< Uruyan Yuhana 18 >

1 Na ile imone wakat vat uwa yene kan gono kadura Kutelle ntulsu cin dak nnuzu kitene kani. A wa di nin likara lidya, uye wa li kanang nin gongon mye.
Baada ya vitu hivi nilimwona malaika mwingine akishuka chini kutoka mbinguni. Yeye alikuwa na mamlaka kuu, na nchi iliangazwa kwa utukufu wake.
2 A taa ntyet nin liwui lidya, abenle, “Udewu, udewu ubabalila udiyai a so kitin lisosin na gbergenu, kiti lisosin vat ti ruhu ti nanzang nin kiti lisosin vat kijin kuzenzen.
Alilia kwa sauti kuu, akisema, “Umeanguka, umeanguka, ule mji mkuu Babeli! Umekuwa sehemu yakaapo mapepo, na sehemu ikaapo kila roho chafu, na sehemu akaapo kila mchafu na ndege achukizaye.
3 Nipinpin ne vat nsono ntoro nzina mye na mina da ninghe tinana nayi. Ago nyii nasu uzina ninghe. Anan malesulesa nanya nyii so anan nimon na cara bara likara lisosin limang mye.”
Kwa kuwa mataifa yote yamekunywa mvinyo ya tamaa ya uasherati wake ambayo humletea ghadhabu. Wafalme wa nchi wamezini naye. Wafanyabiashara wa nchi wamekuwa matajiri kwa nguvu ya maisha yake ya anasa.”
4 Nlanza nlon liwui nnuzu ketene kani nworo, “Nuzun nanya mene, anit ning, bara i wa seru imemun inanzan mye.
Kisha nilisikia sauti nyingine kutoka mbinguni iikisema, “Tokeni kwake watu wangu, ili msije mkashiriki katika dhambi zake, na ili msije mkapokea mapigo yake yoyote.
5 Alapi mye malkulu udu kitene kani, Kutelle nin katwa ka nanzan mye.
Dhambi zake zimerundikana juu kama mbingu, na Mungu ameyakumbuka matendo yake maovu.
6 Kurtunghe ku imon na ame na su anite, kurtwaghe ku tiba iman ile na ana kurtuz anite ku; nanya kakup ka na awa ketelin, ketelenghe ti ba.
Mlipeni kama alivyowalipa wengine, na mkamlipe mara mbili kwa jinsi alivyotenda; katika kikombe alichokichanganya, mchanganyishieni mara mbili kwa ajili yake.
7 Nafo na ana ghantin liti mye anin su mang, naghe gbardang uniu nin tunana naye. A woro nanya kibinai mye, 'Nsosin nafo ushono ngo; Na meng unan diru nlisari ba, na iwa yenu kibinai kisirnebai.
Kama alivyojitukuza yeye mwenyewe, na aliishi kwa anasa, mpeni mateso mengi na huzuni. Kwa kuwa husema moyoni mwake, 'Nimekaa kama malkia; wala siyo mjane, na wala sitaona maombolezo.'
8 Bara nani imon inanzan mye ma se ghe: ukull, lisosin nayi asirne, nin kukpon. Ula ma liighe.”
Kwa hiyo ndani ya siku moja mapigo yake yatamlemea: kifo, maombolezo, na njaa. Atateketezwa kwa moto, kwa kuwa Bwana Mungu ni mwenye nguvu, na ni mhukumu wake.”
9 Agon yee na ina su uzina ninghe inani na nuzu insalin lanzun niliru ninghe ima gilu nin ghe i wa yene mcin nli nla mye din ghanju.
Wafalme wa nchi waliozini na kuchanganyikiwa pamoja naye watalia na kumwombolezea watakapouona moshi wa kuungua kwake.
10 I ma yisinupiit, idin lanzu fiyu nniyu mye, mbenlu, “Kash, kash udu kipin ki diya, Babila, kipin llikara! Nanyan kube kurun uniu fe ndaa.”
Watasimama mbali naye, kwa hofu ya maumivu yake wakisema, “Ole, ole kwa mji mkuu, Babeli, mji wenye nguvu! Kwa saa moja hukumu yako imekuja.”
11 Anan malesulesu nye gila nin lisosin nayi asirne bara ame, bara na umong ma kuru asere imon nlesu mye tutung ba-
Wafanyabiashara wa nchi lieni na kuomboleza kwa ajili yake, kwa kuwa hakuna hata mmoja anunuaye bidhaa zake tena -
12 Imon lesu ni zinariyanin, nin nazurfa, nin natola nikurfung, nin luu-luu, nin liniw ukpekpet, nin nimon nmyein nafo, nin siliki, nin malufi vat nin naca nikurfuung, nin vat nishik nicaut, nin fikoro fishine, nin fikoro fisirne nin mabil,
bidhaa za dhahabu, fedha, mawe ya thamani, lulu, kitani nzuri, zambarau, hariri, nyekundu, aina zote za miti ya harufu nzuri, kila chombo cha pembe za ndovu, kila chombo kilichotengenezwa kwa miti ya thamani, shaba, chuma, jiwe,
13 nin fikoro, nin animon, nin turare, nin mai kuya kunang, nin lubar, nin alkama, nin nina, nin nakam, nin nibark, nin karusa, nin nacin, nin ti lai na nit.
mdalasini, viungo, uvumba, manemane, ubani, mvinyo, mafuta, unga mzuri, ngano, ng'ombe na kondoo, farasi na magari, na watumwa, na roho za watu.
