< Filibiya 2 >

1 In ma yinnu nwo unizu likara nanya Kristi duku. Inma yinnu nwo usoo mang unuzun suume. Inma yinnu nwo ligo nin Ruhu duku. Inma yinnu nwo nkunekune mi cancom nin suun bunu duku.
Ikiwa kuna kutiwa moyo katika Kristo. Ikiwa kuna faraja kutoka katika pendo lake. Ikiwa kuna ushirika wa Roho. Ikiwa kuna rehema na huruma.
2 Tan ayiabo nin kulo nin kpiluzu urum ulele, iyitta nin suu urume, inin yita nin munu ati nanya Ruhu, anin suu nsu nimon irume.
Ikamilisheni furaha yangu kwa kunia mamoja mkiwa na upendo mmoja, mkiwa wamoja katika roho, na kuwa na kusudi moja.
3 Yenje iwasu imonimon bara usuu nati sa ukpilizu unanzang. Na nonkon atime iyenje among nafo ikatin minu.
Msifanye kwa ubinafsi na majivuno. Isipokuwa kwa unyenyekevu mkiwaona wengine kuwa bora zaidi yenu.
4 Yenje iwa kpiliza ubelle nimon ile na idi ninsuwe cas, ama kpilizang imon su namong wang.
Kila mmoja wenu asiangalie tu mahitaji yake binafsi, bali pia ajali mahitaji ya wengine.
5 Kpilizang libau longo na lidi lin Kristi Yesu wang.
Muwe na nia kama aliyonayo Kristo Yesu.
6 Awa yitta nin kulap Kutelle, ama na awa yaun lissosin me nin Kutelle nafo imon ilenge na ame ma minu ba.
Ingawaje yeye ni sawa na Mungu. Lakini hakujali kuwa sawa na Mungu ni kitu cha kushikamana nacho.
7 Awa na wese litime nya liti. Ayauna kulap kucin. Anuzu nin kidowon nit usurne. Iwa seghe nin yenju nafo unit.
Badala yake, alijishusha mwenyewe. Alichukua umbo la mtumishi. Akajitokeza katika mfano wa wanadamu. Alionekana mwanadamu.
8 Awa toltin litime aso una dortun liru udun kul, ukul un kitene kuca.
Yeye alijinyeyekeza na kuwa mtii hadi kifo, kifo cha msalaba.
9 Bara nani Kutelle uni wa ghantighe. Awa ninghe lissa ubun kolome lissa.
Hivyo basi Mungu alimtukuza sana. Alimpa jina kuu lipitalo kila jina.
10 Awa tinane bara nanya lissa Yesu vat nalung ma tumnu, alung nalenge na idi kitene kani nin kutiin a nanya kutiin.
Alifanya hivyo ili kwamba katika jina la Yesu kila goti sharti liiname. Magoti ya walio mbinguni na walio juu ya ardhi na chini ya ardhi.
11 Awa sunani tutung bara kolome lilem ma punu abellin Yesu Kristi Cikilareri, udun gongon Kutelle Ucif.
Na alifanya hivyo ili kwamba kila ulimi sharti ukiri kwamba Yesu kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
12 Bara nani, anan suuning, nafo na idin dortu kolome liri, na se meng duku ba, ama nene gbardang ka nin salininghe, sun katwa ntuccu mine nin fiu nin ketuzu kiti.
Kwa hiyo basi, wapendwa wangu kama mnavyotii siku zote, Si tu katika uwepo wangu lakini sasa ni zaidi sana hata pasipo uwepo wangu, uwajibikeni wokovu wenu wenyewe kwa hofu na kutetemeka.
13 Bara Kutelleri di katwa nanya mine vat nin yinnu a usu katwa bara nmang me.
Kwa kuwa ni Mungu anayetenda kazi ndani yenu ili kuwawezesha kunia na kutenda mambo yale yampendezayo yeye.
14 Sun ko iyapin imon sa ugbondulu sa mayardang.
Fanyeni mambo yote bila malalamiko na mabishano.
15 Sun katwa nin nile imone inan so sa alapi nin nono kidegen Kutelle sa indinon. Sun katwa nin nile imone bara inan balta nafo nkanang nanya yii, kitik kuji ku kwarkwok nin dirun fiu Kutelle.
Fanyeni hivyo ili kwamba msilaumike na kuwa watoto wa Mungu waaminifu wasiyo na lawama. Fanyeni hivyo ili kwamba muwe nuru ya dunia, katika kizazi cha uasi na uovu.
16 Minon gangan tigbulan nlai bara inan se imon ile na imati gongon lirin Kristi. Kubere nmanin yinnu na nnasu uccum sa katwa kahem ba.
