< Luka 22 >

1 Nene ubukin burodin salin nimon infizwe da susut, ule na idin yecu kata natibite.
Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa chachu, iitwayo Pasaka, ilikuwa inakaribia.
2 Adidya kutiin nliara nan nanang niyert soo ikpilza na ima kifu Yesu ku imulughe, bara na iwadin nlanzu fiu na nite.
Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakawa wanatafuta njia ya kumwua Yesu, lakini waliwaogopa watu.
3 Shetan pira nanya Yahuda Iskariyot, owarum nanya likure nin naba me.
Basi, Shetani akamwingia Yuda aitwae Iskarioti, mmoja wa wale mitume kumi na wawili.
4 Yahuda du idi kpilza nang na didya kutii nlira nang nanan niyert na ma nakpu Yesu ku nacara mene.
Yuda akaenda akajadiliana na makuhani wakuu na walinzi wa Hekalu kuhusu atakavyomsaliti Yesu kwao.
5 I lanzan nmang, inin yina imanighe ikurfung.
Nao wakafurahi na kupatana naye kumlipa fedha.
6 Ayina, a nin din piziru nimon baat na ama tii ananakpaghe anit wa yinin.
Yuda akakubali, na akawa anatafuta nafasi nzuri ya kumkabidhi kwao bila umati wa watu kujua.
7 Lirin nborodi sa imon fitize da, na uso doleari inakpa kukam nhadaya.
Basi, siku ya Mikate Isiyotiwa chachu ikafika. Hiyo ndiyo siku ambayo mwana kondoo wa Pasaka huchinjwa.
8 Yesu too Bitrus nin Yohana ku, a benle “Can idi kanja nari imonlin kalu nati bite, bara tinan lau ining.”
Hivyo Yesu akawatuma Petro na Yohane, akawaambia, “Nendeni mkatuandalie karamu ili tupate kula Pasaka.”
9 I tiringhe, “Inweri udin nin sun woro ti di su lakanjwe ku?”
Nao wakamwuliza, “Unataka tuiandae wapi?”
10 Akawa nani, “I wa piru nanya kipine, umon na a yauna ka suu nmyen ma zuru minu, dufinonghe udu kilari kaa na apira nanye.
Akawaambia, “Sikilizeni! Mtakapokuwa mnakwenda mjini, mtakutana na mwanamume anayebeba mtungi wa maji. Mfuateni mpaka ndani ya nyumba atakayoingia.
11 I benle Cikilari kilare, 'Kumallami benle nari, “Kutii na mare dinweri, inweri nba lii imonlin kahu nate nwere nin nono katwa ninghe?”'
Mwambieni mwenye nyumba: Mwalimu anakuuliza, kiko wapi kile chumba ambamo nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu?
12 A ma duru minu kuti ko na I malu kyelu kudya. Kun kitene, kanjan imonle kikane.”
Naye atawaonyesheni chumba kikubwa ghorofani ambacho kimepambwa. Andalieni humo.”
13 I do, I di se vat nmoonghe na abenle nani. Inin kele kiti keleuwa.
Basi, wakaenda, wakakuta kila kitu sawa kama Yesu alivyokuwa amewaambia; wakaandaa karamu ya Pasaka.
14 Na kube ndaa, a so nan nono katwa me.
Saa ilipotimia, Yesu akakaa kula chakula pamoja na mitume wake.
15 A nin woro nani, “Indi nin su nwadi inmalu nlii imonlui ilele nanghinu uworu min niyu.
Akawaambia, “Nimetamani sana kula Pasaka hii pamoja nanyi kabla ya kuteswa kwangu.
16 Bara nan belin minu, na inma kuru nli nan ghinu tutun ba, saidai ikulu nanya kilari tigoo Kutelle.”
Maana nawaambieni, sitaila tena hadi hapo itakapokamilika katika Ufalme wa Mungu.”
17 Yesu nin yira ukoop, na ata ugodiya, a woro, “Seren I kosu nati mine.
Kisha akatwaa kikombe, akashukuru akasema, “Pokeeni, mgawanye ninyi kwa ninyi.
18 Bara nan mbelin minu, na mba kuru nsumo ko kumati kuce kune tutun ba, se kipin tigoo Kutelle ndaa.”
Kwa maana nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka Ufalme wa Mungu utakapokuja.”
19 A nin yira uborodi, na ana ugodiya ku, afucu unin, anin naa nani, abenle, “Kidowa nunghere kane kaa na nna ni bara anung. Sun nene I lizizin nin me.”
Halafu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa akisema, “Huu ni mwili wangu, unaotolewa kwa ajili yenu. Fanyeni hivi kwa kunikumbuka.”
20 A kuru ayira ukoope nafo na ani taa na imala kileuwe, abenle, “Ule ukoope likamali nirghari lipese nanga nmii ning, mo na wa gutun bara anung.
