< مَرَاثِي إِرْمِيَا 5 >
اُذْكُرْ يَارَبُّ مَاذَا صَارَ لَنَا. أَشْرِفْ وَٱنْظُرْ إِلَى عَارِنَا. | ١ 1 |
Kumbuka, Ee Bwana, yaliyotupata, tazama, nawe uione aibu yetu.
قَدْ صَارَ مِيرَاثُنَا لِلْغُرَبَاءِ. بُيُوتُنَا لِلْأَجَانِبِ. | ٢ 2 |
Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni, na nyumba zetu kwa wageni.
صِرْنَا أَيْتَامًا بِلَا أَبٍ. أُمَّهَاتُنَا كَأَرَامِلَ. | ٣ 3 |
Tumekuwa yatima wasio na baba, mama zetu wamekuwa kama wajane.
شَرِبْنَا مَاءَنَا بِٱلْفِضَّةِ. حَطَبُنَا بِٱلثَّمَنِ يَأْتِي. | ٤ 4 |
Ni lazima tununue maji tunayokunywa, kuni zetu zapatikana tu kwa kununua.
عَلَى أَعْنَاقِنَا نُضْطَهَدُ. نَتْعَبُ وَلَا رَاحَةَ لَنَا. | ٥ 5 |
Wanaotufuatilia wapo kwenye visigino vyetu, tumechoka na hakuna pumziko.
أَعْطَيْنَا ٱلْيَدَ لِلْمِصْرِيِّينَ وَٱلْأَشُّورِيِّينَ لِنَشْبَعَ خُبْزًا. | ٦ 6 |
Tumejitolea kwa Misri na Ashuru tupate chakula cha kutosha.
آبَاؤُنَا أَخْطَأُوا وَلَيْسُوا بِمَوْجُودِينَ، وَنَحْنُ نَحْمِلُ آثَامَهُمْ. | ٧ 7 |
Baba zetu walitenda dhambi na hawapo tena, na sisi tunachukua adhabu yao.
عَبِيدٌ حَكَمُوا عَلَيْنَا. لَيْسَ مَنْ يُخَلِّصُ مِنْ أَيْدِيهِمْ. | ٨ 8 |
Watumwa wanatutawala na hakuna wa kutuokoa mikononi yao.
بِأَنْفُسِنَا نَأْتِي بِخُبْزِنَا مِنْ جَرَى سَيْفِ ٱلْبَرِّيَّةِ. | ٩ 9 |
Tunapata chakula chetu kwa kuhatarisha maisha yetu kwa sababu ya upanga jangwani.
جُلُودُنَا ٱسْوَدَّتْ كَتَنُّورٍ مِنْ جَرَى نِيرَانِ ٱلْجُوعِ. | ١٠ 10 |
Ngozi yetu ina joto kama tanuru, kwa sababu ya fadhaa itokanayo na njaa.
أَذَلُّوا ٱلنِّسَاءَ فِي صِهْيَوْنَ، ٱلْعَذَارَى فِي مُدُنِ يَهُوذَا. | ١١ 11 |
Wanawake wametendwa jeuri katika Sayuni, na mabikira katika miji ya Yuda.
ٱلرُّؤَسَاءُ بِأَيْدِيهِمْ يُعَلَّقُونَ، وَلَمْ تُعْتَبَرْ وُجُوهُ ٱلشُّيُوخِ. | ١٢ 12 |
Wakuu wametungikwa juu kwa mikono yao, wazee hawapewi heshima.
أَخَذُوا ٱلشُّبَّانَ لِلطَّحْنِ، وَٱلصِّبْيَانَ عَثَرُوا تَحْتَ ٱلْحَطَبِ. | ١٣ 13 |
Vijana wanataabika kwenye mawe ya kusagia, wavulana wanayumbayumba chini ya mizigo ya kuni.
كَفَّتِ ٱلشُّيُوخُ عَنِ ٱلْبَابِ، وَٱلشُّبَّانُ عَنْ غِنَائِهِمْ. | ١٤ 14 |
Wazee wameondoka langoni la mji, vijana wameacha kuimba nyimbo zao.
مَضَى فَرَحُ قَلْبِنَا. صَارَ رَقْصُنَا نَوْحًا. | ١٥ 15 |
Furaha imeondoka mioyoni mwetu, kucheza kwetu kumegeuka maombolezo.
سَقَطَ إِكْلِيلُ رَأْسِنَا. وَيْلٌ لَنَا لِأَنَّنَا قَدْ أَخْطَأْنَا. | ١٦ 16 |
Taji imeanguka kutoka kichwani petu. Ole wetu, kwa maana tumetenda dhambi!
مِنْ أَجْلِ هَذَا حَزِنَ قَلْبُنَا. مِنْ أَجْلِ هَذِهِ أَظْلَمَتْ عُيُونُنَا. | ١٧ 17 |
Kwa sababu hiyo, mioyo yetu inazimia, kwa sababu ya hayo, macho yetu yamefifia,
مِنْ أَجْلِ جَبَلِ صِهْيَوْنَ ٱلْخَرِبِ. ٱلثَّعَالِبُ مَاشِيَةٌ فِيهِ. | ١٨ 18 |
kwa ajili ya Mlima Sayuni, ambao unakaa ukiwa, nao mbweha wanatembea juu yake.
أَنْتَ يَارَبُّ إِلَى ٱلْأَبَدِ تَجْلِسُ. كُرْسِيُّكَ إِلَى دَوْرٍ فَدَوْرٍ. | ١٩ 19 |
Wewe, Ee Bwana unatawala milele, kiti chako cha enzi chadumu kizazi hadi kizazi.
لِمَاذَا تَنْسَانَا إِلَى ٱلْأَبَدِ وَتَتْرُكُنَا طُولَ ٱلْأَيَّامِ؟ | ٢٠ 20 |
Kwa nini watusahau siku zote? Kwa nini umetuacha kwa muda mrefu?
اُرْدُدْنَا يَارَبُّ إِلَيْكَ فَنَرْتَدَّ. جَدِّدْ أَيَّامَنَا كَٱلْقَدِيمِ. | ٢١ 21 |
Turudishe kwako mwenyewe, Ee Bwana, ili tupate kurudi. Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale,
هَلْ كُلَّ ٱلرَّفْضِ رَفَضْتَنَا؟ هَلْ غَضِبْتَ عَلَيْنَا جِدًّا؟ | ٢٢ 22 |
isipokuwa uwe umetukataa kabisa na umetukasirikia pasipo kipimo.