Shikani sana neno la uzima ili kwamba niwe na sababu ya kutukuza siku ya Kristo. Kisha nitafahamu kwamba sikupiga mbio bure wala sikutaabika bure.
17 Ama ko igutuni nafo unakpu ulau nanyan ni liti nin katwa in yinnu sa uyenu mine, idin su ayiabo, nkuru nsu ayiabo nanghinu vat.
Lakini hata kama ninamiminwa kama sadaka juu ya dhabidhu na huduma ya imani yenu, ninafurahi, na ninafurahi pamoja nanyi nyote.
18 Nanya nimon irume, anung wang dinayi abo, a iyitta nayi abo nin mi wang.
Vilevile na ninyi pia mnafurahi, na mnafurahi pamoja nami.
19 Ama ndin cisu kibinayi kitin Cikilari Yesu a tuu Timitawus ku nayiri alele, meng wang nase likara asa nlaza nbelle mine.
Lakini natumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo kwenu hivi karibuni, ili kwamba niweze kutiwa moyo nitakapojua mambo yenu.
20 Bara na ndi nin mong tutung nafo ame ba, urika na adi nin nayi acine bara anunghe.
Kwa kuwa sina mwingine aliye na mtazamo kama wake, mwenye nia ya kweli kwa ajili yenu.
21 Bara vat mine din pizuru imon nati minere, na imon Yesu Kristi ba.
Wengine wote ambao ningewatuma kwenu wanatafuta mambo yao binafsi tu, na siyo mambo ya Yesu Kristo.
22 Ama fe yiru imon ile na adi, nafo na gono asa asuu ucife katwa, nanenere ame di katwa nin mi nanya nlirun laiye.
Lakini mnaijua thamani yake, kwa sababu kama mtoto anavyomhudumia baba yake, ndivyo alivyotumika pamoja nami katika injili.
23 Ndin kpilizu ntuughe na nin molu kubi ba asa in yene ucin nimone kiti ninghe.
Kwa hiyo ninatumaini kumtuma haraka pindi tu nitakapofahamu nini kitatokea kwangu.
24 Ama ndi ni kibinayi kirum nin Cikilari nworu meng liti ninghe wang ma dak na nin dadaunu ba.
Lakini nina hakika katika Bwana kwamba mimi mwenyewe pia nitakuja hivi karibuni.
25 Ama inyene ukifo gbas ntuu Epaparoditus ku ukpillu kiti mine. Ame gwana nighari nin don katwa ning udu likum ning, a gono kadura nin kucin nsuu ning.
Lakini nafikiri ni muhimu kumrejesha kwenu Epafradito. Yeye ni ndugu yangu na mtenda kazi mwenzangu na askari mwenzangu, mjumbe na mtumishi wenu kwa ajili ya mahitaji yangu.
26 Bara awa lanza kuyamine kang, amini wa yita ni suu awadi amal zuru nan ghinu vat, anung na lanza na adi ucine ba.
Kwa sababu alikuwa na hofu na alitamani kuwa pamoja nanyi nyote, kwa kuwa mlisikia kwamba alikuwa mgonjwa.
27 Nanere, awa su kidowo kang nafo aba ku. Ama Kutelle na lanza nkunekune me, a na ame usamme ba, umunju mengku wang bara nwa se liburi lisirne kitene liburi lisirne.
Maana hakika alikuwa mgonjwa sana kiasi cha kufa. Lakini Mungu alimhurumia, na wema huo haukuwa juu yake tu, lakini pia ulikuwa juu yangu, ili kwamba nisiwe na huzuni juu ya huzuni.
28 Nene nkipina usuu nworu ntuughe, bara andi iyeneghe tutung imanin yitu nin nayiabo ima kalu njirjir nibinayi mine.
Kwa hiyo ninamrejesha kweny haraka iwezekanavyo, Ili kwamba mtakapomwona tena mpate kufurahi na mimi nitakuwa nimeondolewa wasi wasi.
29 Seren Epaporoditus ku nin naburi abo nanyan Cikilari. Taan anit nafo ame ngongong.
Mkaribisheni Epafradito katika Bwana kwa furaha zote. Waheshimuni watu kama yeye.
30 Bara kitene katwan Kristiari awa lantin uku. Awa nari ulai me anan suyi katwa nin kulunu katwa kanga nafe wa yinnin usue ba nanyaa katwa ninghe.
Kwa kuwa ilikuwa kwa ajili ya kazi ya Kristo kwamba alikaribia kufa. Alihatarisha maisha yake ili kuniokoa mimi na akafanya kile ambacho hamkuweza kufanya katika kunihudumia mimi kwa mko mbali nami.

< Filibiya 2 >