Akafanya vivyo hivyo na kikombe, baada ya chakula, akisema, “Kikombe hiki ni agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu inayomwagika kwa ajili yenu.
21 Bara nani yenjen. Ule na alewei adi logowe nin me keetebur kone.
“Lakini, tazameni! Yule atakayenisaliti yuko nami hapa mezani.
22 Bara na Gono nit ma nyeu nafo na ina belin. Bara nani kash nleli unite na amere ina lewughe nacara me!”
Kweli Mwana wa Mtu anakwenda kuuawa kama ilivyopangwa, lakini ole wake mtu anayemsaliti.”
23 I nin cizina utiru nati mene, nghari nanga mene ma su lidungu lone.
Hapo wakaanza kuulizana wao kwa wao ni nani kati yao atakayefanya jambo hilo.
24 Kubung nin fita nanya mene mpeziru ghani ba so udiya nanya mene.
Kulitokea ubishi kati ya hao mitume kuhusu nani miongoni mwao anayefikiriwa kuwa mkuu zaidi kuliko wengine.
25 A woro nani, “Ago na wurme dinin nan cinilare mene, ale na itti nin natek licara udin yicu nani anan tigoo in ruu.
Yesu akawaambia, “Wafalme wa mataifa huwatawala watu wao kwa mabavu, nao huitwa wafadhili wa watu.
26 Bara nani na uma so nani nin ghinu ba, nmaimako nani, na ule na amere udiyawe nanya mine kpilin aso nafo kagono kabene. Na ule na amene idin cisughe iyizi kpilin aso kulin mene.
Lakini isiwe hivyo kati yenu; bali, yule aliye mkuu kati yenu ni lazima awe mdogo wa wote, na aliye kiongozi lazima awe kama mtumishi.
27 Ghari udiyewe, ule na a sosin kitene kutebure sa ule na asu kucin? Na ule na asosin kitene kutibure re ba? Nin nani ndi nanya mene nafo kucin.
Kwa maana, ni nani aliye mkuu: yule anayeketi mezani kula chakula, ama yule anayetumikia? Bila shaka ni yule anayeketi mezani kula chakula! Hata hivyo, mimi niko hapa kati yenu kama mtumishi.
28 Bara nani anughere na I wadi nin me nanya ndumunu ning.
“Ninyi ndio mliobaki nami wakati wote wa majaribu yangu;
29 Mnani minu kipin tigoo, nafo na ucenighe na mo nyii kipin tigowe,
na, kama vile Baba yangu alivyonikabidhi Ufalme, vivyo hivyo nami nitawakabidhi ninyi Ufalme.
30 I nan leu iso kutabur nighe nanya kipin tigoo nighe. Inin so kutet in wucu tilem likure nin tiban Israila.
Mtakula na kunywa mezani pangu katika ufalme wangu, na mtaketi katika viti vya enzi kuyahukumu makabila kumi na mawili ya Israeli.
31 Simon, Simon, yino, Shetan di nin su akifo fi, anan cecile fi nafo ualkama.
“Simoni, Simoni! Sikiliza! Shetani alitaka kuwapepeta ninyi kama mtu anavyopepeta ngano.
32 Bara nani meng mma tifi nlira, bara uyenu nsalin yenu wa dire. Uwadi umalu gitirinu kimal tutung, ta nwana fine likara.”
Lakini mimi nimekuombea ili imani yako isipungue. Nawe utakaponirudia, watie moyo ndugu zako.”
33 Bitrus woroghe, “Ucef, mang ba du ningfi kilari licin nin nkule.”
Naye Petro akamjibu, “Bwana, mimi niko tayari kwenda pamoja nawe gerezani, na hata kufa.”
34 Yesu kawaghe, “Inbelinfi, Bitrus, na ku kuluke ma culsinu ti tat ba, uma benlu na uyiri ba.”
Yesu akamjibu, “Nakwambia wewe Petro, kabla jogoo hajawika leo utakuwa umenikana mara tatu.”
35 Yesu woro nani, “Na awa tuminu sa lijip, nkatizu ni moon, sa akpatak, I wa dira imemoona?” Inin kawa, “Na ti wan dira ba.”
Kisha, Yesu akawauliza wanafunzi wake, “Wakati nilipowatuma bila mfuko wa fedha wala mkoba wala viatu, mlitindikiwa chochote?” Wakajibu, “La.”
36 Anin woro nani, “Bara nani nene, ule na adinin lijip, na a kala linin, tutung nin nkaa ntizu nimoon. Ule na a sali nin kusangali na a leueu kulutukme adi seru kurum.
