu.
32 Ya jame chumule guiya jamyo y mauleg na notisia, ni ayo na promesa y mafatinas gui mañaena,
Hivyo tunawaletea habari njema kuhusu ahadi walizopewa mababu zetu.
33 Jaftaemano si Yuus cumunple guiya jita, ni y famaguonñija, sa ayonae janacajulo si Jesus talo; taegüije locue y esta matugue gui mina dos gui Salmos: Jago y Lajijo ya pago na jaane nae julilis jao.
Mungu aliweka ahadi hizi kwetu, watoto wao, katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai. Hili pia liliandikwa katika Zaburi ya pili: 'Wewe ni Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako'
34 Ya ninacajulo guinin y manmatae, ya pago ti utalo guato gui minitong guinin jasangan taegüine: Guajo junae jao ni y santos yan magajet na bendisjon David.
Pia kuhusu ukweli ni kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi: 'Nitakupatia utakatifu na baraka halisi za Daudi'
35 Enaomina ilegña locue y otro Salmo: Na chamo pumopolo y Santosmo na ulie y minitong.
Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine, 'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'
36 Sa si David anae munjayan jasetbe y generasionña pot y pinagat Yuus, maego ya mapolo manafandaña yan y mañaenaña, ya jalie y minitong.
Kwa kuwa baada ya Daudi kutumikia mapenzi ya Mungu katika kizazi chake, alilala, alilazwa pamoja na baba zake, na aliuona uaharibifu,
37 Lao ayo y ninacajulo as Yuus talo ti jalie minitong.
Lakini aliyefufuliwa na Mungu hakuuona uharibifu.
38 Ya umatungo guiya jamyo mañelo lalaje, na pot este na taotao na mapredidica guiya jamyo y inasiin y isao:
Hivyo na ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi umehubiriwa.
39 Ya pot güiya na todo ayo y jumonggue manunas ni todo y güinaja, sa ti siña jamyo manunas, pot y lay Moises.
Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki na mambo yote ambayo sheria ya Musa isingewapatia haki.
40 Adaje na nosea ufato guiya jamyo, y masangan gui profeta sija;
Hivyo basi kuweni waangalifu kwamba kitu walichokiongelea manabii kisitokee kwenu:
41 Estagüe, jamyo ni y manmañatlilie, yan infanmanman, yan infanmalingo. Sa machochochoyo ni y checho y jaanemniyo, ayo na chocho y ti injengue, ni jaye na taotao unaclaro guiya jamyo.
'Tazama, enyi mnaodharau, na mkashangae na mkaangamie; kwa vile nafanya kazi katika siku zenu, Kazi ambayo hamwezi kuiamini, hata kama mtu atawaeleza.”
42 Ya anae manjuyong gui sinagoga, jagagao na umapredica este na sinangan guiya sija gui siguiente sabado.
Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka, watu wakawaomba waongee maneno haya siku ya Sabato ijayo.
43 Ya anae manadingo y inetnon gui sinagoga, megae na Judios yan y deboto na proselito sija dumalalag si Pablo yan Barnabé; ni y sumangangane siga yan jaeepogna ufañaga gui grasian Yuus.
Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha, Wayahudi wengi na waongofu thabiti waliwafuata Paulo na Barnaba, ambao waliongea nao na waliwahimiza waendelee katika neema ya Mungu.
44 Ya y siguiente sabado canaja todo y taotao y siuda mandaña para ujajungog y sinangan Yuus.
Sabato iliyofuata, karibu mji mzima ulikusanyika kusikia neno la Mungu.
45 Lao anae jalie y Judios y linajyan taotao, manbula linatga, ya manguentos contra ayo y sinangan Pablo ya jachatfino contra si Yuus.
Wayahudi walipoona makutano, walijawa na wivu na kuongea maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo na walimtukana.
46 Ayonae si Pablo yan Barnabé jausa y minatatngañija, ilegñija: Nesesita ayo y sinangan Yuus ni y esta manmasangane jamyo finena, lao pot innasuja guiya jamyo, injisganmaesa jamyo na ti dignojamyo y taejinecog na linâlâ, ya estagüe na tabirajit para y Gentiles. (aiōnios g166)
Lakini Paulo na Barnaba waliongea kwa ujasiri na kusema, “Ilikuwa ni muhimu kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu. Kwa kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele, angalieni tutawageukia Mataifa. (aiōnios g166)
47 Sa taegüenao tinagoña si Yuus nu jita, ilegña: Jupolo jamyo para candet y Gentiles, na jamyo siña para satbasion asta y uttimon patte y tano.
Kama ambavyo Bwana ametuamuru, akisema, 'Nimewaweka ninyi kama nuru kwa watu wa mataifa, kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia.”
48 Ya anae jajungog este y Gentiles, ninafansenmagof, ya maalaba y sinangan Yuus: ya megae manmanjonggue ni ayo sija y manmatancho para y taejinecog na linâlâ. (aiōnios g166)
Mataifa waliposikia hili, walifurahi na kulisifu neno la Bwana. Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele waliamini. (aiōnios g166)
49 Ya machalapon y sinangan Yuus todo güije na tano.
Neno la Bwana lilienea nchi yote.
50 Lao y Judio sija, janafangalamten y mandebota yan y manonra na famalaoan, yan y manmagas na taotao sija gui siuda, ya janafangajulo pinetsigue contra si Pablo yan Barnabé, ya janafanmayute juyong gui tanoñija.
Lakini wayahudi waliwasihi waliojitoa na wanawake muhimu, pia na viongozi wa mji. Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na waliwatupa nje ya mipaka ya mji.
51 Lao sija, jasacude y petbos gui adengñija contra sija, ya manjanao para Iconio.
Lakini Paulo na Barnaba walikung'uta vumbi ya miguu yao. Kisha walienda kwenye mji wa Ikonia.
52 Ya y disipulo sija, manbula minagof yan y Espiritu Santo.
Na wanafunzi walijawa na furaha pamoja na Roho mtakatifu.

< Y Checho Y Apostoles Sija 13 >