< Uruyan Yuhana 2 >

1 “Udu kiti ngono kadura Kutelle kilari nlira in Afisawa nyertine: 'Uliru nlenge na a min iyini kuzore ncara ulime me. Ule na adin cinu nan nya tica nla nizinariya kuzore nworo nenge,
“Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
2 “Meng yiru imon ile na una suu nin katwaa nijasi fe ayi asheu nin teru kibinai fe, ana fe wa sa uso ligowe nin na nan katwaa kananzang ba, uminin na dumun alenge na idin su inung nono kadura, a na nanere yi ta ba, inanin se nani nin kinuu.
Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
3 Meng yiru nsheu nteru kibinai fe, umini na neo kang bara lisa ning, a na una lanza kudirya ba.
Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
4 Vat nani ndi nin nimon nivira nin fi, bara na una sun usuu nburnu fe.
Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
5 Lizino kiti kanga na una diu ku. Suna kulapi fe usu imon ile na una suzu nin burne. A se na ucino likara li nanza fe ba, in wang dak mba da kalu kuca nle kitene.
Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
6 Bara na udi nin lele, udin shina nile imon na an Nikolitiya na su, ile wang na meng nari.
Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
7 Andi udi nin kutuf, lanza imon ile na Uruhu din bellu nilari nliru Kutelle. Ule na a leo likume mba yinunghe ali kucan lai, ko na kudi kipin tigo Kutelle'.
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
8 “Udu kitin gono kadura Kutelle kilarin nlira in Sumaniya nyertine: Ulelere uliru nlenge na awa di nburnue nin ni maline, ulenge na awa ku amini na ti ulai tutung:
“Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
9 “Meng yiru uniu nin likimon fe. (amma udin nin se), nin wulsu na lenge na idininsu innung a Yahudawari (a na naniere ba, ina dii kilarin nlirun Shaitanghari).
Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
10 Na iw a lanza fiu nile imon na iba niu mung ba. Yenen! Kugwergenue din cinu u tuu among mine nan nya kilari licin inan dumun minu, iba niu nan nya nayiri li kure. Yitan ni nayi a kone uduru ukul, meng ma ni minu Litappa nlai.
Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
11 Andi udi nin kutuf, lanza imon ile na Uruhu din belu ninlari nliru Kutell. e Ulenge na aleo likumme na ukul nmba ba seghe ba.
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
12 “Cindu udura nikilisiyan Perigamum nyerte: 'Tuo nye re ttigulan nlengee na adi nin kisangali nlikang nasariaba:
“Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: “Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
13 “'Myen yiru kika na usosin ku-kika na lichur nshaitan nnghari. Vat nani umiin lisa nighye parrt, na usuu nntala nni kibinai fye nmi ba, wan nin nya nayirin Antipas iyizin yenu ning, unan liyisin nanya ninghe, nai wa mdu nan ninghe, kikanye na shaitan sosinku.
Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
14 Nya nani ndi ning nimon baat ugan ninf: Udi ning namon na imiin gangan madudurzun Balaam, na awa duro Balak ku a filo kutalan tiru nbun nnonon Isruila, unang sye ilyeu imon nli njuju uhem nna kwu tichil inin su nzemzem nmulsu.
Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
15 Libau lirumere, i di ning na le wan na imiin gangan madudursuzu na Nikolainiyawa.
Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
16 Kwilzinan, nanere! An nanari ba, mba dak nfi dyedei, mba dak nin su likum kitenye minye ning kisangali na ki nuzu nanya nnuu ning.
Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
17 Asa udi nin kutuf, lanza imeile na unangwaru din belu ikilisiyai. Cindu nlengyye na a lyeu, mba nyinghe ummong u manna nau nyeshin, nning ninghye litala libau ning lisa lipesye na i nyertinye kutalye, lisa lo na umon yiru ba nngiwaa unan serye rye yiru.
“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
18 “Cindu udura ilisiyan Thyatira nyertine: 'Alenge nye rye agwulan Nsaun Kutelleh, ulenge na iyizi mye di fuo lilyem nnla nin nabunu nafuo ikoroishine na, na weltin:
“Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: “Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
19 “'Nyire imoilee na umai ti. Usuu fye nin ntikibinai nin katwa nin terun nkotunu, wan nin nimoile na una worin nsu ikata in cizinue.
Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
20 Nin nyanani ndi nin nimon nnari kitene fye: U yinna nin wani unye Jezebel, na adinsu amye uwa nanan nyenju nimon nchinu. Nnya madursudurzu mye, adin rusuzu a cin nnin isuu nzemnzen nmulsu nin nnli nimonnli nainakwa tichil.
Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
21 Nna nnighye kubi a kwilin, na a yinna a kwilin ba a suun nzemzem nye ba.
Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
22 Yenje! Menba filu nnghe unonku ro nkonu, nin na lenge na ichindin nmolsu nanghe cin piru nijasi idya, ankuru na i kwilla nnuzu nimon nsu mye ba.
Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
23 Mbaa dazunu nonomye ikuzu, vat niklisiyai ba nin yinnu ning woru myeri din piziru nibinai nin na nyanti nimon. Mba nnyi vat nlenge na asuu imon ile na unit risuu.
Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
24 Nanyere kagisin minye nnyan Thyatira, cindu vat na lye na isali sa u minnu madursuzu ma nye, inin tani imoile na idinsu muun imon ichancham nshaitan-udu nnghinu ndinsu, 'Na myen ba kwin minu nmong nugetyek ku ba.'
“Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
25 Sa isu nnyiziari, uba minuarye part uchicha cin dak nin.
Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
26 Ulenge na alyeu nin iye na suu imoilye na myen nsuu cindu liganghe, cindu nghe mba nyi likalin kityenye timinn.
“Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
27 'Amye ba sun tigo kityeneminye nin ncha fikoro, fuo a dul tiwing a baa puchua ni chinchwun.
Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
28 Na fuo na nsere kitin Ncif nin, mme wang ba nnighe fibir.
Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
29 Asa u di nin kutuf, lanza imoile na unangwaru din bellu Iklisiyai.'
“Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!

< Uruyan Yuhana 2 >