Naye akawaambia, “Lakini sasa, yule aliye na mfuko wa fedha auchukue; na aliye na mkoba, hali kadhalika. Na yeyote asiye na upanga, auze koti lake anunue mmoja.
37 Bara nan beleng minu, I mon ile na ina yertin litinighe ima kulu gbas, 'I yeneghe nafo unan salin duka.' Bara nani ile iman na iwa beling litinighe din kulusu.”
Maana nawaambieni, haya maneno ya Maandiko Matakatifu: Aliwekwa kundi moja na wahalifu, ni lazima yatimie. Naam, yale yanayonihusu yanafikia ukamilifu wake.”
38 Inin woro, “Ucef, yene! Asangali aba ale.” Anin woro nani, “A batina.”
Nao wakasema, “Bwana, tazama; hapa kuna panga mbili.” Naye akasema, “Basi!”
39 Na ileu imari, Yesu nga, nafo na amene udi litalan Nzaitu, nono katwa mge nin dofinghe.
Yesu akatoka, na kama ilivyokuwa desturi yake, akaenda katika mlima wa Mizeituni; wanafunzi wake wakamfuata.
40 Ma iduru, aworo nani, “taan nlira iwa piru nanyan njaraba.”
Alipofika huko akawaambia, “Salini, msije mkaingia katika kishawishi.”
41 A cacana kupuu mene nafo utuu litala, anin tumuro nin nalung ataa nlira.
Kisha akawaacha, akaenda umbali wa mtu kuweza kutupa jiwe, akapiga magoti, akasali:
42 A benle, “Ucef, wase y yina, kala ukoop ulele litining, min nani na uwa dofin kibinai ning ba, na kin fere so.”
“Baba, kama wapenda, ukiondoe kwangu kikombe hiki; hata hivyo, mapenzi yako yatimizwe, wala siyo yangu.”
43 Unan kadura Kutelle nin daa unuzu kitene kani, a taaghe likara.
Hapo, malaika kutoka mbinguni, akamtokea ili kumtia moyo.
44 Na awaadin niyu, a kpina nlire ku, tinuntu me tantizo kang nafo nmyii na ngutuna kuteen.
Akiwa katika uchungu mkubwa, alisali kwa bidii zaidi; na jasho likamtoka, kama matone ya damu, likatiririka mpaka chini.
45 Na afita unuzun nlire, adaa kitin nono katura me, ada se nani idin moro bara nibinai nisirne mene,
Baada ya kusali, aliwarudia wanafunzi wake, akawakuta wamelala, kwani walikuwa na huzuni.
46 anin tirino nani, “Inyarin taa idin moro? Fitan iti nlira, bara I wa piru ticankira.”
Akawaambia, “Mbona mnalala? Amkeni msali, msije mkaingia katika kishawishi.”
47 Na awa din nlire, iyene, ligozin na nite ndaa, ligowe nin Yahuda, uwarum nanya likure nin nabe, a dewu nbune. Ada kupoon Yesu anan taghe usumba,
Alipokuwa bado anaongea, kundi la watu likaja likiongozwa na yule aliyeitwa Yuda, mmoja wa wale mitume kumi na wawili. Yuda akaenda kumsalimu Yesu kwa kumbusu.
48 bara nani Yesu woroghe, “Yahuda uma lewu Gano nit nin sumbaa?”
Lakini Yesu akamwambia, “Yuda! Je, unamsaliti Mwana wa Mtu kwa kumbusu?”
49 Na ale na I wa killinghe nyene nani, I woro, “Cikilari, ti kewu umong nin kusangalia?”
Wale wanafunzi wake walipoona hayo wakasema, “Bwana, tutumie panga zetu?”
50 Umong nanya mene kewe kucin ndiya nang yenju kutii nlere, kutuf, ncara ulime a nin werne kunin.
Na mmoja wao akampiga upanga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio lake la kulia.
51 Yesu woro, “Naneli mbatina,” a nin dudo kutufe, ku shino.
Hapo, Yesu akasema, “Acha! Hii inatosha.” Akaligusa sikio la mtu huyo akaliponya.
52 Yesu woro udiya nnan yenju kutii nlire, anan ncaa kutiin nlire, nin nadidiya ntardu nacara kutii nlira na iwa dak kiti me nin mayardam, “Idaa nafo anang kifun kiria nin nasangali nan tiyupa?
Kisha Yesu akawaambia makuhani wakuu, wakubwa wa walinzi wa Hekalu na wazee waliokuja kumkamata: “Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kana kwamba mimi ni mnyang'anyi?
53 Na uwadi nan ghinu nanya kutii nlire vat lire, na umong myene nakpa ucara liti nighe ba bara nenere kubi myene, nin likara nsirti.”
Nilipokuwa pamoja nanyi kila siku Hekaluni hamkunitia nguvuni. Lakini, huu ndio wakati wenu hasa, ndio wakati wa utawala wa giza.”
