< اَلْمَزَامِيرُ 150 >

هَلِّلُويَا. سَبِّحُوا ٱللهَ فِي قُدْسِهِ. سَبِّحُوهُ فِي فَلَكِ قُوَّتِهِ. ١ 1
Msifuni Bwana. Msifuni Mungu katika patakatifu pake, msifuni katika mbingu zake kuu.
سَبِّحُوهُ عَلَى قُوَّاتِهِ. سَبِّحُوهُ حَسَبَ كَثْرَةِ عَظَمَتِهِ. ٢ 2
Msifuni kwa matendo yake makuu, msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
سَبِّحُوهُ بِصَوْتِ ٱلصُّورِ. سَبِّحُوهُ بِرَبَابٍ وَعُودٍ. ٣ 3
Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,
سَبِّحُوهُ بِدُفٍّ وَرَقْصٍ. سَبِّحُوهُ بِأَوْتَارٍ وَمِزْمَارٍ. ٤ 4
msifuni kwa matari na kucheza, msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,
سَبِّحُوهُ بِصُنُوجِ ٱلتَّصْوِيتِ. سَبِّحُوهُ بِصُنُوجِ ٱلْهُتَافِ. ٥ 5
msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
كُلُّ نَسَمَةٍ فَلْتُسَبِّحِ ٱلرَّبَّ. هَلِّلُويَا. ٦ 6
Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana. Msifuni Bwana!

< اَلْمَزَامِيرُ 150 >