14 Ku mat na ca ko na una din nin serwe i wulu fi. Vat mmang fe nin nimon fo figiri i nana kiti fe, na ima kuru ise inin tutung ba.
Matunda uliyoyatamani kwa nguvu zako yameondoka kutoka kwako. Anasa zako zote na mapambo yametoweka, hayatapatikana tena.
15 Ale na i wa din nlesu nile imone se ikurfung kang bara usu mye yisina piit ninghe bara fiiyu nniyu mye, kuculu nin tiit nayi asirne.
Wafanyabiashara wa vitu hivi waliopata utajiri kwa mapenzi yake watasimama mbali kutoka kwake kwa sababu ya hofu ya maumivu yake, wakilia na sauti ya maombolezo.
16 I ma woro, “Kash, kash nin kipin ki diya kane na ki wa su kuyuk nin ni ninoon icene, nanya nimon nmyein nafa, nin kye kidowome nin nizinariya, nin nimoon natuf nikurfung nin luu-luu.”
Wakisema, “Ole, ole mji ule mkuu uliovikwa kitani nzuri, zambarau, na nyekundu, na kupambwa kwa dhahabu, na vito vya thamani na lulu!”
17 Nanya kube kurum vat nilele imoon nikurfunghe nana. Vat nanan con njirgi myeen, vat nanang cin nanya njirgi myeen, nin na le na i din sessu imonli nanyan kurawa ku dundya we, yisina piit.
Ndani ya saa moja utajiri wote huo ulitoweka. Kila nahodha wa meli, kila baharia, na wote wanamaji, na wote wafanyao kazi baharini, walisimama mbali.
18 I taa ntest na iyene incin nli nla mye. I woro, “Kiyeme kipinari masin fo ka kipin ki dya?”
Walilia walipouona moshi wa kuungua kwake. Walisema, “Ni mji gani unafanana na mji huu mkubwa?”
19 i tiza lidao nidowo mene, inin taa nteet, ning myiziin mi gbagbai nin lisosin tiyoom, “Kash, kash udu kipin kidya kane ki kaa na vat nale na i di nin tijirgin myen kurawa kudin dya nda se ikurfun ku unuzun dukiya mye. Bara na nanya kubi kurum ida nanza ghe.”
Walitupa mavumbi juu ya vichwa vyao, na walilia, wakitokwa machozi na kuomboleza, “Ole, ole mji mkubwa mahali wote waliokuwa na meli zao baharini walikuwa matajiri kutokana na mali zake. Ndani ya saa moja umeangamizwa.”
20 “Taan liburi liboo bara ameh, kitene kani, anung anit alau, anang kaduran Yesu, nin nanan liru nin nuu Kutelle, bara na Kutelle nda nin mawucu wuce mye lite mye!”
“Furahini juu yake, mbingu, ninyi waumini, mitume, na manabii, kwa maana Mungu ameleta hukumu yenu juu yake!”
21 Unan katwa Kutelle yira litala nafo litala tiyazung a too linin nanya kurawa kudya we, a benle, “Nanya nlo libau ule, uBabila, kipin kidya, i ma fillu kutyein nin tinana nayi na i ma kuru i yene tutung ba.
Malaika mwenye nguvu aliinua jiwe kama jiwe kuu la kusagia na alilitupa baharini, akisema, “Kwa njia hii, Babeli, ule mji mkuu, utatupwa chini kwa ukatili na hautaonekana tena.
22 Ti wui nanang foo nidowo, anang navu, anan pee nishiriya, nin nanang wulsu na langtung na i ma kuru ilanza nani. Nanya fe ba na i ma kuru i se anang makeke nimon nanya fe tutung ba. Na ima kuru i lanzan tiyazun nanya fe tutung ba.
Sauti ya vinanda, wanamuziki, wacheza filimbi, na tarumbeta hawatasikika tena kwenu. Wala fundi wa aina yoyote hataonekana kwenu. Wala sauti ya kinu haitasikika tena kwenu.
23 Nkanan nla ma bicu na ima kuru iyene mining tutung ba. Liwui na wanlapese nang na lese na ima kuru ilanza tutun ba, bara na imoon nlesu fe wadi ashoono na goo nyii, nin myin uwa rusuzu nani ning niyuu fe.
Mwanga wa taa hautaangaza ndani yako. Sauti ya bwana harusi na bibi harusi hazitasikiwa tena ndani yako, maana wafanyabiashara wako walikuwa wakuu wa nchi, na wa mataifa, wamedanganywa kwa uchawi wako.
24 Nanya mye i wa se nmyii nanang liru ning nuu Kutelle nin nanit a lau, ning myii na le na i wa mulsu nani nanya nyii.”
Ndani yake damu ya manabii na waamini ilionekana, na damu ya wote waliouawa juu ya nchi.”

< Uruyan Yuhana 18 >