54 Na I kifoghe, I yaa nin ghe, I duu ninghe kilari ndya kutii nlire. Bara nani Bitrus difino nani piit.
Basi, wakamkamata, wakamchukua na kwenda naye nyumbani kwa Kuhani Mkuu. Petro akawa anamfuata nyuma kwa mbali.
55 Na I suso ula nanya kudarwe inin so ligowe idin lanzwe, Bitrus soo nanya myene.
Moto ulikuwa umewashwa katikati ya ua, nao wakawa wameketi pamoja Petro akiwa miongoni mwao.
56 Nkan kabera kucin yeneghe a sosin nkanang nlee, ayene iyizemye anin woro, “Ule unite nyita ligowe nanghe.”
Mjakazi mmoja alipomwona Petro ameketi karibu na moto, akamkodolea macho, akasema, “Mtu huyu alikuwa pia pamoja na Yesu.”
57 Bara nani Bitrus ta mayardan ku, aworo, “Uwani nan yirughe ba.”
Lakini Petro akakana akisema, “Wee! simjui mimi.”
58 Na idandouna ba, umong kuru ada yeneghe, a woro, “Fe wang di nan ghinu.” Bara nani Bitrus woro, “Unit, na meyari ba.”
Baadaye kidogo, mtu mwingine akamwona Petro, akasema, “Wewe ni mmoja wao.” Lakini Petro akajibu “Bwana we; si mimi!”
59 Na ita kubiri kubi umong unit kuru ada woro, “Kedegene unit ulelen yita nin ghe, bara ane kunan Galiliari.”
Kama saa moja baadaye, mtu mwingine akasisitiza, “Hakika huyu alikuwa pamoja naye; ametoka Galilaya ati.”
60 Bara nani Bitrus woro, “Unit nang yiru imon ile na udin belu ba.” Na aduu inlire kukulok kolsuno.
Lakini Petro akasema, “Bwana wee; sijui hata unachosema!” Na papo hapo, akiwa bado anaongea, jogoo akawika.
61 Na a kpilia umuro me, Cikilare yene Bitrus ku, Bitrus nin lizino imon ile na Cikilare nni belinghe, na aworoghe, “Na kukulok ma kulsinu titat ba uma woro na uyirwui ba.”
Bwana akageuka na kumtazama Petro, naye Petro akakumbuka yale aliyokuwa ameambiwa na Bwana: “Leo kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
62 Na a nuzu udas, Bitrus gila kang.
Hapo akatoka nje, akalia sana.
63 Anite na iwa din caan Yesu su ghe liyong inin fooghe.
Wale watu waliokuwa wanamchunga Yesu, walimpiga na kumdhihaki.
64 Na ituswughe iyizi, itininghe i woro, “Su anabci, ghari ulenge na areofi?”
Walimfunga kitambaa usoni, wakawa wanamwuliza, “Ni nani aliyekupiga? Hebu bashiri tuone!”
65 I bele imon gbardang litin Yesu, izoguzo ghe.
Wakamtolea maneno mengi ya matusi.
66 Na kitin shanta, a kukune na nite da pitiruno ligowe. Umunu adidya na priest nin na nan ni nyerte. I pira nin ghe kudaru nwuchun liru,
Kulipokucha, kikao cha wazee wa watu kilifanyika, ambacho kilihudhuriwa na makuhani wakuu na walimu wa Sheria. Yesu akaletwa mbele ya Baraza hilo.
67 iworo, “Andi fere Kriste, belle nari.” Ama a woro nana, “Asa nbelling minu, na ima yinnu ba,
Nao wakamwambia, “Twambie! Je, wewe ndiwe Kristo?” Lakini Yesu akawaambia, “Hata kama nikiwaambieni, hamtasadiki;
68 asa meng tirin minu, na ima kawu ba.
na hata kama nikiwaulizeni swali, hamtanijibu.
69 Ama ucizunu nene udu ubun, Gono nit ma so ncara uline unlikara Kutelle.”
Lakini tangu sasa, Mwana wa Mtu atakuwa ameketi upande wa kulia wa Mungu Mwenyezi.”
70 Vat mine woro, “Ani fera Gono Kutelle?” Yesu woro nani, “Anughere nworo mere.”
Hapo wote wakasema, “Ndiyo kusema wewe ni Mwana wa Mungu?” Naye akasema, “Ninyi mnasema kwamba mimi ndiye.”
71 I woro, “Iyaghari nta tidu nin su nnan ba? Bara arik nin nati bite nlanza nnu me.”
Nao wakasema, “Je, tunahitaji ushahidi mwingine? Sisi wenyewe tumesikia akisema kwa mdomo wake mwenyewe.”

< Luka 22 >