< Katwa Nono Katwa 26 >

1 Agrippa woro in Bulu ku, “Uwasa usu uliru nin litife” Bulus nakpa ucara me asu uliru nkussu litime.
Basi, Agripa akamwambia Paulo, “Unaruhusiwa kujitetea.” Hapo Paulo alinyosha mkono wake akajitetea hivi:
2 “In yira liti ning unan ayi abo, ugo Agrippa, nsu uliru nighe nbunfe kimone nbelleng nimon ile ena a Yhudawa na belin liti ning;
“Mfalme Agripa, ninajiona mwenye bahati leo kujitetea mbele yako kuhusu yale mashtaka yote ambayo Wayahudi walikuwa wamesema juu yangu.
3 bara fe unan yiraari kitine vat ntanda na Yahudawa nin tiru mine. Ndin tiru fi nworo ulanzai nin nayi ashau.
Hasa kwa vile wewe mwenyewe ni mtaalamu wa desturi za Wayahudi na migogoro yao, ninakuomba basi unisikilize kwa uvumilivu.
4 Kidegere, a Yahudawa vat yiru imusun lissosin longo na nna su a in yita kwanyana nmin nighe nin Ushalima.
“Wayahudi wanajua habari za maisha yangu tangu utoto, jinsi nilivyoishi tangu mwanzo kati ya taifa langu huko Yerusalemu.
5 Innung yiru ucizunighe tutung ucaun inin yinin nworu meng ku farisawari, alenge na idin kpilizu imon hem ba.
Wananifahamu kwa muda mrefu, na wanaweza kushuhudia, kama wakipenda, kwamba tangu mwanzo niliishi kama mmoja wa kikundi chenye siasa kali zaidi katika dini yetu, yaani kikundi cha Mafarisayo.
6 Nene in yissing kikane bara ndin piziru nciu nliru ulenge na kutelle wa ni acifi bite.
Na sasa niko hapa nihukumiwe kwa sababu ninaitumainia ile ahadi ambayo Mungu aliwaahidia babu zetu.
7 Bara nanere akura nnonon Israila na su Kutelle katwa kitik nin lirin nan nya kidegen, arik ani nceo ayi ti duru kite bara ule uciu nayere a Yahudawa nvuroyi, Ugo!
Ahadi hiyo ndiyo ileile inayotumainiwa na makabila kumi na mawili ya taifa letu, wakimtumikia Mungu kwa dhati mchana na usiku. Mheshimiwa mfalme, Wayahudi wananishtaki kwa sababu ya tumaini hilo!
8 Iyaghari nta idin yenju uma konu Kutelle fya anan kul?
Kwa nini ninyi mnaona shida sana kuamini kwamba Mungu huwafufua wafu?
9 Nkon kubi asa nkpilza nsu imon gambalang gbardang kitene lissan Yesu Nnazareth.
Kwa kweli mimi mwenyewe niliamini kwamba ni wajibu wangu kufanya mambo mengi kulipinga jina la Yesu wa Nazareti.
10 Nna su in Urshalima; nwa yaccu anan katwa kacine kilari licin gbardang, nwa seru likara nsu nani kiti ndya na priest iwa molusu nani, asa mere yinna isu nani.
Mambo hayo ndiyo niliyoyafanya huko Yerusalemu. Mimi binafsi, nikiwa nimepewa mamlaka kutoka kwa makuhani wakuu, nilipata kuwatia gerezani wengi wa watu wa Mungu. Nao walipohukumiwa kuuawa, nilipiga kura ya kukubali.
11 Ina tizu nani ineo kang nan nya nilari nlira mine nkuru ntiza nani izoguzu Kutelle. Nwa yita nin tinana nayi nin ghinu kang ndortu nani uduzu mmin das.
Mara nyingi niliwafanya waadhibiwe katika masunagogi yote nikiwashurutisha waikane imani yao. Hasira yangu kwao ilikuwa kubwa hata nikawasaka mpaka miji ya mbali.
12 Na nwa din su nani, Nwa do Udamaska nin yinnu a likara ngo na priest;
“Kwa mujibu huohuo, nilikwenda Damasko wakati mmoja, nikiwa na mamlaka na maagizo kutoka kwa makuhani wakuu.
13 libowe ucin due, nin wui gberere, Ugo, in yene imon nkanan unuzu kitene Kutelle mida mala kiti bite vat umunu alenge na iwa din cin ligowe nan mi.
Mheshimiwa, wakati nilipokuwa njiani, saa sita mchana, niliona mwanga mkubwa kuliko wa jua ukiangaza kutoka mbinguni, ukanizunguka mimi na wale wasafiri wenzangu.
14 na vat bite ndeo kutyen, nlanza liwui nin ti Ibrananci din liru nin mi, 'Shawulu, Shawulu, iyaghari nta udin tizui nneo? Uwa konui men nari.'
Sisi sote tulianguka chini, nami nikasikia sauti ikiniambia kwa Kiebrania: Saulo, Saulo! Kwa nini unanitesa? Unajiumiza bure kama punda anayepiga teke fimbo ya bwana wake.
15 Ntunna nworo, fe ghari, Cikilaria? Cikilare kawa, ' men Yesu ule na udin funu ghe.
Mimi nikauliza: Ni nani wewe Bwana? Naye Bwana akajibu: Mimi ni Yesu ambaye wewe unamtesa.
16 Nene fita uyissin nin nabunu fe; bara ile imonere ndurso liti nighe kitife, nfere fi uso kucin a unan wazi nbell nimon ile na uyiru inin nin nen nin nimon ile na Mma dursu fi iwa dandaun;
Haidhuru, inuka sasa; simama wima. Nimekutokea ili nikuweke rasmi kuwa mtumishi wangu. Utawathibitishia watu wengine mambo uliyoyaona leo na yale ambayo bado nitakuonyesha.
