< Filibiya 1 >

1 Bulus nin Timitawus, acin Kristi Yesu, udu kiti nalenge vat na ina ceo ani ugan nanya Kristi Yesu arika na idin Pilippi, nin nadidya a a Dikons.
Waraka wa Paulo na Timotheo, watumishi wa Kristo Yesu: Kwa watakatifu wote katika Kristo Yesu walioko Filipi, pamoja na waangalizi na mashemasi:
2 Na ubolu Kutelle yita nanghinu nin lissosin liman unuzu kiti Kutelle Ucifbit nin Cikilari Yesu Kristi.
Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
3 Ndin su Kutelle ning ugodo vat kubi ko nan lizino ninghinu.
Ninamshukuru Mungu wangu kila niwakumbukapo ninyi.
4 Kolome liri nanyan lira nin bara anunghe vat, nanya liburi libowari asa nta nlira.
Katika maombi yangu yote daima nimekuwa nikiwaombea ninyi nyote kwa furaha,
5 Ndin nin godo uzursu mine nanyan liru umang ucizunue udak nene.
kwa sababu ya kushiriki kwenu katika kueneza Injili, tangu siku ya kwanza hadi leo.
6 Indi nin likara kibinayi kitene nimon ilele, nworu ame ulenge na acizina katwa kacine nanya mine ma lii ubun amalu kani udu lirin Yesu Kristi.
Nina hakika kwamba yeye aliyeianza kazi njema mioyoni mwenu, ataiendeleza na kuikamilisha hata siku ya Kristo Yesu.
7 Ucaun menku nlanza nani kitenen vat mine bara idinin ninghinu nya nayining. Anung vat wadi ninmi nanya bolu Kutelle nin licin ning tutung nin kesu litining a upunu libaun liru umang.
Ni haki na ni wajibu wangu kufikiri hivi juu yenu nyote, kwa sababu ninyi mko moyoni mwangu. Ikiwa nimefungwa au nikiwa ninaitetea na kuithibitisha Injili, ninyi nyote mnashiriki neema ya Mungu pamoja nami.
8 Bara Kutelleri iyizi inba ning, ninworu kolome liri ayedi nyene minu vat nanya kulin nsuu Kristi Yesu.
Mungu ni shahidi wangu jinsi ninavyowaonea shauku ninyi nyote kwa huruma ya Kristo Yesu.
9 Tutung meng din lira mone: nworu usuu mine na kulo gbardang nanyan yiru nin yinnu.
Haya ndiyo maombi yangu: kwamba upendo wenu uongezeke zaidi na zaidi katika maarifa na ufahamu wote,
10 Meng din lira mone bara fe nanse uciro unin fere imon ile na idi icine. Idin bara fenan yita nin kidegen sa kulapi lirin Kirsti.
ili mpate kutambua yale yaliyo mema, mkawe safi, wasio na hatia hadi siku ya Kristo,
11 ilenge imone di nani tutung fe nan kulo nin niburi katwa kacine na kadin dasu nanyan Yesu Kristi, udun gongon nin zazunu Kutelle.
mkiwa mmejawa na matunda ya haki yapatikanayo kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa za Mungu.
12 Nene ayedi iyinnin linuana, nworu imon ile na iwasesue, ina nakpin ulinbun katwa in liru umanghere kang.
Basi, ndugu zangu, nataka mjue kwamba mambo yale yaliyonipata kwa kweli yamesaidia sana kueneza Injili.
13 Udi nani bara tiseleng nin nanya Kristi kogha nayiru mun nanya kowe anan caa nin koyeme unit wang.
Matokeo yake ni kwamba imejulikana wazi kwa walinzi wote wa jumba la kifalme na kwa wengine wote kuwa nimefungwa kwa ajili ya Kristo.
14 Tutung gbardang linuana nanya Kristi nase ukpilu bara tiseleng ninghere nin se likaran bellu lire sa fiu.
Kwa sababu ya vifungo vyangu, ndugu wengi katika Bwana wametiwa moyo kuhubiri neno la Mungu kwa ujasiri zaidi na bila woga.
15 Amon kidegen ina bellu ubelle Kristi nin shina a nnung, among tutung bara usuu nibinayi nilau mine.
Ni kweli kwamba wengine wanamhubiri Kristo kutokana na wivu na kwa kutaka kushindana, lakini wengine wanamhubiri Kristo kwa nia njema.
16 Alenge na idin bellu Kristi ku nanya suu yirru ina tikikane bara ukessu liru umanghere.
Hawa wa mwisho wanamhubiri Kristo kwa moyo wa upendo, wakifahamu kwamba nimo humu gerezani kwa ajili ya kuitetea Injili.
17 Ama among din bellu Kristi unuzun sunati nin kpilzun diru kidegen. Inung dinsu idin kpizunu mengku kabun nanya tiseleng ning.
