< Luka 16 >

1 Yesu kuru a woro nono katwa me, “Umong unan nikurfung wadi nin nang tamani me, ida belinghe unang yeujun ntamanie din nanzu unis.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake: “Tajiri mmoja alikuwa na karani wake. Huyu karani alichongewa kwamba alitumia ovyo mali ya tajiri wake.
2 Unan nikurfughe yicila ghe aworoghe, 'I yanghari ndin lanze litife? Daa uda nyii kibatiza nimon ile na nwa nili uyenje bana na fe unit ucineari ba.'
Yule tajiri akamwita akamwambia: Ni mambo gani haya ninayosikia juu yako? Toa hesabu ya mapato na matumizi ya mali yangu, kwa maana huwezi kuwa karani tena.
3 Unan yenjughe ntamane woro letime, 'I yanghari mbati nin litining, I yanghari mba ti, bara na cikilari nighe ma kalu katwa kane nacara nighe? Na indi nin likava mawuzu wuzu ba, tutung indi lanzu incin kufili.
Yule karani akafikiri: Bwana wangu amenifukuza kazi ya ukarani; nitafanya nini? Kwenda kulima siwezi; kwenda kuombaomba kama maskini ni aibu.
4 In yiru imon ile na mba ti, bara na lwa kala katwa kane nacara nighe, anit ma sesui ngamine.'
Naam, najua la kufanya, ili nitakapofukuzwa kazi, watu waweze kunikaribisha nyumbani kwao.
5 Unan yeujun ntamane yicila vat nale na cikilare din durtu nami tire, anin tirino unan burne, 'Imashinari cikilare din durtu fi?'
Basi, akawaita wadeni wa bwana wake, mmoja mmoja, akamwambia yule wa kwanza: Unadaiwa kiasi gani na bwana wangu?
6 A woro, 'A mudu akut likure nnuf kuca.' Anin waroghe 'Soo mas, kibatiza fe kaa, u nyertin akut ataun.'
Yeye akamjibu: Mapipa mia ya mafuta ya zeituni. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, keti haraka, andika hamsini.
7 Unang yeuju ntamane woro mmong, 'I mashinari idin durtufi?' A woro, 'A mudu akut likure nialkama.' A woroghe 'Kibatiza fe kanga yertina akut likure sa aba.'
Kisha akamwuliza mdeni mwingine: Wewe unadaiwa kiasi gani? Yeye akamjibu: Magunia mia ya ngano. Yule karani akamwambia: Chukua hati yako ya deni, andika themanini.
8 Unan nikurfughe taghe njah bara na awa su katwa me caut ba, bara na nono nyii ulele di nin nibinai nsu nimon icine bara anit mime ba na nafo nonon nkananghe di. (aiōn g165)
“Basi, yule bwana akamsifu huyo karani asiye mwaminifu, kwa kuwa alitumia busara. Kwa maana watu wa dunia hii wana busara zaidi na mambo yao kuliko watu wa mwanga.” (aiōn g165)
9 In belin fi, pizira adondong bara litife nin nimon nyii, bara I wa nyaa ima pirizin fi nanya nilari mi ne. (aiōnios g166)
Naye Yesu akaendelea kusema, “Nami nawaambieni, jifanyieni marafiki kutokana na mali ya dunia, ili zitakapowaishieni, mweze kupokewa nao katika makao ya milele. (aiōnios g166)
10 Ule na adi nin yinnu-sa-uyenu nanya nimon baat ade nin yinnu-sa-uyenu nanya ni dya, ule na adi nin salin yinnu-sa-uyenu nanya ni baat na ama yitu nin yinnu-sa-uyenu nanya nimon idya ba.
Yeyote aliye mwaminifu katika mambo madogo, atakuwa mwaminifu katika mambo makubwa; na yeyote asiye mwaminifu katika mambo madogo, hatakuwa mwaminifu katika mambo makubwa.
11 Bara nani, andi na udi nin yinna-sa-uyenu nimoon inyii ba, ghari ba yinnu ninfi nin nimoon kidegene?
Kama basi, ninyi si hamjawa waaminifu mali mbaya za dunia, ni nani atakayewakabidhi zile mali za kweli?
12 Nanere, andi na udi nin yinnu-sa-uyenu kitene kuturan mong ba, ghari ma nifi ile na idi infe?
Na kama hamjakuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewakabidhi mali yenu wenyewe?
13 Na kucin wasaa amyino an cin nilara naba kubi kurume ba, sa a ma nari umong ati usun mmong, sa a su umong katwa amari usun mmong, na u wasa usu Kutelle licin nin tamani kubi kurume ba.”
“Hakuna mtumishi awezaye kuwatumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au ataambatana na mmoja na kumdharau mwingine. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.”
14 Afarsayawe na i wadi anam su nikurfunghari, I lanza ule ulire vat, itunna nsisu ghe.
Lakini Mafarisayo waliposikia hayo, kwa vile wao walikuwa wanapenda sana fedha, wakamdharau Yesu.
15 A woro nani, “Idin suzu kidegen mine niyizi nanitari, bara nani Kutelle yiru nibinai mine. Ileli imon na idin ruu ining idi zemzem nizi Kutelle.
Hapo akawaambia, “Ninyi mnajifanya wema mbele ya watu, lakini Mungu anaijua mioyo yenu. Kwa maana kile kinachoonekana kuwa kitukufu mbele ya watu, Mungu anakiona kuwa takataka.