17 mma tucu fi na cara nanite nin na wurme alenge na mma tuu fi ucindu kitimine;
Nitakuokoa na watu wa Israeli na watu wa mataifa mengine ambao mimi ninakutuma kwao.
18 udi pun iyizi mine uti nani ikpilin isun adu nsirti mine udak nan nya nkanang, nan nya likara nshaitan udak likara Kutelle, inan se ukussu nalapi kiti Kutelle, nin gadu ulenge na ina ni ceo nani nin liti nighe nan nya yinnu sa uyenu.'
Utayafumbua macho yao na kuwawezesha watoke gizani na kuingia katika mwanga; watoke katika utawala wa Shetani, wamgeukie Mungu; ili kwa kuamini, wapate kusamehewa dhambi na kuchukua nafasi yao kati ya wale ambao wamepata kuwa watu wa Mungu.
19 Bara nani, Ugo Agrippa, Na nna dira uyinnu nin anabci Kutelle ba;
“Hivyo, mfalme Agripa, sikuweza kuwa mkaidi kwa maono hilo la mbinguni.
20 amma, kiti na lenge na idin Damaska tukuna, nin na nan Urshalima, nin na lenge vat na idi nmin in Yhudiya, a ining awurmi, ndi wazi i sun alapi mine ikpilin kiti Kutelle, isu imon ile na ima dak nin sunu nalapi.
Ila nilianza kuhubiri kwanza kwa watu wa Damasko, halafu kwa wale wa Yerusalemu na nchi yote ya Yudea, na pia kwa watu wa mataifa mengine. Niliwahimiza wamgeukie Mungu na kuonyesha kwa vitendo kwamba wamebadilisha mioyo yao.
21 Bara ile imonere a Yahudawa na kifo nannya kilari nlira inani pizira imolui.
Kwa sababu hiyo, Wayahudi walinikamata nikiwa Hekaluni, wakajaribu kuniua.
22 Kutelle koni na buni udak nene, in yissin nbelin nbun na talaka nin nanit adidya na umong ubeleng ugan ba se ulenge na anan liru nin nuu Kutelle nin Musa na belin uma se;
Lakini Mungu alinisaidia; na hivyo mpaka siku ya leo nimesimama imara nikitoa ushuhuda kwa wote, wakubwa na wadogo. Ninayosema ni yale ambayo manabii na Mose walisema yatatukia;
23 nworu Kristi ma niu gbas, tutng ama yitu unan burnun fitu nan nya nissek anin kuru a durso nkanang kiti na Yahudawa nin na wurmi.
yaani ilimpasa Kristo ateseke na kuwa wa kwanza kufufuka kutoka wafu, ili atangaze kwamba mwanga wa ukombozi unawaangazia sasa watu wote, Wayahudi na pia watu wa mataifa mengine.”
24 Na Bulus nmala ukusu litime, Fastos woro nin liwui gberere, “Bulus uta ilaza; uyiru udya fe nta fi ilaza.”
Paulo alipofika hapa katika kujitetea kwake, Festo alisema kwa sauti kubwa, “Paulo! Una wazimu! Kusoma kwako kwingi kunakutia wazimu!”
25 Amma Bulus woro ghe, “Na ndi nin nilaza ba Fastos unit udya; amma nin nayi akone ndin su liru kidegen nin toltenu liti.
Lakini Paulo akasema, “Sina wazimu mheshimiwa Festo: Ninachosema ni ukweli mtupu.
26 Bara Ugo yiru ubelleng nilenge imone, bara nani, ndi woas nsu nin ghe, bara meng yiru na imonmong nyeshin kiti me ba, bara na ina su ilenge imone likot ba.
Wewe Mfalme unayafahamu mambo haya, kwa hiyo ninaweza kuongea bila uoga mbele yako. Sina mashaka kwamba matukio hayo yanajulikana kwako maana jambo hili halikutendeka mafichoni.
27 Uyinna nin na annabawe, Ugo Agrippa? Ina yiru uyinna nin ghinu.”
Mfalme Agripa, je, una imani na manabii? Najua kwamba unaamini.”
28 Agrippa woro Bulus ku “nan nya kabiri bar uma kpiliu nso unan dortu Kutelle?”
Agripa akamjibu Paulo, “Kidogo tu utanifanya Mkristo!”
29 Bulus woro, “Ndi inlira kiti kutelle, sa nin kabiri bat sa nin kubiri gbardang, na fe usanfi ba, amma umunu alenge na idin lanzui kiti mone, iso nafo mewe, amma na nin ninyang kilari licin ba.
Paulo akamjibu, “Namwomba Mungu kwamba, kwa muda mfupi au mrefu, si wewe tu bali wote wanaonisikia leo wapate kuwa kama nilivyo mimi, lakini bila hii minyororo.”
30 Ugowe tunna a fita ayissina, a udya mine nin Barniki wang fita umuni alenge na iwa sossin ligowe nan ghinu;
Hapo mfalme Agripa, mkuu wa mkoa, Bernike na wale wote waliokuwa pamoja nao, walisimama.
31 na isuna kudarua, itunna nliru nin nanit mine idin su, “Na unit ulele nati nkon kulapi kongo na ku batina ukul so utecu ba.”
Walipokwisha ondoka, waliambiana, “Mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo au kifungo.”
32 Agrippa woro Festus ku, “Iwa sunu unit ulele nda fo na afo acara kitin Kaisar ba.”
Naye Agripa akamwambia Festo, “Mtu huyu angeweza kufunguliwa kama asingalikuwa amekata rufani kwa Kaisari.”

< Katwa Nono Katwa 26 >