Hao wa kwanza wanamtangaza Kristo kutokana na tamaa zao wenyewe wala si kwa moyo mweupe, bali wanakusudia kuongeza mateso yangu katika huku kufungwa kwangu.
18 Se inyang? Kolome libau, sa nanya kinu sa kidegen, idin bellu Kristi ku, tutung nanya nilele indi nayi abo! E e, nmasu ayiabo.
Lakini inadhuru nini? Jambo la muhimu ni kwamba kwa kila njia, ikiwa ni kwa nia mbaya au njema, Kristo anahubiriwa. Nami kwa ajili ya jambo hilo ninafurahi. Naam, nami nitaendelea kufurahi,
19 Bara inyirru ile imone ma dak nin buntu ning. Nani mayitu bara nlira mine nin bunu Ruhun Kristi.
kwa maana ninajua kwamba kwa maombi yenu na kwa msaada unaotolewa na Roho wa Yesu Kristo, yale yaliyonipata mimi yatageuka kuwa wokovu wangu.
20 Bara likaran ceo nayi nighari tutung kidegen na nma lanzu ncin ba. Imone wang manani likara kibinayiari, nafo kolome liri, nin nene wang, idin ceo nayi Kristi se ughatinu nanya kidowo ning, sa nanyan lai sa nkul.
Ninatarajia kwa shauku kubwa na kutumaini kwamba sitaaibika kwa njia yoyote, bali nitakuwa na ujasiri wa kutosha ili sasa kama wakati mwingine wowote, Kristo atukuzwe katika mwili wangu, ikiwa ni kwa kuishi au kwa kufa.
21 Bara usoo nin lai Kristiari, a ukul tutung ulinbunari.
Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo, na kufa ni faida.
22 Ama adin lissosin nin lai kidowo din maccu niburi nanya katwa ning, nan yirru uyemeri in ma feru ba.
Kama nitaendelea kuishi katika mwili, kwangu hili ni kwa ajili ya matunda ya kazi. Lakini sijui nichague lipi? Mimi sijui!
23 Bara vat inodini nin to tiyenje. Idi nin konnayi nworu nnyan diso nin Kristi, urika na ukatin vat ulele!
Ninavutwa kati ya mambo mawili: Ninatamani kuondoka nikakae pamoja na Kristo, jambo hilo ni bora zaidi.
24 Tutung inso nanya kidowe macaunu bara anunghe.
Lakini kwa sababu yenu ni muhimu zaidi mimi nikiendelea kuishi katika mwili.
25 Nene na indinin likara kibinayi kitene nimon ilele, inyirru nwo nma lawu nlii ubun nanghinu vat, bara ulinbun nin nayi abo mine nanya yinnu sa uyene.
Kwa kuwa nina matumaini haya, ninajua kwamba nitaendelea kuwepo na kuwa pamoja nanyi nyote, ili mpate kukua na kuwa na furaha katika imani.
26 Imanin se idi gogon nanyan Kristi Yesu bara meng, imase nani bara uyitu ning nanya mine.
Ili kwamba furaha yenu iwe nyingi katika Kristo Yesu kwa ajili yangu kwa kule kuja kwangu kwenu tena.
27 Anun dei minon tilai mine libau longo na ima yenu Kristi ku. Sun nani nwo, ko meng dak inda yenne minu, sa nin sali ninghe, ibata nlanza uyissunu gangan mine nanyan Ruhu urum. Indi nin suu nlanza idi kidowo kirum nfokidowo ligowe nanya yinnu sa uyenun liru umanghe.
Lakini lolote litakalotukia, mwenende kama ipasavyo Injili ya Kristo, ili kwamba nikija na kuwaona au ikiwa sipo, nipate kusikia haya juu yenu: Kuwa mnasimama imara katika roho moja, mkiishindania imani ya Injili kwa umoja,
28 Tutung yenje fiu wa daminu bara vat nimon ilenge na anan nivira din sue. Ilele kiti mine kulap nkul minere. Ama kiti mine, kulap ntuccu minere, tutung ilele kiti Kutelleri.
wala msitishwe na wale wanaowapinga. Hii ni ishara kwao kuwa wataangamia, lakini ninyi mtaokolewa, na hii ni kazi ya Mungu.
29 Bara kiti mine ina mallu uniminu, bara Kristi, na nwo iyinin nighe cas ba, ama tutung iniu bara ame.
Kwa maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, bali pia kuteswa kwa ajili yake,
30 Bara idi nin mayardang marum mane nafo manga na ina yene kiti ning, tutung ilanza ndumun nene.
kwa kuwa mnashiriki mashindano yale yale mliyoyaona nikiwa nayo na ambayo hata sasa mnasikia kuwa bado ninayo.

< Filibiya 1 >