16 Uduka nin nanan liru nin nuu Kutelle wa di, Yohana nin daa. Unuzun koni kubi udu sa ligang, uliru Kutelle idim belun nin, vat nanit din shoo ati nanya ti bau ti bau.
“Sheria na maandishi ya manabii vilikuweko mpaka wakati wa Yohane mbatizaji. Tangu hapo, Ufalme wa Mungu unahubiriwa, na kila mmoja anauingia kwa nguvu.
17 Bara nani ukatin nin sauki nworu kitene kani nin kadas kata nin waru fiyert firum nanyan nliru me ikala sa uti kinuu.
Lakini ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita, kuliko hata herufi moja ya Sheria kufutwa.
18 Vatin nlenge na akoo uwani me ayira umong adin nozu nin na wani ahem, nanere uwani ule na akoo ules me aminin di yira umong adin nozu nin les uhem.
“Yeyote anayemwacha mke wake na kuoa mwingine, anazini; na yeyote anayemwoa mwanamke aliyepewa talaka, anazini.
19 Umong unan nikurfung wa duku na iwa shonghe imoon icine anin din lanzun mmang vat liri nanya ntamani udya.
“Palikuwa na mtu mmoja tajiri, ambaye alikuwa anavaa mavazi ya bei kubwa sana ya rangi ya zambarau, na ya kitani safi, na kufanya sherehe kila siku.
20 Umong unan kufilli nunnu kibulung me nin nanut kidowo me.
Kulikuwa pia na maskini mmoja jina lake Lazaro, aliyekuwa amejaa vidonda na alikuwa analazwa mlangoni pa nyumba ya huyo tajiri.
21 A wadin su a li mbubun nimon li na idin disu kuteen, banin nani, ninau nin din lelu anut kidowo me.
Lazaro alitamani kula makombo yaliyoanguka kutoka meza ya tajiri; na zaidi ya hayo, mbwa walikuwa wanakuja na kulamba vidonda vyake!
22 Usuo inlong liyiri unam kufille kuu anan kadura Kutelle da yiraghe udu abunu Ibrahim. Unam nikurfughe wang kuu ikasaghe.
“Ikatokea kwamba huyo maskini akafa, malaika wakamchukua, wakamweka karibu na Abrahamu. Na yule tajiri pia akafa, akazikwa.
23 Nanyan nla, adin niu, a fiya iyisi me ayene Ibrahim ku piit nin Liazaru figiri me. (Hadēs g86)
Huyo tajiri, alikuwa na mateso makali huko kuzimu, akainua macho yake, akamwona Abrahamu kwa mbali na Lazaro karibu naye. (Hadēs g86)
24 A fiya liwai me aworo, 'Ibrahim ucif lanza nkune-kune ning utuu Liazaru ku, a diti liyicin me nanyan myen adak ada tii limila cancam, indin niu namyan nla ulele.'
Basi, akaita kwa sauti: Baba Abrahamu, nionee huruma; umtume Lazaro angalau achovye ncha ya kidole chake katika maji, auburudishe ulimi wangu, maana ninateseka mno katika moto huu.
25 Bara nani Ibrahim woro, 'Gono kubin laife uwa seru imon icine nlaife, Liazaru sere imon inanzang. Bara nani itaghe insheu kibinai kikane, fe tutung uniu.
Lakini Abrahamu akamjibu: Kumbuka mwanangu, kwamba ulipokea mema yako katika maisha, naye Lazaro akapokea mabaya. Sasa lakini, yeye anatulizwa, nawe unateswa.
26 Banin nani kuwu kudya nkese nari bara na alenge na ima kafinu udu kiti fe na iwasa i kafina ba, a na umong wasa a kafina udak kiti bite ba.
Licha ya hayo, kati yetu na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wanaotaka kuja kwenu kutoka huku wasiweze, wala wanaotaka kutoka kwenu kuja kwetu wasiweze.
27 Unan nikurfughe woro, 'Ndin foo fi nacara, Ibrahim ucif. U tuughe udun ngan cif nighe.
Huyo aliyekuwa tajiri akasema: Basi baba, nakuomba umtume aende nyumbani kwa baba yangu,
28 Bara na idi nin nwana inung nataun bara anan wunno nani atuf, bara iwa dak imus kitin niu kaane tutung.'
maana ninao ndugu watano, ili awaonye wasije wakaja huku kwenye mateso.
29 Bara nani Ibrahim woro, 'Idi nin Musa nan nanan liru nin nuu Kutelle; na ilanza nani.'
Lakini Abrahamu akamwambia: Ndugu zako wanao Mose na manabii; waache wawasikilize hao.
30 Unan nikurfunghe kpana aworo, 'na nanere ba, Ibrahim ucif, bara nani iwase umong ulenge na aba du kitimene nanya nabi, I ma kpiliu nibinai mine.'
Lakini yeye akasema: Sivyo baba Abrahamu, ila kama mtu atafufuka kutoka wafu na kuwaendea, watatubu.
31 Bara nani Ibrahim woroghe, 'Andi na ima lanzu Musa ku nan nanan liru nin nuu Kutelle ba, na ima lanzu umong tutung ba sa afita nanya nani.'”
Naye Abrahamu akasema: Kama hawawasikilizi Mose na manabii, hawatajali hata kama mtu angefufuka kutoka wafu.”

< Luka 16 >