< Titus 2 >

1 Bara nani febele ilemon iyina nin ti pipin ticine.
Inakupasa kufundisha itikadi sahihi.
2 Anit akune suu anan kifuu batiitikune anan yenju upi, uyinu sa uyenua anan suu, nin nanan ciu nayi.
Wafundishe wazee kuwa na kiasi, wastahivu, wenye busara na wanyofu katika imani, upendo na saburi.
3 Awani akune inin wang nanere iso anan nakpinati, na anan kubelin ba. Naniwa suu acin kitin nssu turo b. Na idursuzo ilemong na idi gigime
Vivyo hivyo, wafundishe wanawake wazee kuwa na mwenendo wa utakatifu, wala wasiwe wasingiziaji au walevi, bali wafundishe yale yaliyo mema,
4 bara ina taa awni abebene isu dert nanya kpilzu mer, iti nani likara nibinai iti usuu nales mine nang nono isoo anang yeju ipiit.
ili waweze kuwafundisha wanawake vijana kuwa na kiasi, wawapende waume zao na kuwapenda watoto wao,
5 Nlau anang lisosin licine ndarrti isau anan nanku nati nin nales mine bara uliru Kutelle wa so imong infillu
wawe waaminifu, watakatifu, wakitunza vyema nyumba zao, wema, watiifu kwa waume zao, ili mtu yeyote asije akalikufuru neno la Mungu.
6 Nanere tutung beleng azamane iso anan kpilzunupiit.
Vivyo hivyo, himiza vijana wawe na kiasi.
7 nanya nimong vat durum atee mine nafo anan katwa ka cine; iwa dursuzu durung nlau durung tikune, nin tigbulang tine tin salin yenu.
Katika kila jambo uwe kielelezo kwa kutenda mema. Katika mafundisho yako uonyeshe uadilifu, utaratibu,
8 Belen pipinghe tuu na ti na so sa ukye, bara tina soo nin cin kitene nle na aba tifi mayarda, bara nani na imenmun inanzan duku na iba benlu nati bite ba.
na usemi sahihi usio na lawama, ili wanaokupinga watahayari, wakose neno lolote baya la kusema juu yetu.
9 Acin ba suu unaku nati kit nacinilarimine idertin inan poo nani nibina, na iwa sa mayardan nan ghinu ba.
Wafundishe watumwa kuwatii mabwana zao katika kila jambo, wakijitahidi kuwapendeza wala wasijibizane nao,
10 Na iwa su nani likiri b, bara nani na idursu nni uyinu sa uyen, bara inan taa udursuzu bite mbelen Kutelle unan tucu bite kuna niyizi nanya tibau vat.
wala wasiwaibie, bali waonyeshe kuwa wanaweza kuaminika kabisa, ili kwa kila namna wayafanye mafundisho ya Mungu Mwokozi wetu yawe ya kuvutia.
11 Iyen, ubolu Kutelle na uma dak nin tucu udu nanit vat.
Kwa maana neema ya Mungu ambayo inawaokoa wanadamu wote imefunuliwa.
12 Unin dursuzu nani ti nari imon inanzang nin kunanizi nimun iyi ti suu anan kujijin, anit alau nin libau Kutelle nanya ku kuje. (aiōn g165)
Nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia, ili tupate kuishi maisha ya kiasi, ya haki na ya utaua katika ulimwengu huu wa sasa, (aiōn g165)
13 Na ti din ncaa ti saru nin nayi aboo dak ngongon udiya Kutelle bit nin Yesu Kristi unan tucu.
huku tukilitazamia tumaini lenye baraka na ufunuo wa utukufu wa Mungu wetu Mkuu, aliye Mwokozi wetu Yesu Kristo.
14 Yesu wa ni liti mee bara arik tinan se ulau kusain nuzu na lapibit tinin soo lau kitime, alena a ceu nibinai nsu nimon icine
Ndiye alijitoa nafsi yake kwa ajili yetu, ili atukomboe kutoka uovu wote na kujisafishia watu kuwa mali yake Mwenyewe, yaani, wale walio na juhudi katika kutenda mema.
15 Beleng ni likara kibinai ni le mone nin te nke nin tigoo vat na imong wa nari minu ba.
Basi wewe fundisha mambo haya. Onya na kukaripia kwa mamlaka yote. Mtu yeyote asikudharau.

< Titus 2 >